Friday, January 27, 2012

Mchakato Halali wa Katiba Mpya Unavyostahili kuwa...

MCHAKATO halali wa katiba unastahili kufuata utaratibu kama huu hapa chini au unaokaribia kufanana nao (kwa kuzingatia kwamba ridhaa inaweza kutoka kwa kiongozi lakini maamuzi yanatoka kwa wawakilshi halali wa wananchi ndani na nje ya bunge), na unaozingatia kuwa washika mamlaka na madaraka ya nchi ni watu na sio serikali na viongozi wake (maana hawa ni vibarua tu):


1. Kiongozi wa serikali iliyopo madarakani (kwa kuzingatia nchi inafuata mfumo wa vyama vingi), analiandikia bunge kuwa wanaowawakilisha wanataka katiba mpya, hivyo bunge lishirikiane na wawakilishi wengine wa wananchi kupitia vyama vyao mbalimbali, ikiwemo vya wafanyaazi, kitaaluma, kijamii na kadhalika kuandaa muswaada wenye ridhaa ya wananchi kuanza mchakato wa kutafuta katiba mpya. Hatua hii ni muhimu kwani inadhihirisha kuwa rais si mfalme, bali ni mwajiriwa wa wananchi;
2. Bunge linawaarifu wananchi juu ya kukubaliwa kwa madai yao ya kupata katiba mpya na kuwaomba wasio na uwakilishi wa aina nyingine nje ya bunge kufanza haraka ya kuwatafuta wawakilishi wao ili washiriki katika Baraza la Kitaifa la Kuandika Katiba Mpya;
3. Wabunge wanarudi kwenye majimbo yao na kuwasaidia wananchi wao kupata wawakilishi katika kila eneo ikiwemo yale ya kijamii, kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni na kiimani;
4. Wananchi wanapendekeza kwa ushauri wa bunge idadi ya wajumbe na makundi maslahi na maalum yatakayo wakilishwa, katika Baraza la Kitaifa la Kuandika Katiba Mpya;
5. Waliochaguliwa wanaketi kama wajumbe wa Baraza la Kitaifa la Kuandika Katiba Mpya kuchagua kamati mbalimbali mojawapo ikiwa ile ya kuandika muswaada wa kisheria kuhusiana na mchakato wa katiba mpya, tofauti na ilivyofanyika kwa kutokea ofisi ya rais na watumishi wa chama tawala nchini;
6. Muswaada unaidhinishwa na asilimia ya wajumbe iliyokubalika awali na kuwasilishwa kwa viongozi na washika dau mbalimbali kama taarifa na vilevile kwa nyongeza au ukinzani ili urekebishwa na kuimarishwa zaidi kwa faida ya walio wengi;
7. Mgawanyo wa kazi katika Baraza la Kitaifa la Kuandika Katiba Mpya unafanyika na kazi mbalimbali kuhusiana na kuhamasihwa na kuelimishwa wananchi; kuandka rasimu mbalimbali; kujifunza toka nchi nyingine na kukusanya mawazo na fikra za wananchi ndani na nje ya nchi zinaanza;
8. Baraza la Kitaifa la Kuandika Katiba Mpya linapaswa kuwa na vikao kadhaa vya kutathmini kazi na ubora wa kazi iliyofanyika katika hatua mbalimbali na wakati huohuo kuwa na uwezo wa kisheria wa kuamrisha yanayostahili kufanyika kwa manufaa na faida ya nchi, sheria, usalama na haki za wananchi/binadamu kufanyika bila ya kusubiri mchakato kukamilika. Vikao hivi vitakuwa wazi na huru na kuhudhuriwa na yeyote yule anayetaka ili kukamilisha dhana ya wananchi kudhibiti mchakato mzima toka mwanzo mpaka mwisho;
9. Ili kuliepusha taifa na mzigo wa kubeba gharama kubwa katika zoezi la kupata katiba mpya Baraza la Kitaifa la Kuandika Katiba Mpya litapaswa kuweka muda wa mwisho wa kufanya kila jambo na gharama zitakazoendana na kila shughuli inayopaswa kufanyika;
10. Baraza lina haki ya kukataa na kubatilisha tamko, sheria au hatua yoyote ile ambayo italifanya zoezi la kuandika katiba mpya kuwa gumu, la kiujanjaujanja, kitu kisicho wazi au lenye mizengwe kwa faida ya mtu au chama fulani;
11. Baraza la Kitaifa la Kuandika Katiba Mpya lina haki ya kuomba wataalamu wa mambo ya sheria toka ndani na nje ya nchi kuajiriwa ili kurahisisha na kufanikisha zoezi hilo kama lilivyopangwa;
12. Baraza la Kitaifa la Kuandika Katiba Mpya litakuwa huru kutangaza mahala linapokwama, nani analikwamisha na aidha kuomba ridhaa toka kwa wananchi kwa muda wa kufanya kazi zake ili zikamilike vizuri kama ilivyopangwa toka mwanzo.

Monday, January 9, 2012

Mapendekezo huru na yasiyo na uchama: wala umimi

ILI kufanikisha uandikwaji katiba mpya ninapendekeza yafuatayo, bila ushawishi kutoka kwea yeyote:


1. Mheshimiwa rais asitishe kuchagua tume yake ya katiba;

2. Muswaada wa uundwaji wa tume ya katiba urejeshwe bungeni baada ya kufanyiwa kazi na wataalam wa Katiba kama Maprofesa Issa Shivji na Chris-Peter Maina.

3. Taifa liunde Baraza la Kikatiba litakalotokana na wawakilishi wa makundi maslahi mbalimbali, vyama vya kisiasa, taasisi za kidini, wabunge na kadhalika:

4. Tume ya Uchaguzi inayonukia Uchama iliyopo ivunjwe. Tume Huru ya Uchaguzi ichaguliwa na Baraza Jipya la Kikatiba, kama uthibitisho kwamba mamlaka sasa imerudishwa mikononi mwa wananchi;

5. Baraza Jipya la Kikatiba likishirikiana na ofisi ya rais kuteua Waziri mpya wa Sheria na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

6. Baraza Jipya la Kikatiba liteue Kamati Maalum Kushughulikia upatikanaji maoni na uandikwaji wa Katiba mpya;

7. Maamuzi yote yanayopitukia Chama Kimoja na masuala ya demokrasia yaamuliwe na Baraza Jipya la Kikatiba badala ya Serikali au Ikulu ili kulinda amani na umoja wa nchi;

8. Mapendekezo ya Kikatiba yagawanywe kait ya yale yanayostahili kushughulikiwa moja kwa moja na kwa haraka sana na yale yanayoweza kutekelezwa baada ya Katiba mpya kupitishwa;

9. Ili kuiepusha nchi na gharama zisizo za lazima wakati huu mgumu kiuchumi, Mahakama na Mwanasheria Mkuu wa serikali badala ya kuingilia uhuru wa vyama vya upinzani wapitishe sheria ya kuruhusu mgombea huru wa uchaguzi, na kwa maana hiyo, ruhusa ya mbunge anayefukuzwa toka chama fulani kuendelea na ubunge wake kama mbunge asiye na chama au mbunge huru;

10. Baraza jipya la Katiba kuruhusu vyama, mashirika yasiyo ya kiserikali, wanaharakati, wanasheria na vyama vya kijamii mbalimbali kutumia kipindi cha mwaka huu kuwaelimisha Watanzania juu ya katiba ya zamani na mbinu na mikakati ya kuwa na katiba itakaowafaa Watanzania kwa miaka 50 au zaidi.

11. Baraza jipya la katiba litaunda kamati au vyombo maalum vya kitaalaamu ambavyo kwa ushirikiano na makundi maslahi katika jamii yetu vitafanya mchakato wa kuhakikisha kila kisichopo katika katiba kinazungumzwa na kisha kuingizwa katika katiba kwa mujibu ya matakwa ya watawaliwa wa nchi hii.

