Kwanini tunasema katiba ni mali ya wananchi ?
HUFIKA wakati katika historia ya nchi ikawalazimu viongozi waliopo kukaa pembeni na kuwaachia wananchi madaraka au mamlaka ya kufanya maamuzi muhimu ya kitaifa. Mojawapo ya wakati kama huo ni pale nchi inapotka kuwa na katiba mpya. Kwa kuwa wananchi ndio wenye sauti ya mwisho na maamuzi makuu katika suala hili ni uungwana, haki na kuona mbali na mbele kwa viongozi waliokuwepo kusalimu amri kwa wananchi na kuwakabidhi kupitia watu ambao wananchi wenyewe watakaowachagua kuwawakilisha katika kuandaa utaratibu mzima toka kuanza hadi kumaliza kazi ya kupata mchakato wa njia na namna za kuipata katiba na vilevile upatikanaji wa toleo la mwisho la katiba mpya litakalopigiwa kura na wananchi.
Hii ni hatua inayohitaji viongozi wanaojiweka zaidi kama viongozi wa kitaifa na wafanya maamuzi makuu yatakayoathiri maisha ya kizazi hiki na vizazi vijavyo kwa wema au ubaya. Wanaoshindwa kufanya hili hawatendei haki wajibu na majukumu wanayostahili kuyabeba kama viongozi wa watu na nchi yao.
Uongozi unaoshindwa kutambua kwamba muda wa KUSALIMU AMRI KWA WANANCHI WAKE umefika ni uongozi wenye hatari ya kuiingiza nchi kwenye matatizo makubwa ya kisiasa, kijamii na kiuchumi. Ni uongozi usiotakia kheri kizazi kilichopo na vizazi vijavyo katika nchi husika.
Ukubwa mlionao
Ukubwa mlionao, mmepewa na wananchi,
Hawa ndio waamuao, hatima yenu na nchi,
Na muda wautakao, huwapeleka benchi,
Wafanye maazimio, kula mbivu au mbichi,
Ukubwa muutakao,kwa nachi na upanchi,
Hamjui mfanyayo,si wananchi ni wenyenchi,
Ni hasama mleltao,wana waje enda uchi,
Hayo kama matamanio,iwe kucha haukuchi,
Fanyeni wayatakayo,Tanzania wananchi,
Na siyo muyatakayo,mlio kwenye makochi,
Taabu si mjuao,wala hamli vibichi,
Sio muhangaikao,ni rahisi zenu mechi,
Na sio muelewao,nini hatima ya nchi!
Akizungumzia uwezekano wa kuandikwa katiba mpya ya Tanzania kwa mara yake ya kwanza, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti na mwanachama wa Chama kimojawapo cha siasa nchini Tanzania, CCM, Bwana Jakaya Kikwete pamoja na mambo mengine alionesha kutamani sana kwamba katiba itakayoandikwa iweze kutufaa kwa miaka 50 kama sio 100. Hata hivyo, kile kilichowasilishwa na Waziri wake wa katiba hakikufanana kabisa na matamanio mema yake hayo.
Tofauti na msimamo huu wa mheshimiwa Rais, muswada wa serikali yake kwa bunge la Jamhuri ulidhihirisha nia ya serikali ya Chama cha Mapinduzi kuitumia fursa hiyo ili iweze kujikita vyema zaidi nchini kwa halali au haramu kisiasa kwa kuwatumia wabunge wao ambao ilionekana kama walishapewa mafunzo maalum kuhusu kinachotegemewa kutoka kwao.
Pamoja na spika wa bunge hilo kudai kwamba wanaharakati, wapinzani na waandishi wa habari wanapotosha kilicho mezani mwa wabunge, kazi nzuri ya uchambuzi wa kina iliyofanywa na Mheshimiwa Tundu Lissu (CHADEMA) ilionesha kulikuwa na uwezekano mkubwa wa wabunge wa CCM kutokuwa wameusoma muswada huo na Tundu akawa anapigia gitaa mbuzi.
