KUMEZUKA mtindo wa viongozi na watendaji katika ngazi za chini kudharau imani misimamo ya wakazi mitaani kitu ambacho kinaashiria kuhatarisha umoja na amani nchini.
Baa, vilabu na maeneo mengine ya starehe kwa upande wa Waislamu, Walokole na watu wa dini nyingine wanaopenda kulea watoto wao katika maadili yanayokubalika visijengwe hadi wakazi wote wameridhia.
Serikali za mitaa hazina sauti kuliko wakazi wa mitaa husika. Na uroho na ulafi wa viongozi usiwe chimbuko la kuwageuza wananchi kuwa wavunja sheria na katiba wakati ni viongozi na mabwana zao ndio wanaovunja katiba.
Kwa mfano hili la ujenzi wa baa na vilabu vya starehe na ngono ovyo ovyo kila mahala kiasi kwamba sasa inakuwa ni vigumu kwa wakazi mitaani kulala na kupumzika kwa amani. Juu ya hili unaongezewa magari yanayopita mitaani na makelele na promosheni za kijinga na zisizoendana na maadili ya Watanzania.
Ni lazima katiba imlinde mwananchi wa kawaida na sio matajiri na wenye fedha na viongozi na hasa wale wenye mabaa na vilabu vya starehe!
Hadidu:
. Baa zijengwe karibu na misikiti, kanisa na makazi ya watu?
. Maduka ya Pombe na Baa ziwepo kwenye maeneo ya watu wenye imani zinazokataza vitu hivyo?
. Kuwe na utaratibu gani wa kuzuia polusheni ya sauti na makelele watu wasiyotaka kusikia?
. Ni nani aruhusu ujenzi wa baa karibu na makazi ya wananchi? Wananchi wenyewe au maofisa serikali na viongozi wa vyama waroho na walafi?
. Malaya waendeshe biashara zao kwa utaratibu gani na mahala gani?
. Wasenge na mabaasha wawe na haki gani katika jamii ya Kitanzania?
. Baa ziruhusiwe kuwa kwenye maeneo ya wazi na kuwatamanisha watoto na vijana wa waumini ambao kwao ni haramu?
HUU ni mchango wangu katika kusaidia kuwepo kwa katiba bora nchini itakayoweza kutumika sio tu kwa miaka hamsini lakini hata kwa karne kumi na zaidi. Katiba itakayosimama kama katiba na sio matakwa ya mtu fulani au chama fulani hapa nchini.
Monday, January 31, 2011
Zanzibar, Mikoa na Katiba
Zanzibar yenye wapiga kura laki nne tu iweje iwe na rais, waziri mkuu na baraza la mawaziri wakati mikoa yenye idadi kubwa mata tatu au nne ya hiyo huku bara haina mfumo huo?
. Je, katiba haistahili kuwa na kifungu juu ya mfumo na muundo mpya wa serikali za mikoa ?
. Badala ya kuwa tu serikali za mikoa serikali hizo zikawa ni serikali huru kiuchumi na kijamii?
. Je, serikali hizo huru za mkoa kiuchumi na kijamii hazitakuwa bora kuliko kuwa na Mkuu wa Mkoa ambaye aghalabu ni CCM pigaua? Si mwenye uchungu na mkoa? Huichukulia nafasi yake ya uongozi kama njia ya kujitajirisha kibinafsi na kukinufaisha chama chake kisiasa ?
. Waziri Mkuu wa Mkoa atakuwa mkazi wa mkoa husika, mwenye uchungu na mkoa wake na watu wake na atatoka kwenye chama chenye wabunge wengi kimkoa?
. Bunge litaundwa na wabunge wa kitaifa na wabunge toka makundi yote makuu kijamii na kiuchumi mkoani?
. Mawaziri wa mkoa watatokana na wabunge hao? Na mbunge akishachaguliwa waziri ataachia nafasi ya ubunge ili kufanya kazi zake bila upendeleo ?
. Je, kwa namna hii taifa halitanufaika kwa sababu mikoa yote itakuwa ni shule za viongozi wa aina mbalimbali ? Na kwamba mawaziri wa kitaifa itakuwa ni nadra kuwa watu ambao hawakuwa mawaziri katika ngazi ya mkoa?
. Je ni muundo wa kuwa na Mkuu wa Mkoa wa Kichama au kuwa na Waziri Mkuu, Mawaziri na Wabunge kutakakoharakisha maendeleo ya mkoa na wakazi wake haraka ?
. Je, katiba haistahili kuwa na kifungu juu ya mfumo na muundo mpya wa serikali za mikoa ?
. Badala ya kuwa tu serikali za mikoa serikali hizo zikawa ni serikali huru kiuchumi na kijamii?
. Je, serikali hizo huru za mkoa kiuchumi na kijamii hazitakuwa bora kuliko kuwa na Mkuu wa Mkoa ambaye aghalabu ni CCM pigaua? Si mwenye uchungu na mkoa? Huichukulia nafasi yake ya uongozi kama njia ya kujitajirisha kibinafsi na kukinufaisha chama chake kisiasa ?
. Waziri Mkuu wa Mkoa atakuwa mkazi wa mkoa husika, mwenye uchungu na mkoa wake na watu wake na atatoka kwenye chama chenye wabunge wengi kimkoa?
. Bunge litaundwa na wabunge wa kitaifa na wabunge toka makundi yote makuu kijamii na kiuchumi mkoani?
. Mawaziri wa mkoa watatokana na wabunge hao? Na mbunge akishachaguliwa waziri ataachia nafasi ya ubunge ili kufanya kazi zake bila upendeleo ?
. Je, kwa namna hii taifa halitanufaika kwa sababu mikoa yote itakuwa ni shule za viongozi wa aina mbalimbali ? Na kwamba mawaziri wa kitaifa itakuwa ni nadra kuwa watu ambao hawakuwa mawaziri katika ngazi ya mkoa?
. Je ni muundo wa kuwa na Mkuu wa Mkoa wa Kichama au kuwa na Waziri Mkuu, Mawaziri na Wabunge kutakakoharakisha maendeleo ya mkoa na wakazi wake haraka ?
Subscribe to:
Posts (Atom)