12. Baraza jipya la katiba litaunda kamati na vyombo mbalimbali vya kitaalamu kupitia ibara na vifungu vyote ambavyo vimekoslewa kwa njia moja au nyingine ili kuviboresha au kuviondoa kabisa kama havifai.

Thursday, November 17, 2011

Muswada wa katiba ni waCCM na serikali yake na hauna nia njema na Watanzania wa sasa na wajao......

Kwanini tunasema katiba ni mali ya wananchi ?

HUFIKA wakati katika historia ya nchi ikawalazimu viongozi waliopo kukaa pembeni na kuwaachia wananchi madaraka au mamlaka ya kufanya maamuzi muhimu ya kitaifa. Mojawapo ya wakati kama huo ni pale nchi inapotka kuwa na katiba mpya. Kwa kuwa wananchi ndio wenye sauti ya mwisho na maamuzi makuu katika suala hili ni uungwana, haki na kuona mbali na mbele kwa viongozi waliokuwepo kusalimu amri kwa wananchi na kuwakabidhi kupitia watu ambao wananchi wenyewe watakaowachagua kuwawakilisha katika kuandaa utaratibu mzima toka kuanza hadi kumaliza kazi ya kupata mchakato wa njia na namna za kuipata katiba na vilevile upatikanaji wa toleo la mwisho la katiba mpya litakalopigiwa kura na wananchi.

Hii ni hatua inayohitaji viongozi wanaojiweka zaidi kama viongozi wa kitaifa na wafanya maamuzi makuu yatakayoathiri maisha ya kizazi hiki na vizazi vijavyo kwa wema au ubaya. Wanaoshindwa kufanya hili hawatendei haki wajibu na majukumu wanayostahili kuyabeba kama viongozi wa watu na nchi yao.

Uongozi unaoshindwa kutambua kwamba muda wa KUSALIMU AMRI KWA WANANCHI WAKE umefika ni uongozi wenye hatari ya kuiingiza nchi kwenye matatizo makubwa ya kisiasa, kijamii na kiuchumi. Ni uongozi usiotakia kheri kizazi kilichopo na vizazi vijavyo katika nchi husika.


Ukubwa mlionao

Ukubwa mlionao, mmepewa na wananchi,
Hawa ndio waamuao, hatima yenu na nchi,
Na muda wautakao, huwapeleka benchi,
Wafanye maazimio, kula mbivu au mbichi,
Ukubwa muutakao,kwa nachi na upanchi,
Hamjui mfanyayo,si wananchi ni wenyenchi,
Ni hasama mleltao,wana waje enda uchi,
Hayo kama matamanio,iwe kucha haukuchi,
Fanyeni wayatakayo,Tanzania wananchi,
Na siyo muyatakayo,mlio kwenye makochi,
Taabu si mjuao,wala hamli vibichi,
Sio muhangaikao,ni rahisi zenu mechi,
Na sio muelewao,nini hatima ya nchi!


Akizungumzia uwezekano wa kuandikwa katiba mpya ya Tanzania kwa mara yake ya kwanza, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti na mwanachama wa Chama kimojawapo cha siasa nchini Tanzania, CCM, Bwana Jakaya Kikwete pamoja na mambo mengine alionesha kutamani sana kwamba katiba itakayoandikwa iweze kutufaa kwa miaka 50 kama sio 100. Hata hivyo, kile kilichowasilishwa na Waziri wake wa katiba hakikufanana kabisa na matamanio mema yake hayo.

Tofauti na msimamo huu wa mheshimiwa Rais, muswada wa serikali yake kwa bunge la Jamhuri ulidhihirisha nia ya serikali ya Chama cha Mapinduzi kuitumia fursa hiyo ili iweze kujikita vyema zaidi nchini kwa halali au haramu kisiasa kwa kuwatumia wabunge wao ambao ilionekana kama walishapewa mafunzo maalum kuhusu kinachotegemewa kutoka kwao.

Pamoja na spika wa bunge hilo kudai kwamba wanaharakati, wapinzani na waandishi wa habari wanapotosha kilicho mezani mwa wabunge, kazi nzuri ya uchambuzi wa kina iliyofanywa na Mheshimiwa Tundu Lissu (CHADEMA) ilionesha kulikuwa na uwezekano mkubwa wa wabunge wa CCM kutokuwa wameusoma muswada huo na Tundu akawa anapigia gitaa mbuzi.

Pengine wabunge wa CCM walishaambiwa kwamba ni lazima upite kama ulivyo na hakuna aliyesumbuka kuusoma kikwelikweli, lakini baadaye ilidhihirika waziwazi kwamba muswada huo ulikuwa na udhaifu mkubwa na kasoro nyingi za kimaudhui, kisheria, kisiasa na kikanuni kikatiba ambao kwa watunga sheria makini lazima wangelihitaji muda wa ziada wa kuufanyia kazi na sio kama wenzetu walivyoanza kuchangia wakiwa na uelewa 'finyu kiuzalendo' kwa kazi iliyokwa mbele yao.

Sio siri kwamba CCM inachokitaka pengine ni kujihakikishia uzima wa milele. Kitu ambacho hakiwezekani. Na haitawezekana kwa sababu hizi si zama za Nyerere, Mkapa na Mwinyi na chochote kinaweza kutokea kwa watu ambao hali ya uchumi inawawia ngumu kila kukichwa, mali asili zao zinatwaliwa bure, watu wanauawa na kubakwa migodini na wakubwa wanapora fedha, wanyama pori, miti, ardhi na rasilimali nyingine kwa jinsi wanavyotaka. Na wasichonacho wananyang'anywa hata kile kidogo walicho nacho, wakati wenye nacho wanazidi kuongezewa kila siku.

Watanzania hawatakaa wasahau kwamba kunako mwezi Novemba, mwaka 2011 baadhi ya wabunge wao kupitia CCM walipoteza fursa ya kipekee katika kuutanguliza Utanzania mbele ya nafsi na uchama wao. Matokeo ya ubinafsi na uchama wao yakawapotezea fursa hii adhimu ambayo ingeliwaweka pazuri sana katika historia ya nchi yao na watu wake.

Kilichotokea ni kwa wabunge hao wa CCM-CUF kuonesha dhahiri kuwa ni mbwa-mwitu (wawakilishi wa chama na serikali) waliovaa ngozi ya kondoo (wawakilishi wa wananchi). Kipaumbele siku hiyo hakikupewa wananchi na vizazi vyao vijavyo bali chama, matashi yake na ubinafsi wa wabunge hata kama Watanzania kwa ujumla wao watapoteza kikubwa zaidi siku zijazo.


UCCM na UCUF kwa kiasi fulani katika hili umewafanya wengi waamini kuwa wabunge wa vyama hivyo wanastahili kupata shahada ya udaktari katika uchama, usisi, umimi na katika mapambano ya maslahi na maendeleo ya wabunge binafsi.

Kwa maneno mengine, wabunge wa CCM na CUF walikuwa wakituambia kwamba vyama vyao na uongozi wa chama chao ni muhimu kuliko Utanzania wetu au utaifa wetu, watu wetu na vizazi vyetu vijavyo.

Kubwa zaidi ni lile la spika, muwakilishaji muswada na wabunge wa CCM waliochangia muswada huo kusingizia eti kuna urongo, uzushi, upotoshaji na tafsiri mbovu ya kile kilichotakiwa kuwakilishwa. Haraka aliyokuwa nayo spika, wabunge wa CCM kuchangia na mwasilisha muswada na wenzake kuliacha maswali mengi kuliko majibu. Mwisho wa siku kilio cha spika, muwasilisha mada na wabunge wa CCM na CUF kilifanana na kile kilio cha mchunga kondoo aliyekuwa akisumbua wanakijiji wenzake kwa kupiga mayowe ya MBWA MWITU, MBWA MWITU kumbe yote ilikuwa ni mzaha kama sio urongo.