Pengine wabunge wa CCM walishaambiwa kwamba ni lazima upite kama ulivyo na hakuna aliyesumbuka kuusoma kikwelikweli, lakini baadaye ilidhihirika waziwazi kwamba muswada huo ulikuwa na udhaifu mkubwa na kasoro nyingi za kimaudhui, kisheria, kisiasa na kikanuni kikatiba ambao kwa watunga sheria makini lazima wangelihitaji muda wa ziada wa kuufanyia kazi na sio kama wenzetu walivyoanza kuchangia wakiwa na uelewa 'finyu kiuzalendo' kwa kazi iliyokwa mbele yao.
Sio siri kwamba CCM inachokitaka pengine ni kujihakikishia uzima wa milele. Kitu ambacho hakiwezekani. Na haitawezekana kwa sababu hizi si zama za Nyerere, Mkapa na Mwinyi na chochote kinaweza kutokea kwa watu ambao hali ya uchumi inawawia ngumu kila kukichwa, mali asili zao zinatwaliwa bure, watu wanauawa na kubakwa migodini na wakubwa wanapora fedha, wanyama pori, miti, ardhi na rasilimali nyingine kwa jinsi wanavyotaka. Na wasichonacho wananyang'anywa hata kile kidogo walicho nacho, wakati wenye nacho wanazidi kuongezewa kila siku.
Watanzania hawatakaa wasahau kwamba kunako mwezi Novemba, mwaka 2011 baadhi ya wabunge wao kupitia CCM walipoteza fursa ya kipekee katika kuutanguliza Utanzania mbele ya nafsi na uchama wao. Matokeo ya ubinafsi na uchama wao yakawapotezea fursa hii adhimu ambayo ingeliwaweka pazuri sana katika historia ya nchi yao na watu wake.
Kilichotokea ni kwa wabunge hao wa CCM-CUF kuonesha dhahiri kuwa ni mbwa-mwitu (wawakilishi wa chama na serikali) waliovaa ngozi ya kondoo (wawakilishi wa wananchi). Kipaumbele siku hiyo hakikupewa wananchi na vizazi vyao vijavyo bali chama, matashi yake na ubinafsi wa wabunge hata kama Watanzania kwa ujumla wao watapoteza kikubwa zaidi siku zijazo.
UCCM na UCUF kwa kiasi fulani katika hili umewafanya wengi waamini kuwa wabunge wa vyama hivyo wanastahili kupata shahada ya udaktari katika uchama, usisi, umimi na katika mapambano ya maslahi na maendeleo ya wabunge binafsi.
Kwa maneno mengine, wabunge wa CCM na CUF walikuwa wakituambia kwamba vyama vyao na uongozi wa chama chao ni muhimu kuliko Utanzania wetu au utaifa wetu, watu wetu na vizazi vyetu vijavyo.
Kubwa zaidi ni lile la spika, muwakilishaji muswada na wabunge wa CCM waliochangia muswada huo kusingizia eti kuna urongo, uzushi, upotoshaji na tafsiri mbovu ya kile kilichotakiwa kuwakilishwa. Haraka aliyokuwa nayo spika, wabunge wa CCM kuchangia na mwasilisha muswada na wenzake kuliacha maswali mengi kuliko majibu. Mwisho wa siku kilio cha spika, muwasilisha mada na wabunge wa CCM na CUF kilifanana na kile kilio cha mchunga kondoo aliyekuwa akisumbua wanakijiji wenzake kwa kupiga mayowe ya MBWA MWITU, MBWA MWITU kumbe yote ilikuwa ni mzaha kama sio urongo.
Uzaini wa CCM wa kujionesha eti wana CCM na viongozi wao wanaipenda na wana uchungu sana na Tanzania kuliko watu wengine umewafanya jamaa hao kuangukia pua katika siku ambayo wengi wao hawataiashau na wao wenyewe wameamua kujizika kihistoria.
CCM na wakewenza Unguja
Baya zaidi ni lile la muswada huo kudiriki kuifanya Zanzibar kuwa sawasawa na Tanganyika isiyopo katika kuamua hatima ya nchi yetu na watu wake. Hiki ni kitendo cha waendesha utumwa, kikoloni, kibabe, kihuni na cha kidhalimu ambacho hakistahili kukubalika.
Kwani nia ya kuwapa ukubwa huu Wazanzibari wasiostahili kuupata ni kurahisisha siasa ndani ya CCM kati ya Wazanzibari na Wabara. Kwa maneno mengine, CCM imediriki kuwauza Watanganyika kwa Wazanzibari, kama walivyouza migodi ya dhahabu, ili mradi tu mambo yao yawe safi.
Ukewenza Zanzibar na Serikali ya JMT, unatuweka pabaya kitamathali na kiuyakinifu kwa kiasi cha eti watu asilimia 2 Tanzania kuamua hatima ya asilimia 98 iliyobakia.
Kwa maneno mengine, muswada huo unawageuza Wazanzibar wakoloni na Watanganyika watawaliwa katika nchi yao wenyewe. Sijui hata kama muswada huo utapita kama hili litakaa likubalike kesho na keshokutwa.
Hadhi ya Zanzibar kiukweli haina tofauti na ya mkoa wowote bara. Tofauti tu ni kuwa mikoa inabanwa kuwa huru kisiasa, kijamii na kiuchumi kwa mafaniko yake makubwa na haraka zaidi. Kilichokosekana ni uamsho kwa wakazi mikoani na uadilifu kwa serikali kuipa mikoa serikali huru zinazosimamiwa na waziri mkuu wa mkoa, baraza la mawaziri wa mkoa na wawakilishi wa mkoa na mikoa mingi tu ingeiacha Zanzibar nyuma kimaendeleo, bila ya visiwa hivyo kuona hata indiketa za mikoa hiyo kwenye mbio za ustawi wa jamii na maendeleo ya mkoa.
Itakuwa ni jambo la fedheha kama wabunge na serikali yetu baada ya kushindwa kuafikiana na wapinzani wa kweli ndani ya bunge itakuja kufanza hivyo kwa kupata shinikizo toka Marekani na EU. Jambo hili litaonesha kwamba viongozi wetu hawajaiva wala kukomaa na hakika hawastahili kuiongoza nchi hii kama kweli tunataka kuendelea na umoja na amani tuliyo nayo hivi leo. Kinachoonekana hapa ni kwamba kuna Watanzania wenye akili na uwezo mkubwa tu lakini kwa kukosa uongozi adilifu na mzuri wanashindwa kuwatumia.
Viongozi wa dini
Viongozi wa dini kama ilivyokuwa kwa wenzetu nchini Kenya wana mchango mkubwa katika kuhakikisha Tanzania inakuwa na katiba nzuri na safi na itakayowafaa Watanzania kwa muda mrefu kuliko hii ya kupandikizwa ilivyotsukuma sukuma.
Yapo mambo kadhaa ambayo viongozi wa dini wanaowatakia Watanzania na vizazi vyao amani na umoja wanaweza kuhoji na kutoa mwongozo yaende vipi kwa faida ya watu wote. Mathalani, hivi leo kanisa katoliki linafanya vizuri sana katika elimu na sekta ya afya, lakini siasa za uziwi na upofu zinaweza kuhujumu haya yote kama katiba isipohifadhi sheria na haki muhimu za kulinda kanisa, mali zake na viongozi wake. Misikiti na Makanisa yakikaa nyuma, viongozi wa dini wasije anza kulalama baadaye kwamba katiba imewapendelea hawa, au kuwaonea hawa.
Makampuni na taasisi na katiba
Makampuni na taasisi kisheria ni sawa na mtu au raia. Makampuni na taasisi zikikaa nyuma na kutokushiriki kwenye mchakato wa katiba mpya yapo masuala mengi yanayoweza kuja kuzuka baadaye kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni yakaya kuwa ni kwa hasara kubwa kwa upande wao.