Uzaini wa CCM wa kujionesha eti wana CCM na viongozi wao wanaipenda na wana uchungu sana na Tanzania kuliko watu wengine umewafanya jamaa hao kuangukia pua katika siku ambayo wengi wao hawataiashau na wao wenyewe wameamua kujizika kihistoria.


CCM na wakewenza Unguja

Baya zaidi ni lile la muswada huo kudiriki kuifanya Zanzibar kuwa sawasawa na Tanganyika isiyopo katika kuamua hatima ya nchi yetu na watu wake. Hiki ni kitendo cha waendesha utumwa, kikoloni, kibabe, kihuni na cha kidhalimu ambacho hakistahili kukubalika.
Kwani nia ya kuwapa ukubwa huu Wazanzibari wasiostahili kuupata ni kurahisisha siasa ndani ya CCM kati ya Wazanzibari na Wabara. Kwa maneno mengine, CCM imediriki kuwauza Watanganyika kwa Wazanzibari, kama walivyouza migodi ya dhahabu, ili mradi tu mambo yao yawe safi.

Ukewenza Zanzibar na Serikali ya JMT, unatuweka pabaya kitamathali na kiuyakinifu kwa kiasi cha eti watu asilimia 2 Tanzania kuamua hatima ya asilimia 98 iliyobakia.
Kwa maneno mengine, muswada huo unawageuza Wazanzibar wakoloni na Watanganyika watawaliwa katika nchi yao wenyewe. Sijui hata kama muswada huo utapita kama hili litakaa likubalike kesho na keshokutwa.

Hadhi ya Zanzibar kiukweli haina tofauti na ya mkoa wowote bara. Tofauti tu ni kuwa mikoa inabanwa kuwa huru kisiasa, kijamii na kiuchumi kwa mafaniko yake makubwa na haraka zaidi. Kilichokosekana ni uamsho kwa wakazi mikoani na uadilifu kwa serikali kuipa mikoa serikali huru zinazosimamiwa na waziri mkuu wa mkoa, baraza la mawaziri wa mkoa na wawakilishi wa mkoa na mikoa mingi tu ingeiacha Zanzibar nyuma kimaendeleo, bila ya visiwa hivyo kuona hata indiketa za mikoa hiyo kwenye mbio za ustawi wa jamii na maendeleo ya mkoa.

Itakuwa ni jambo la fedheha kama wabunge na serikali yetu baada ya kushindwa kuafikiana na wapinzani wa kweli ndani ya bunge itakuja kufanza hivyo kwa kupata shinikizo toka Marekani na EU. Jambo hili litaonesha kwamba viongozi wetu hawajaiva wala kukomaa na hakika hawastahili kuiongoza nchi hii kama kweli tunataka kuendelea na umoja na amani tuliyo nayo hivi leo. Kinachoonekana hapa ni kwamba kuna Watanzania wenye akili na uwezo mkubwa tu lakini kwa kukosa uongozi adilifu na mzuri wanashindwa kuwatumia.

Viongozi wa dini

Viongozi wa dini kama ilivyokuwa kwa wenzetu nchini Kenya wana mchango mkubwa katika kuhakikisha Tanzania inakuwa na katiba nzuri na safi na itakayowafaa Watanzania kwa muda mrefu kuliko hii ya kupandikizwa ilivyotsukuma sukuma.

Yapo mambo kadhaa ambayo viongozi wa dini wanaowatakia Watanzania na vizazi vyao amani na umoja wanaweza kuhoji na kutoa mwongozo yaende vipi kwa faida ya watu wote. Mathalani, hivi leo kanisa katoliki linafanya vizuri sana katika elimu na sekta ya afya, lakini siasa za uziwi na upofu zinaweza kuhujumu haya yote kama katiba isipohifadhi sheria na haki muhimu za kulinda kanisa, mali zake na viongozi wake. Misikiti na Makanisa yakikaa nyuma, viongozi wa dini wasije anza kulalama baadaye kwamba katiba imewapendelea hawa, au kuwaonea hawa.

Makampuni na taasisi na katiba

Makampuni na taasisi kisheria ni sawa na mtu au raia. Makampuni na taasisi zikikaa nyuma na kutokushiriki kwenye mchakato wa katiba mpya yapo masuala mengi yanayoweza kuja kuzuka baadaye kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni yakaya kuwa ni kwa hasara kubwa kwa upande wao.
Katika suala hili lal katiba mpya sisi sote ni wadau na washiriki na hakuna anayestahili kubakia kuwa mtazamaji tu au juu ya wenzake kwa namna yoyote ile.

Muswada huu kama ilivyokuwa kwa miswaada mingine dhaifu, inayovuja na dhalimu kwa wananchi na vizazi vijavyo, imedhirisha mapungugu mengi mengine katika muundo, mifumo na taratibu zetu za uongozi na uendeshaji nchi. Baadhi ya kasoro hizi ni pamoja na hatari ya kuwa na wabunge wa kuteuliwa badala ya kuchaguliwa kwenye bunge la kiwakilishi; jinsi ambavyo serikali iliyoko madarakani inaweza ikapora mamlaka na madaraka ya wananchi na kufanya mapinduzi ya kikatiba bila kuwajibishwa ipasavyo; muungano unavyozidi kuonekana kukosa maana kwa Watanganyika na kuwa mzigo usiobebeka; na ule ukweli kuwa nchi bado imo kizani na haijajaliwa kuwa na kiongozi na wanasiasa wanaoweza kututoa kwenye shimo refu la giza ambalo tumejikuta tumo leo.

Muswada wa katiba ni waCCM na serikali yake na hauna nia njema na Watanzania wa sasa na wajao......

Kwanini tunasema katiba ni mali ya wananchi ?

HUFIKA wakati katika historia ya nchi ikawalazimu viongozi waliopo kukaa pembeni na kuwaachia wananchi madaraka au mamlaka ya kufanya maamuzi muhimu ya kitaifa. Mojawapo ya wakati kama huo ni pale nchi inapotka kuwa na katiba mpya. Kwa kuwa wananchi ndio wenye sauti ya mwisho na maamuzi makuu katika suala hili ni uungwana, haki na kuona mbali na mbele kwa viongozi waliokuwepo kusalimu amri kwa wananchi na kuwakabidhi kupitia watu ambao wananchi wenyewe watakaowachagua kuwawakilisha katika kuandaa utaratibu mzima toka kuanza hadi kumaliza kazi ya kupata mchakato wa njia na namna za kuipata katiba na vilevile upatikanaji wa toleo la mwisho la katiba mpya litakalopigiwa kura na wananchi.

Hii ni hatua inayohitaji viongozi wanaojiweka zaidi kama viongozi wa kitaifa na wafanya maamuzi makuu yatakayoathiri maisha ya kizazi hiki na vizazi vijavyo kwa wema au ubaya. Wanaoshindwa kufanya hili hawatendei haki wajibu na majukumu wanayostahili kuyabeba kama viongozi wa watu na nchi yao.

Uongozi unaoshindwa kutambua kwamba muda wa KUSALIMU AMRI KWA WANANCHI WAKE umefika ni uongozi wenye hatari ya kuiingiza nchi kwenye matatizo makubwa ya kisiasa, kijamii na kiuchumi. Ni uongozi usiotakia kheri kizazi kilichopo na vizazi vijavyo katika nchi husika.


Ukubwa mlionao

Ukubwa mlionao, mmepewa na wananchi,
Hawa ndio waamuao, hatima yenu na nchi,
Na muda wautakao, huwapeleka benchi,
Wafanye maazimio, kula mbivu au mbichi,
Ukubwa muutakao,kwa nachi na upanchi,
Hamjui mfanyayo,si wananchi ni wenyenchi,
Ni hasama mleltao,wana waje enda uchi,
Hayo kama matamanio,iwe kucha haukuchi,
Fanyeni wayatakayo,Tanzania wananchi,
Na siyo muyatakayo,mlio kwenye makochi,
Taabu si mjuao,wala hamli vibichi,
Sio muhangaikao,ni rahisi zenu mechi,
Na sio muelewao,nini hatima ya nchi!