Katika suala hili lal katiba mpya sisi sote ni wadau na washiriki na hakuna anayestahili kubakia kuwa mtazamaji tu au juu ya wenzake kwa namna yoyote ile.
Muswada huu kama ilivyokuwa kwa miswaada mingine dhaifu, inayovuja na dhalimu kwa wananchi na vizazi vijavyo, imedhirisha mapungugu mengi mengine katika muundo, mifumo na taratibu zetu za uongozi na uendeshaji nchi. Baadhi ya kasoro hizi ni pamoja na hatari ya kuwa na wabunge wa kuteuliwa badala ya kuchaguliwa kwenye bunge la kiwakilishi; jinsi ambavyo serikali iliyoko madarakani inaweza ikapora mamlaka na madaraka ya wananchi na kufanya mapinduzi ya kikatiba bila kuwajibishwa ipasavyo; muungano unavyozidi kuonekana kukosa maana kwa Watanganyika na kuwa mzigo usiobebeka; na ule ukweli kuwa nchi bado imo kizani na haijajaliwa kuwa na kiongozi na wanasiasa wanaoweza kututoa kwenye shimo refu la giza ambalo tumejikuta tumo leo.
HUU ni mchango wangu katika kusaidia kuwepo kwa katiba bora nchini itakayoweza kutumika sio tu kwa miaka hamsini lakini hata kwa karne kumi na zaidi. Katiba itakayosimama kama katiba na sio matakwa ya mtu fulani au chama fulani hapa nchini.
Thursday, November 17, 2011
Muswada wa katiba ni waCCM na serikali yake na hauna nia njema na Watanzania wa sasa na wajao......
Kwanini tunasema katiba ni mali ya wananchi ?
HUFIKA wakati katika historia ya nchi ikawalazimu viongozi waliopo kukaa pembeni na kuwaachia wananchi madaraka au mamlaka ya kufanya maamuzi muhimu ya kitaifa. Mojawapo ya wakati kama huo ni pale nchi inapotka kuwa na katiba mpya. Kwa kuwa wananchi ndio wenye sauti ya mwisho na maamuzi makuu katika suala hili ni uungwana, haki na kuona mbali na mbele kwa viongozi waliokuwepo kusalimu amri kwa wananchi na kuwakabidhi kupitia watu ambao wananchi wenyewe watakaowachagua kuwawakilisha katika kuandaa utaratibu mzima toka kuanza hadi kumaliza kazi ya kupata mchakato wa njia na namna za kuipata katiba na vilevile upatikanaji wa toleo la mwisho la katiba mpya litakalopigiwa kura na wananchi.
Hii ni hatua inayohitaji viongozi wanaojiweka zaidi kama viongozi wa kitaifa na wafanya maamuzi makuu yatakayoathiri maisha ya kizazi hiki na vizazi vijavyo kwa wema au ubaya. Wanaoshindwa kufanya hili hawatendei haki wajibu na majukumu wanayostahili kuyabeba kama viongozi wa watu na nchi yao.
Uongozi unaoshindwa kutambua kwamba muda wa KUSALIMU AMRI KWA WANANCHI WAKE umefika ni uongozi wenye hatari ya kuiingiza nchi kwenye matatizo makubwa ya kisiasa, kijamii na kiuchumi. Ni uongozi usiotakia kheri kizazi kilichopo na vizazi vijavyo katika nchi husika.
Ukubwa mlionao
Ukubwa mlionao, mmepewa na wananchi,
Hawa ndio waamuao, hatima yenu na nchi,
Na muda wautakao, huwapeleka benchi,
Wafanye maazimio, kula mbivu au mbichi,
Ukubwa muutakao,kwa nachi na upanchi,
Hamjui mfanyayo,si wananchi ni wenyenchi,
Ni hasama mleltao,wana waje enda uchi,
Hayo kama matamanio,iwe kucha haukuchi,
Fanyeni wayatakayo,Tanzania wananchi,
Na siyo muyatakayo,mlio kwenye makochi,
Taabu si mjuao,wala hamli vibichi,
Sio muhangaikao,ni rahisi zenu mechi,
Na sio muelewao,nini hatima ya nchi!
Akizungumzia uwezekano wa kuandikwa katiba mpya ya Tanzania kwa mara yake ya kwanza, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti na mwanachama wa Chama kimojawapo cha siasa nchini Tanzania, CCM, Bwana Jakaya Kikwete pamoja na mambo mengine alionesha kutamani sana kwamba katiba itakayoandikwa iweze kutufaa kwa miaka 50 kama sio 100. Hata hivyo, kile kilichowasilishwa na Waziri wake wa katiba hakikufanana kabisa na matamanio mema yake hayo.
Tofauti na msimamo huu wa mheshimiwa Rais, muswada wa serikali yake kwa bunge la Jamhuri ulidhihirisha nia ya serikali ya Chama cha Mapinduzi kuitumia fursa hiyo ili iweze kujikita vyema zaidi nchini kwa halali au haramu kisiasa kwa kuwatumia wabunge wao ambao ilionekana kama walishapewa mafunzo maalum kuhusu kinachotegemewa kutoka kwao.
Pamoja na spika wa bunge hilo kudai kwamba wanaharakati, wapinzani na waandishi wa habari wanapotosha kilicho mezani mwa wabunge, kazi nzuri ya uchambuzi wa kina iliyofanywa na Mheshimiwa Tundu Lissu (CHADEMA) ilionesha kulikuwa na uwezekano mkubwa wa wabunge wa CCM kutokuwa wameusoma muswada huo na Tundu akawa anapigia gitaa mbuzi.
Pengine wabunge wa CCM walishaambiwa kwamba ni lazima upite kama ulivyo na hakuna aliyesumbuka kuusoma kikwelikweli, lakini baadaye ilidhihirika waziwazi kwamba muswada huo ulikuwa na udhaifu mkubwa na kasoro nyingi za kimaudhui, kisheria, kisiasa na kikanuni kikatiba ambao kwa watunga sheria makini lazima wangelihitaji muda wa ziada wa kuufanyia kazi na sio kama wenzetu walivyoanza kuchangia wakiwa na uelewa 'finyu kiuzalendo' kwa kazi iliyokwa mbele yao.
Sio siri kwamba CCM inachokitaka pengine ni kujihakikishia uzima wa milele. Kitu ambacho hakiwezekani. Na haitawezekana kwa sababu hizi si zama za Nyerere, Mkapa na Mwinyi na chochote kinaweza kutokea kwa watu ambao hali ya uchumi inawawia ngumu kila kukichwa, mali asili zao zinatwaliwa bure, watu wanauawa na kubakwa migodini na wakubwa wanapora fedha, wanyama pori, miti, ardhi na rasilimali nyingine kwa jinsi wanavyotaka. Na wasichonacho wananyang'anywa hata kile kidogo walicho nacho, wakati wenye nacho wanazidi kuongezewa kila siku.
Watanzania hawatakaa wasahau kwamba kunako mwezi Novemba, mwaka 2011 baadhi ya wabunge wao kupitia CCM walipoteza fursa ya kipekee katika kuutanguliza Utanzania mbele ya nafsi na uchama wao. Matokeo ya ubinafsi na uchama wao yakawapotezea fursa hii adhimu ambayo ingeliwaweka pazuri sana katika historia ya nchi yao na watu wake.
Kilichotokea ni kwa wabunge hao wa CCM-CUF kuonesha dhahiri kuwa ni mbwa-mwitu (wawakilishi wa chama na serikali) waliovaa ngozi ya kondoo (wawakilishi wa wananchi). Kipaumbele siku hiyo hakikupewa wananchi na vizazi vyao vijavyo bali chama, matashi yake na ubinafsi wa wabunge hata kama Watanzania kwa ujumla wao watapoteza kikubwa zaidi siku zijazo.