Akizungumzia uwezekano wa kuandikwa katiba mpya ya Tanzania kwa mara yake ya kwanza, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti na mwanachama wa Chama kimojawapo cha siasa nchini Tanzania, CCM, Bwana Jakaya Kikwete pamoja na mambo mengine alionesha kutamani sana kwamba katiba itakayoandikwa iweze kutufaa kwa miaka 50 kama sio 100. Hata hivyo, kile kilichowasilishwa na Waziri wake wa katiba hakikufanana kabisa na matamanio mema yake hayo.

Tofauti na msimamo huu wa mheshimiwa Rais, muswada wa serikali yake kwa bunge la Jamhuri ulidhihirisha nia ya serikali ya Chama cha Mapinduzi kuitumia fursa hiyo ili iweze kujikita vyema zaidi nchini kwa halali au haramu kisiasa kwa kuwatumia wabunge wao ambao ilionekana kama walishapewa mafunzo maalum kuhusu kinachotegemewa kutoka kwao.

Pamoja na spika wa bunge hilo kudai kwamba wanaharakati, wapinzani na waandishi wa habari wanapotosha kilicho mezani mwa wabunge, kazi nzuri ya uchambuzi wa kina iliyofanywa na Mheshimiwa Tundu Lissu (CHADEMA) ilionesha kulikuwa na uwezekano mkubwa wa wabunge wa CCM kutokuwa wameusoma muswada huo na Tundu akawa anapigia gitaa mbuzi.

Pengine wabunge wa CCM walishaambiwa kwamba ni lazima upite kama ulivyo na hakuna aliyesumbuka kuusoma kikwelikweli, lakini baadaye ilidhihirika waziwazi kwamba muswada huo ulikuwa na udhaifu mkubwa na kasoro nyingi za kimaudhui, kisheria, kisiasa na kikanuni kikatiba ambao kwa watunga sheria makini lazima wangelihitaji muda wa ziada wa kuufanyia kazi na sio kama wenzetu walivyoanza kuchangia wakiwa na uelewa 'finyu kiuzalendo' kwa kazi iliyokwa mbele yao.

Sio siri kwamba CCM inachokitaka pengine ni kujihakikishia uzima wa milele. Kitu ambacho hakiwezekani. Na haitawezekana kwa sababu hizi si zama za Nyerere, Mkapa na Mwinyi na chochote kinaweza kutokea kwa watu ambao hali ya uchumi inawawia ngumu kila kukichwa, mali asili zao zinatwaliwa bure, watu wanauawa na kubakwa migodini na wakubwa wanapora fedha, wanyama pori, miti, ardhi na rasilimali nyingine kwa jinsi wanavyotaka. Na wasichonacho wananyang'anywa hata kile kidogo walicho nacho, wakati wenye nacho wanazidi kuongezewa kila siku.

Watanzania hawatakaa wasahau kwamba kunako mwezi Novemba, mwaka 2011 baadhi ya wabunge wao kupitia CCM walipoteza fursa ya kipekee katika kuutanguliza Utanzania mbele ya nafsi na uchama wao. Matokeo ya ubinafsi na uchama wao yakawapotezea fursa hii adhimu ambayo ingeliwaweka pazuri sana katika historia ya nchi yao na watu wake.

Kilichotokea ni kwa wabunge hao wa CCM-CUF kuonesha dhahiri kuwa ni mbwa-mwitu (wawakilishi wa chama na serikali) waliovaa ngozi ya kondoo (wawakilishi wa wananchi). Kipaumbele siku hiyo hakikupewa wananchi na vizazi vyao vijavyo bali chama, matashi yake na ubinafsi wa wabunge hata kama Watanzania kwa ujumla wao watapoteza kikubwa zaidi siku zijazo.


UCCM na UCUF kwa kiasi fulani katika hili umewafanya wengi waamini kuwa wabunge wa vyama hivyo wanastahili kupata shahada ya udaktari katika uchama, usisi, umimi na katika mapambano ya maslahi na maendeleo ya wabunge binafsi.

Kwa maneno mengine, wabunge wa CCM na CUF walikuwa wakituambia kwamba vyama vyao na uongozi wa chama chao ni muhimu kuliko Utanzania wetu au utaifa wetu, watu wetu na vizazi vyetu vijavyo.

Kubwa zaidi ni lile la spika, muwakilishaji muswada na wabunge wa CCM waliochangia muswada huo kusingizia eti kuna urongo, uzushi, upotoshaji na tafsiri mbovu ya kile kilichotakiwa kuwakilishwa. Haraka aliyokuwa nayo spika, wabunge wa CCM kuchangia na mwasilisha muswada na wenzake kuliacha maswali mengi kuliko majibu. Mwisho wa siku kilio cha spika, muwasilisha mada na wabunge wa CCM na CUF kilifanana na kile kilio cha mchunga kondoo aliyekuwa akisumbua wanakijiji wenzake kwa kupiga mayowe ya MBWA MWITU, MBWA MWITU kumbe yote ilikuwa ni mzaha kama sio urongo.

Uzaini wa CCM wa kujionesha eti wana CCM na viongozi wao wanaipenda na wana uchungu sana na Tanzania kuliko watu wengine umewafanya jamaa hao kuangukia pua katika siku ambayo wengi wao hawataiashau na wao wenyewe wameamua kujizika kihistoria.


CCM na wakewenza Unguja

Baya zaidi ni lile la muswada huo kudiriki kuifanya Zanzibar kuwa sawasawa na Tanganyika isiyopo katika kuamua hatima ya nchi yetu na watu wake. Hiki ni kitendo cha waendesha utumwa, kikoloni, kibabe, kihuni na cha kidhalimu ambacho hakistahili kukubalika.
Kwani nia ya kuwapa ukubwa huu Wazanzibari wasiostahili kuupata ni kurahisisha siasa ndani ya CCM kati ya Wazanzibari na Wabara. Kwa maneno mengine, CCM imediriki kuwauza Watanganyika kwa Wazanzibari, kama walivyouza migodi ya dhahabu, ili mradi tu mambo yao yawe safi.

Ukewenza Zanzibar na Serikali ya JMT, unatuweka pabaya kitamathali na kiuyakinifu kwa kiasi cha eti watu asilimia 2 Tanzania kuamua hatima ya asilimia 98 iliyobakia.
Kwa maneno mengine, muswada huo unawageuza Wazanzibar wakoloni na Watanganyika watawaliwa katika nchi yao wenyewe. Sijui hata kama muswada huo utapita kama hili litakaa likubalike kesho na keshokutwa.

Hadhi ya Zanzibar kiukweli haina tofauti na ya mkoa wowote bara. Tofauti tu ni kuwa mikoa inabanwa kuwa huru kisiasa, kijamii na kiuchumi kwa mafaniko yake makubwa na haraka zaidi. Kilichokosekana ni uamsho kwa wakazi mikoani na uadilifu kwa serikali kuipa mikoa serikali huru zinazosimamiwa na waziri mkuu wa mkoa, baraza la mawaziri wa mkoa na wawakilishi wa mkoa na mikoa mingi tu ingeiacha Zanzibar nyuma kimaendeleo, bila ya visiwa hivyo kuona hata indiketa za mikoa hiyo kwenye mbio za ustawi wa jamii na maendeleo ya mkoa.