UCCM na UCUF kwa kiasi fulani katika hili umewafanya wengi waamini kuwa wabunge wa vyama hivyo wanastahili kupata shahada ya udaktari katika uchama, usisi, umimi na katika mapambano ya maslahi na maendeleo ya wabunge binafsi.
Kwa maneno mengine, wabunge wa CCM na CUF walikuwa wakituambia kwamba vyama vyao na uongozi wa chama chao ni muhimu kuliko Utanzania wetu au utaifa wetu, watu wetu na vizazi vyetu vijavyo.
Kubwa zaidi ni lile la spika, muwakilishaji muswada na wabunge wa CCM waliochangia muswada huo kusingizia eti kuna urongo, uzushi, upotoshaji na tafsiri mbovu ya kile kilichotakiwa kuwakilishwa. Haraka aliyokuwa nayo spika, wabunge wa CCM kuchangia na mwasilisha muswada na wenzake kuliacha maswali mengi kuliko majibu. Mwisho wa siku kilio cha spika, muwasilisha mada na wabunge wa CCM na CUF kilifanana na kile kilio cha mchunga kondoo aliyekuwa akisumbua wanakijiji wenzake kwa kupiga mayowe ya MBWA MWITU, MBWA MWITU kumbe yote ilikuwa ni mzaha kama sio urongo.
Uzaini wa CCM wa kujionesha eti wana CCM na viongozi wao wanaipenda na wana uchungu sana na Tanzania kuliko watu wengine umewafanya jamaa hao kuangukia pua katika siku ambayo wengi wao hawataiashau na wao wenyewe wameamua kujizika kihistoria.
CCM na wakewenza Unguja
Baya zaidi ni lile la muswada huo kudiriki kuifanya Zanzibar kuwa sawasawa na Tanganyika isiyopo katika kuamua hatima ya nchi yetu na watu wake. Hiki ni kitendo cha waendesha utumwa, kikoloni, kibabe, kihuni na cha kidhalimu ambacho hakistahili kukubalika.
Kwani nia ya kuwapa ukubwa huu Wazanzibari wasiostahili kuupata ni kurahisisha siasa ndani ya CCM kati ya Wazanzibari na Wabara. Kwa maneno mengine, CCM imediriki kuwauza Watanganyika kwa Wazanzibari, kama walivyouza migodi ya dhahabu, ili mradi tu mambo yao yawe safi.
Ukewenza Zanzibar na Serikali ya JMT, unatuweka pabaya kitamathali na kiuyakinifu kwa kiasi cha eti watu asilimia 2 Tanzania kuamua hatima ya asilimia 98 iliyobakia.
Kwa maneno mengine, muswada huo unawageuza Wazanzibar wakoloni na Watanganyika watawaliwa katika nchi yao wenyewe. Sijui hata kama muswada huo utapita kama hili litakaa likubalike kesho na keshokutwa.
Hadhi ya Zanzibar kiukweli haina tofauti na ya mkoa wowote bara. Tofauti tu ni kuwa mikoa inabanwa kuwa huru kisiasa, kijamii na kiuchumi kwa mafaniko yake makubwa na haraka zaidi. Kilichokosekana ni uamsho kwa wakazi mikoani na uadilifu kwa serikali kuipa mikoa serikali huru zinazosimamiwa na waziri mkuu wa mkoa, baraza la mawaziri wa mkoa na wawakilishi wa mkoa na mikoa mingi tu ingeiacha Zanzibar nyuma kimaendeleo, bila ya visiwa hivyo kuona hata indiketa za mikoa hiyo kwenye mbio za ustawi wa jamii na maendeleo ya mkoa.