Itakuwa ni jambo la fedheha kama wabunge na serikali yetu baada ya kushindwa kuafikiana na wapinzani wa kweli ndani ya bunge itakuja kufanza hivyo kwa kupata shinikizo toka Marekani na EU. Jambo hili litaonesha kwamba viongozi wetu hawajaiva wala kukomaa na hakika hawastahili kuiongoza nchi hii kama kweli tunataka kuendelea na umoja na amani tuliyo nayo hivi leo. Kinachoonekana hapa ni kwamba kuna Watanzania wenye akili na uwezo mkubwa tu lakini kwa kukosa uongozi adilifu na mzuri wanashindwa kuwatumia.

Viongozi wa dini

Viongozi wa dini kama ilivyokuwa kwa wenzetu nchini Kenya wana mchango mkubwa katika kuhakikisha Tanzania inakuwa na katiba nzuri na safi na itakayowafaa Watanzania kwa muda mrefu kuliko hii ya kupandikizwa ilivyotsukuma sukuma.

Yapo mambo kadhaa ambayo viongozi wa dini wanaowatakia Watanzania na vizazi vyao amani na umoja wanaweza kuhoji na kutoa mwongozo yaende vipi kwa faida ya watu wote. Mathalani, hivi leo kanisa katoliki linafanya vizuri sana katika elimu na sekta ya afya, lakini siasa za uziwi na upofu zinaweza kuhujumu haya yote kama katiba isipohifadhi sheria na haki muhimu za kulinda kanisa, mali zake na viongozi wake. Misikiti na Makanisa yakikaa nyuma, viongozi wa dini wasije anza kulalama baadaye kwamba katiba imewapendelea hawa, au kuwaonea hawa.

Makampuni na taasisi na katiba

Makampuni na taasisi kisheria ni sawa na mtu au raia. Makampuni na taasisi zikikaa nyuma na kutokushiriki kwenye mchakato wa katiba mpya yapo masuala mengi yanayoweza kuja kuzuka baadaye kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni yakaya kuwa ni kwa hasara kubwa kwa upande wao.
Katika suala hili lal katiba mpya sisi sote ni wadau na washiriki na hakuna anayestahili kubakia kuwa mtazamaji tu au juu ya wenzake kwa namna yoyote ile.

Muswada huu kama ilivyokuwa kwa miswaada mingine dhaifu, inayovuja na dhalimu kwa wananchi na vizazi vijavyo, imedhirisha mapungugu mengi mengine katika muundo, mifumo na taratibu zetu za uongozi na uendeshaji nchi. Baadhi ya kasoro hizi ni pamoja na hatari ya kuwa na wabunge wa kuteuliwa badala ya kuchaguliwa kwenye bunge la kiwakilishi; jinsi ambavyo serikali iliyoko madarakani inaweza ikapora mamlaka na madaraka ya wananchi na kufanya mapinduzi ya kikatiba bila kuwajibishwa ipasavyo; muungano unavyozidi kuonekana kukosa maana kwa Watanganyika na kuwa mzigo usiobebeka; na ule ukweli kuwa nchi bado imo kizani na haijajaliwa kuwa na kiongozi na wanasiasa wanaoweza kututoa kwenye shimo refu la giza ambalo tumejikuta tumo leo.

Sunday, November 13, 2011

Tahadhari: Mswaada wa katiba usisomwe kama vile unasomwa kwa mara ya pili, usomwe kwa mara ya kwanza.....

WAKATI tayari wabunge wanashinikizwa kuusoma mswaada wa katiba mpya kwa mara ya pili badala ya kusomwa mara ya kwanza, ninachukua fursa hii kuwaasa viongozi na wabunge wetu kwamba kitendo cha kuusoma mswaada huu kama unaosomwa mara ya pili haitakuwa tofauti na wao kuipindua katiba ya nchi na kosa hilo ni sawa sawa na mapinduzi ya kijeshi, tofauti ikiwa yale ya kijeshi watu wengi watakufa siku hiyo hiyo, wakati haya ya kikatiba Watanzania wote watakuwa wanauawa taratibu na kimya kimya.

Watanzania wana haki kwa kutumia wawakilishi wao wa kweli na halali kuhusiana na suala la katiba na sio wanafiki na vibarakala wa wale walioko madarakani, kuchukua hatua zote za kisheria ni kiharakati ili 'wanaoazimia kuipindua' katiba kinyume cha sheria wanachukuliwa hatua zinazostahili. Na sio tu serikali imeamua kuipindua katiba, bali inawaziba mdomo na masikio wananchi ili wasijue kinachofanyika kwa kuwatumia wale waliochaguliwa kulinda haki na maslahi ya watawala na sio ya watawaliwa!

Aidha, damu, dhiki na machungu yoyote yatakayosababishwa na kuusoma na kuupitisha mswadaa huu, laana yake iwaangukie viongozi wa Tanzania wa zamani na wa sasa.

Tunajua ugumu wa viongozi wa Afrika na hasa hawa wetu wa Tanzania kusalimu amri. Inatisha pale viongozi hao tena wanaposemekana ni wale wanaosalmi amri kwa Mwenyezi Mungu, lakini labda si hawa wa sasa...na kama wanalaghaiwa na wale wanaowashauri kwa sababu binafsi za washauri hao, basi huu ni wakati muafaka wa hususan rais, kusalimu amri na kuwarudishia Watanzania haki yao ya kikatiba ya kuwa ndio wenye mamlaka na madaraka ya juu kabisa kwenye suala kama hili na sio yeye rais. Anachoshauriwa kukifanya rais kwa hivi sasa ni sawa na 'kuwapindua Watanzania' kwa kuipindua katiba yao iliyopo hivi sasa ambayo ndiyo inayosema wao ndio wenye sauti ya mwisho juu ya katiba na sio rais.


Kwa kuzingatia hayo hapo juu, ni muhimu awali ya yote kuweka jambo moja muhimu kuliko yote sawa hapa. Je, ni rais au ni wananchi wenye haki ya kusimamia mchakato wa katiba mpya ? Je, rais si kiongozi wa seriikali taasisi ambayo ni mmoja wa wadau katika suala hili la katiba? Na rais huyo huyo sio mwenyekiti wa chama tawala ambacho ni mmoja wa wadau katika suala hili la katiba? Katika hali kama hii haki na uadilifu uko wapi? Ni katiba gani inayomruhusu rais kuwapora wananchi haki yao ya kuwa ndio walio na mamlaka na madaraka ya juu na ya mwisho kwenye masuala kama haya?


Kuna mambo kadhaa ambayo ninafikiri ni muhimu
kuwekwa wazi na ikiwezekana kutekelezwa hata kabla ya Tanzania kuwa na katiba mpya.

1. Mosi ni ufafanuzi wa nani ndiye mwenye sauti na maamuzi kuhusu mchakato wa katiba mpya kwa mujibu wa katiba tuliyonayo, yaani, ni nani kati ya wananchi kupitia chombo au vyombo vyao halali vya uwakilishi vilivyopo au kitakachoundwa au ni serikali na kiongozi wake. Utata unakuja pale tunapobaini kwamba serikali nayo pia ni mdau katika mchakato huu. Na kwamba si haki kwa chama au serikali kujipa mamlaka au madaraka ambayo hawastahili kuwa nayo, kwani huko ni sawa na kupora mamlaka ya wananchi na kufanya mapinduzi ya kikatiba bila kutumia silaha.

2. Haki ya Kuandamana na Maandamano. Tofauti na katiba ya sasa inavyoruhusu, utawala wa sasa, unadai kwamba watu hawana uhuru wa kuandamana na kufanya maandamano. Pamoja na kuwatia ulemavu wa maisha baadhi ya Watanzania wasio na kosa, usalama wa taifa na vyombo vya dola hususan FFU, vinatumika kuvuruga amani na kuharibu mali za Watanznia. Kazi ya usalama wa taifa na vyombo vya dola si kuzuia maandamano na mikutano bali kuweka taratibu za kuhakikisha wanaofanya mikutano na maandamano hayo wana ulinzi na usalama wa kutosha.

3. Haki ya kukutana na kufanya mikutano. Ilivyo hivi sasa kama hapo juu inaonekana Watanzania hawana haki ya kukutana na kufanya mikutano inayohusu maisha na maendeleo yao na mitaa na vijiji vyao ila pale wanaporuhusiwa na chama tawala kupitia serikali yake iliyoko madarakani.Kazi ya usalama wa taifa na vyombo vya dola si kuzuia maandamano na mikutano bali kuweka taratibu za kuhakikisha wanaofanya mikutano na maandamano hayo wana ulinzi na usalama wa kutosha.

4. Mikoa na haki za wakazi wa mkoa. Hali ilivyo sasa chama tawala na wale wanaoteuliwa kuwa viongozi wa mikoa wanachaguliwa sio kwa uwezo wao wa kimenejimneti na kuchangia maendeleo ya wakazi wa mkoa husika bali kwa sababu za kisiasa. Ni mfumo wa kikoloni ambao mkoloni mkuu anachagua wakoloni wa kumasaidia kuidhulumu na kuinyonya mkoa husika. Tz. kwa mfano mikoa ya Mwanza na Arusha hivi leo. Mikoa inastahili kutawaliwa na chama ambacho kina wabunge na madiwani wengi katika mkoa husika na sio vinginevyo. Aidha, kukidhi changamoto za kimaendeleo zilizopo wakati umefika kwa mkoa kuwa na Waziri wake mkuu na baraza lake la mawaziri wa mkoa husika ili kuimarisha uhuru, umoja, haki na kuharakisha maendeleo ya mkoa husika.

5. Endapo kiongozi anatoa AHADI na anashindwa kuzitekeleza nini kifanyike dhidi yake na wanaohusika kwa ujumla?

6. Nini liwe jukumu la serikali na wanasiasa kuhusu mustakabali wa vijana wasio na ajira, wamachinga na waendesha biashara ndogondogo.

7. Haki ya vyama kuungana. Mpaka sasa haieleweki kwanini kuna ugumu kwa vyama vya kisiasa kuungana ili kupunguza utitiri wa vyama nchini ambao hausaidii kuimarisha mfumo wa vyama vingi nchini bali kuudhoofisha zaidi na zaidi.

8. Haki ya Mgombea huru nchini. Mpaka sasa sheria imepindwa na katiba imepinduliwa kinyemela kwa kumnyima haki Mtanzania anayetaka kugombea uchaguzi bila kufungamana na chama chochote cha kisiasa.

9. Apartheid ya viongozi kutibiwa nchi za nje wakati walalahoi wanakufa kwa kukosa fedha za kuchangia katika zahanati na mahospitali sehemu mbalimbali nchini iendelee au ife kwa kuwa na hospitali bora zaidi nchini na madakta wasio na kazi kwenye nchi zenye matatizo ya kiuchumi hivi leo duniani.

10. Nini iwe nafasi ya upinzani katika uongozi wa nchi, mikoa, wilaya na majimbo? Na je tutarahisishaje vyama mbadala kuchangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika sehemu mbalimbali nchini.

11. Vyama viendeshwe vipi ili vipate mapato halali na sio kutegemea hazina ya serikali au kupata fedha kupitia njia ambazo zitahatarisha uhuru na utu wetu.

12. Vipi vinastahili kuwa vyombo vya habari vya wananchi na vipi vya serikali na chama tawala. Mkurugenzi achaguliwe vipi na nani? Uhuru wa vyombo hivyo utahakikishwaje?

13. Nini iwe kazi za majeshi yetu wakati wa amani? Yatashirikishwaje katika uzalishaji mali, huduma za jamii, biashara, uchimbaji madini ili kuhakikisha rasilimali za Watanzania hazipewi sawa na bure kwa wageni eti tu kwa sababu hatuna utaalamu na mitambo ya kufanya shughuli fulani?

14. Nini yawe majukumu ya usalama wa taifa ili uwe na tija zaidi katika maendeleo ya kiuchumi na kiteknolojia ya Watanzania kuliko ilivyo sasa. Na je ni sahihi usalama wa taifa kuchunguza viongozi wa zamani au wa upinzani kikatiba na kisheria?

15. Je, mamlaka ya Rais kuteua watu kama wakuu wa polisi, wakuu wa mikoa, wakuu wa Wilaya, majaji, mahakimu, wabunge wasiochaguliwa ni jambo zuri na linaloimarisha demokrasia au ni baya na linalodhoofisha uhuru, haki za binaadamu na demokrasia. Nini kifanyike kumaliza utata huu?

16. Je, Soko huru linastahili kuingiliwa na viongozi wa serikali ili kutafuta umaarufu wa bei rahisi? Nini kifanyike kama tumeshakubali kuwa nchi ya kibepari na soko huru. Nchi ifuate mfumo gani wa kisiasa bora kuliko ubepari na ukomunisti kesho na keshokutwa? Nini kimilikiwe na wageni na watu binafsi au wanajamii husika au serikali au ubia wa aina hii au ule?

17. Je, tunahitaji kikomo cha safari za nje ambazo kiongozi aliyeko madarakani anaweza kuzifanya katika kipindi chake cha miaka 5?

18. Je, ni magari ya aina gani na gharama gani wanastahili kuwa nayo viongozi wa serikali na wabunge na watumishi wa umma?

19. Ni vipi maji ya mito, maziwa, bahari, ardhini na mvua yanaweza kupatikana na kuhakikisha upatikanji wa maji safi kwa Watanzania sehemu zote za nchi na wakati wote?

20. Je, ni wanasiasa au watu wenye utaalamu fulani, k.m. walimu, wahadhiri na madaktari ndio wanaostahili kulipwa vizuri zaidi? Na kwanini mwanasiasa asilipwe kutokana na tarafu au kazi aliyoisomea na cheo anachostahili kuwa nacho wakati huu?

KIMSINGI, hayo hapo juu ni machache tu katika kero, vilio, matamanio, ndoto na matarajio ya Watanzania na hususan vijana ambao ndio wazazi na wenye nchi wa kesho kuhusu jinsi ambavyo wangelipenga kuona suala hili la katiba likishughulikiwa kama inavyostahili na sio kwa kutumia ujanja, maguvu, mabavu, uzaini, uzandiki, ubabe na uhuni huku wanaofanya hivi wakijua fika kwamba njia wanayotupeleka ni ya shari na siyo ya kheri!!!

Kama Rais, waziri mkuu, mawaziri, wabunge, jaji mkuu, mwanasheria mkuu na washauri wengine wa waheshimiwa wana nafasi ya kuonesha hekima na busara basi ni leo Jumatatu, tarehe 14, Novemba 2011 ni KUSALIMU AMRI NA KURUHUSU MSWAADA HUU USOMWE MARA YA KWANZA NA SIYO YA PILI!!!

Monday, May 2, 2011

Yamahitajika Mapinduzi ya Uongozi ngazi za chini

KUNA tabia iliyojengeka miongoni mwa Watanzania kwa baadhi yao kujiona bora na hivyo kuona kwamba nafasi au vyeo vya chini katika uongozi sio laiki yao. Kwa sababu wenzetu hao wanajiona wamesoma sana, matajiri sana au wana vyeo vikubwa sana basi wanawaachia watu wasiosoma, masikini na wanyonge nafasi za uongozi katika ngazi za chini kama vile usimamizi wa nyumba kumi, ukatibu kata, uenyekiti wa mitaa na udiwani. Wao wote wanakimbilia kuwa wabunge, wawakilishi na maraisi japo wanajua fika nafasi hizo ni chache mno na kwamba uongozi si lazima uwe mbunge au waziri au rais wa nchi. Chukulia mfano wa Zanzibar kuna wagombea wengi tu ambao wangelifaa kuwa wakuu wa mikoa na wakaleta mabadiliko ya kweli katika jamii lakini hawataki nafasi hiyo ila wanataka tu urais. Kuna nini Ikulu na kwenye bunge ndugu zetu ? Kwanini vipaji hivyo msivitumie kwenye ngazi ya mkoa na wilaya ? Au mwadhani nafasi zimejaa ? Matokeo yake ni kwamba taifa zima katika ngazi za chini halina viongozi ambao wanajua menejimenti, uongozi (leadership), utawala (governance) achilia mambo kama uchumi, sosholojia, saikolojia, usimamizi wa bajeti na fedha, kompyuta na teknohama, teknolojia nyingine za miaka hii na mlolongo wa mengi mengineyo yanayohitajika katika dunia ya siku hizi ili kuleta mabadiliko ya kina na kimsingi katika jamii inayoongozwa.

Funzo ambalo ningelipenda lijulikane asubuhi na mapema na dhamira kuu ya insha hii ni kwamba bila kuwa na viongozi walioelimika, walioridhikia kimaisha na wanaojua kutofautisha kati ya kutumiwa na viongozi na kuongoza wenyewe nchi hii haitaondokana na umasikini wa kutupwa kwa miaka mingi ijayo.

Kwa maneno mengine, mapinduzi ya kweli ya kiungozi yatakuja tu pale tutakapokuwa na viongozi wa ngazi za chini wanaojua uongozi, uchumi, nadharia tofauti za njia, mbinu, mikakati ya maendeleo na elimu zinazoendana na masuala kama hayo. Hawa watakuwa ni viongozi wanaoweza kuunda baraza la mawaziri la mkoa na ambao wanaweza wakahoji maamuzi yanayofanywa na bunge la taifa na baraza la mawaziri la taifa kwa kuwa wana elimu sawa na walioko juu, ingawa wao zaidi ni katika lugha mama ya taifa, Kiswahili.

Isitoshe uongozi wa namna hii ukipatikana katika ngazi ya chini kabisa itakuwa ni rahisi kutathmini viongozi na kuwapa dhamana kubwa zaidi kulingana na mafanikio yao katika ngazi za chini.

Chini ya Uongozi wa kijamaa Watanzania wengi waliokuwa na elimu, vyeo na mali walikataa katakata kugombea nafasi za ujumbe wa nyumba kumi,udiwani na uongozi wa mitaa. Ikawa ni kawaida kwa nafasi hizo kuchukuliwa na watu wasiokuwa na elimu au wenye elimu ndogo sana; wasiowahi kushika cheo chochote na waliokuwa wanaongoza kwa umasikini na hali ngumu ya maisha katika mitaa yao.

Hali hiyo ukienda leo kwenye mikoa mbalimbali na hasa huko vijijini bado ipo na inaendelea. Swali la kujiuliza ni kwamba ikiwa familia, mitaa na vijiji ndio msingi au matofali ya msingi ya taifa leltu hivi kweli tunaweza kujenga taifa lililo imara kisiasa na madhubuti kiuchumi, kijamii, kitekonoojia na kijeshi endapo uongozi wake unashikwa na watu sampuli hii ?

Ieleweke kwamba siwadharau hata kidogo wale walioshika dhamana hii pale ambapo matajiri, wasomi na watu wengine wenye majina walipoidharau na kuikataa. Ila kutokana na mabadiliko ya wakati ambapo sasa Tanzania ni sehemu tu kiuchumi katika ulimwengu mkubwa zaidi naona upo umuhimu wa kujitazama na kujipanga upya ili tuweze kuzikabili changamoto mbalimbali za maendeleo zinazotukabili.

Pengine kuna kosa la kiufundi lililofanyika katika ugawaji dhamana na maslahi yanayoendana na hili. HIvi anayestahili kulipwa mshahara mzuri ni kiongozi wa ngazi ya chini kabisa (ambaye anaweza kuibadili hali ya watu wake toka umaskini au daraja la tatu wakawa la pili au la kwanza) au kiongozi wa ngazi ya juu ambaye nadra kuwa na mawasiliano na wananchi huko waliko?

Ukweli ni kuwa viongozi wetu wa nyumba kumi, wenyeviti wa mitaa na makatibu kata wote elimu yao, uzoefu wao, uono wao na ufahamu wao wa dunia ya utandawazi bado uko chini kwa upande mmoja. Na kwa upande wa pili maslahi na motisha yao ya kuleta mabadiliko ya kimsingi katika jamii zao ni sawa na hamna au ni kidunchu mno. Hii haina tofauti na mameneja, makocha na viongozi wengine wa timu ya michezo kulipwa mara kumi au ishirini ya wachezaji halafu timu ikawa inadorora mwaka nenda, mwaka rudi -halafu unatafuta mchawi nje yenu !

Viongozi au watu wanaoitwa viongozi katika ngazi za chini kwenye nchi hii ni watu wasiolipwa mishahara; hawana elimu ya kutosha kuongoza na kuleta mabadiliko katika jamii; hawana ari, motisha wala moyo wa kufanya kazi; hawana ujuzi na uzoefu katika kazi wanazozifanya na wala hakuna taasisi iliyojipanga au kupangwa kuwafunza na kuwaendeleza.

Viongozi hao wa chini wengi ni masikini kiasi cha kutisha kiasi ambacho sio tu wana vishawishi vingi bali pia wanakuwa sio amana bali deni kwa taifa na hasa pale wageni toka nje ya eneo lao au nje ya nchi wanapokuja na kitita cha fedha na kuwashawishi zaidi. Au wanapotishwa na viongozi wa ngazi ya kitaifa hadi kuwadhulumu na kuwaonea watu wao wenyewe.

Hata tupate viongozi wa kitaifa ambao wote ni maprofesa lakini huku chini tuna watu wasiosoma, masikini na wenye ujuzi sawa na hamna katika masula ya uchumi, biashara, uwekezaji, ujasiriamli, menejimenti, usimamizi wa fedha, sheria na kadhalika nchi yetu haiwezi kamwe kuendelea.
Tutajenga kama mataifa mengine yaliyopotea kizazi cha viongozi wanaorithiwa na watoto wao mwaka nenda, mwaka rudi. Ni mwanzo wa kuwa na nchi ambayo itakubali na itaendelea kukubali uongozi mbovu kwa sababu mfumo uliopo hauna chachu wala changamoto inayoiwezesha kupata fikra mbadala na viongozi wenye misimamo na mitazamo mipya na inayobadilika na wakati.

Kazi zao nyingi hazina usaidizi wa aina yoyote ile ukiwa ule wa zana, fedha au rasilimali watu. Na kwa hiyo, kwa wakati mwingi ni sehemu ndogo ya yale yaliyostahili kuwa majukumu yao yanatekelezwa kikamilifu.

Wrengi wanajiona wanatumika zaidi kisiasa na baadhi yao wanaamini pengine kile walichostahili kulipwa huliwa na wale walio juu yao. Zaidi ya hilo mara chache sana maamuzi yana sauti katika masuala mbalimbali. Kwa hiyo huiona zaidi ni yoyo kuliko watu wenye sauti katika mambo mengi yanayowazunguka. Nafuu kwao huja wakati wa chaguzi kwani ndipo wanapoweza kupambanisha pande mbalimbali na kuzikamua angalau wapate maziwa ya watoto.

Huu ni wakati mzuri wa kujiuliza, hivi, kama viongozi wa ngazi za chini wangekuwa na elimu, maarifa na uono sawa na wale wa juu majimbo yetu ya uchaguzi yangelikuwa kama hivi yalivyo. Na, je ni mtaji kwa serikali kwa wananchi vijijini kuwa mbumbumbu wa faida za siasa za ushindani ? Na wabunge tunaowapata kwa mfumo huu wa sasa wangelikuwa ndio hao hao katika mazingira ambayo kuna wasomi kushinda wao katika ngazi za uongozi wa chini ?

Ni rahisi kuelewa kwa nini hakuna anayetaka kugombea nafasi za kuwa mjumbe wa nyumba kumi au balozi au diwani au mwenyekiti wa serikali ya mtaa. Kwa upande mwingine kila mtu anataka kugombea ubunge, uwakilishi na urais. Hata hao waliopo asilimia 80 ya muda wao hutumika kujitafutia riziki kwingineko na ni kama asilimia 20 tu ndiyo hutumika kuangalia mambo ya wananchi/serikali.

Kutokana na ukweli huu kwamba kuna mfumo na hali ambayo inasababisha watu watake kugombea ubunge, uwakilishi na urais lakini hakuna wanaotaka kugombea ubalozi wa mitaa au uenyekiti wa mtaa ni dhahiri kuwa ipo haja ya kuleta mapinduzi makubwa ya uongozi katika ngazi za chini ikiwa kama kweli tunataka tujikwamue na hali hii ya kuwa masikini wakubwa duniani. Na uongozi wowote (uwe wa chini au wa juu) lazima uwe ni kazi au tarafu inayolipwa kima mahsusi kinachowawezesha viongozi hao wote kujitoa kwa hali na mali kutimiza zaidi majukumu yao ya kikazi kuliko ya kibinafsi.

Tuanze na utafiti na ushauri

Ninapendekeza kuwa Chuo Kikuu cha Mzumbe kikishirikiana na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania chenye tawi karika kila mkoa waanze kwa utafiti na ushauri katika kila mkoa kuona ni namna gani tunavyoweza kuongeza hatua kwa hatua, ubora wa viongozi waliopo na wakati huo huo kuwashawishi watu wenye uwezo, elimu na ujuzi zaidi kukubali kuwa wajumbe wa nyumba kumi na viongozi wa serikali za mitaa. Bila kuwasahau madiwani wetu. Baada ya kazi za utafiti na ushauri yaanze mafunzo na uandaaji wa mipango ya urithishaji uongozi kwa namna ambayo kila mtaa, kila kata inapata kiongozi anayestahili kushika nafasi hiyo.

Ninaamini ya kwamba, masomo kama vile yale ya uchumi, uongozi( leadership) utawala (governance) , uangalizi wa fedha, menejimenti, sayansi ya jamii, usimamizi rasilimali watu, mipango, udhibiti, sayansi ya maamuzi na kadhalika hayatakosekana na yatatolewa kwa lugha mama ya Watanzania, yaani, Kiswahili.

Sio rahisi bila ya nafasi za uongozi katika ngazi za chini kushikwa na watu wenye ujuzi, elimu na uono mpana wa dunia hii ya utandawazi kwa watu wetu kuamka na kufanya kile kinachotakikana kama majibu yetu kwa mfumo wa uchumi, biashara na teknolojia unaogeuka kila kuchwao.

Mapinduzi ya uongozi Tanzania yataanza pale itakapogundulika kuwa nafasi hizo si za wanasesere au vibarakala(puppets) bali za watu muhimu mno katika kuikwamua Tanzania kutoka kwenye umaskini na wanaostahili kupewa ila nyenzo ili waweze kuhamasisha watu na jambo hilo likafanyika bila kusubiri ziara na misaada ya wakubwa toka makao makuu ya nchi yawayo.

Saturday, April 30, 2011

Mishahara, Maendeleo na Rasilimali Watu

Ibara ya 23 katika kifungu (1) inabainisha kwamba: "Kila mtu, bila ya kuwapo ubaguzi wa aina yoyote,
anayo haki ya kupata ujira unaolingana na kazi yake, na watu
wote wanaofanya kazi kulingana na uwezo wao watapata malipo
kulingana na kiasi na sifa za kazi wanayoifanya."

Kifungu hiki kinahitaji kupanuliwa ili kutoacha sintofahamu katika masuala muhimu ya ajira, ujira na maslahi ya wafanyakazi.

a) Malipo ya haki ni yepi, yanapimwa vipi, yanarekebishwa vipi na kiwango kinabadilikaje kutokana na mabadiliko katika uchumi na jamii?
b) Kwanini watu wenye ngozi nyeupe, toka nje wanalipwa vizuri kuliko ngozi nyeusi na wazawa kiujumla? Ubaguzi wa aina yoyote hautakiwa kukubalika isipokuwa kama ni ubaguzi wa kumpendelea mzawa.
b) Ni lazima mishahara ioanishwe na kapu la mahitaji ya msingi ya mtu, na kiwango hiki cha chini cha mahitaji ya msingi ndio kiamue ujira wa chini na sio kiwango hiko kuwekwa jinsi wakubwa watakavyo.
c) Mishahara na mapenzi ya rais visiunganishwa. Isiendelee kuonekana kama watu wanapata mishahara kutokana na huruma ya kiongozi huyo.
d) Machelewesho yote ya mfanyakazi au mtumishi wa umma yalipwe riba kwa muda wote utakaocheleweshwa.
e) Makato kwenda NSSF,PPF, LAPF na kwingineko kama huko yawe na kiasi fulani cha ununuzi wa hisa wa mashirika husika. Kinachofanyika hivi sasa ni kuwa wakatwa michango ndio wamiliki wanaostahili, lakini wanaofaidi faida za umilikaji ni serikali na wengineo na sio mwananchi anayestahili kuwa mmilikaji wa mashirika hayo.
f) Mtu yeyote mwenye elimu na ujuzi unaostahili kumfanya aajiriwe lakini hana ajira awe analipwa kiwango na mahitaji ya msingi kwake na familia yake.
g) TUMEWABEBA sana viongozi kwa kuwalipa MISHAHARA MIKUBWA kuliko kazi wanayoifanya katika kuondoa umaskini, ujinga, maradhi na nchi yetu kubaki nyuma kimaendeleo. Kama mwalimu alivyofanya mwaka 1966/7 viongozi wetu walikubali hili; wajione ni wanyonyaji; na mishahara yao iwe nusu kama sio robo ya hii ya leo na iwe inaongezeka kutokana na michango yao katika kuondoa ujinga, umaskini, maradhi katika maeneo yao husika.
h) Wabunge walipwe mishahara inayoendana na elimu, ujuzi na kazi zao za mwisho walizoajiriwa kabla ya kuingia bungeni. Kwa utaratibu huu tutawaondoa wale wote wanaotaka kutajirika kupitia ubunge na siasa.
Wafanyabiashara wote wanaojiingiza katika siasa watatakiwa kujilipa wenyewe bila kugusa senti toka hazina.

i) Ili kujivunia rasilimali watu zetu wenyewe kama Imarati inavyofanya hata pakiwa na bosi toka nje, Mtanzania aliyeko chini yake na anayejifunza kutoka kwake alipwe vizuri kuliko huyo mgeni.
j) Madaktari, manesi, walimu, wahadhiri, wanajeshi na polisi ambao kazi zao haziwaruhusu kufanya (kwa haki) zaidi ya lile waliloajiriwa kama tunataka lifanyike vizuri walipwe mishahara mizuri tu inayowafanya wasitamani kufanya kitu kingine
k) Tofauti kati ya viongozi wa juu na viongozi wa chini na wananchi wengine katika mafao yao baada ya kustaafu yatazamwe na yasipishane kwa kiasi kikubwa na cha kutisha.
l) Wakuu wa mikoa na wilaya kama hawatachaguliwa na wakazi wa mikoa na wilaya husika walipwe na chama tawala.
m) Mishahara miwili iwe marufuku, badala yake mtu apate alawansi inayostahili.
n) Pawe na utaratibu ambao utahakikisha mishahara na mafao ya wafanyakazi ( k.m. EAC) hailiwi na wajanja wachache.
o) Uongezaji mishahara kwa viongozi uendane na jinsi serikali na watumishi wake wanavyochangia kukuza pato la taifa. Likipungua mishahara hiyo ishuke. Likikua mishahara hiyo ipande.