Itakuwa ni jambo la fedheha kama wabunge na serikali yetu baada ya kushindwa kuafikiana na wapinzani wa kweli ndani ya bunge itakuja kufanza hivyo kwa kupata shinikizo toka Marekani na EU. Jambo hili litaonesha kwamba viongozi wetu hawajaiva wala kukomaa na hakika hawastahili kuiongoza nchi hii kama kweli tunataka kuendelea na umoja na amani tuliyo nayo hivi leo. Kinachoonekana hapa ni kwamba kuna Watanzania wenye akili na uwezo mkubwa tu lakini kwa kukosa uongozi adilifu na mzuri wanashindwa kuwatumia.
Viongozi wa dini
Viongozi wa dini kama ilivyokuwa kwa wenzetu nchini Kenya wana mchango mkubwa katika kuhakikisha Tanzania inakuwa na katiba nzuri na safi na itakayowafaa Watanzania kwa muda mrefu kuliko hii ya kupandikizwa ilivyotsukuma sukuma.
Yapo mambo kadhaa ambayo viongozi wa dini wanaowatakia Watanzania na vizazi vyao amani na umoja wanaweza kuhoji na kutoa mwongozo yaende vipi kwa faida ya watu wote. Mathalani, hivi leo kanisa katoliki linafanya vizuri sana katika elimu na sekta ya afya, lakini siasa za uziwi na upofu zinaweza kuhujumu haya yote kama katiba isipohifadhi sheria na haki muhimu za kulinda kanisa, mali zake na viongozi wake. Misikiti na Makanisa yakikaa nyuma, viongozi wa dini wasije anza kulalama baadaye kwamba katiba imewapendelea hawa, au kuwaonea hawa.
Makampuni na taasisi na katiba
Makampuni na taasisi kisheria ni sawa na mtu au raia. Makampuni na taasisi zikikaa nyuma na kutokushiriki kwenye mchakato wa katiba mpya yapo masuala mengi yanayoweza kuja kuzuka baadaye kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni yakaya kuwa ni kwa hasara kubwa kwa upande wao.
Katika suala hili lal katiba mpya sisi sote ni wadau na washiriki na hakuna anayestahili kubakia kuwa mtazamaji tu au juu ya wenzake kwa namna yoyote ile.
Muswada huu kama ilivyokuwa kwa miswaada mingine dhaifu, inayovuja na dhalimu kwa wananchi na vizazi vijavyo, imedhirisha mapungugu mengi mengine katika muundo, mifumo na taratibu zetu za uongozi na uendeshaji nchi. Baadhi ya kasoro hizi ni pamoja na hatari ya kuwa na wabunge wa kuteuliwa badala ya kuchaguliwa kwenye bunge la kiwakilishi; jinsi ambavyo serikali iliyoko madarakani inaweza ikapora mamlaka na madaraka ya wananchi na kufanya mapinduzi ya kikatiba bila kuwajibishwa ipasavyo; muungano unavyozidi kuonekana kukosa maana kwa Watanganyika na kuwa mzigo usiobebeka; na ule ukweli kuwa nchi bado imo kizani na haijajaliwa kuwa na kiongozi na wanasiasa wanaoweza kututoa kwenye shimo refu la giza ambalo tumejikuta tumo leo.
HUFIKA wakati katika historia ya nchi ikawalazimu viongozi waliopo kukaa pembeni na kuwaachia wananchi madaraka au mamlaka ya kufanya maamuzi muhimu ya kitaifa. Mojawapo ya wakati kama huo ni pale nchi inapotka kuwa na katiba mpya. Kwa kuwa wananchi ndio wenye sauti ya mwisho na maamuzi makuu katika suala hili ni uungwana, haki na kuona mbali na mbele kwa viongozi waliokuwepo kusalimu amri kwa wananchi na kuwakabidhi kupitia watu ambao wananchi wenyewe watakaowachagua kuwawakilisha katika kuandaa utaratibu mzima toka kuanza hadi kumaliza kazi ya kupata mchakato wa njia na namna za kuipata katiba na vilevile upatikanaji wa toleo la mwisho la katiba mpya litakalopigiwa kura na wananchi.
Hii ni hatua inayohitaji viongozi wanaojiweka zaidi kama viongozi wa kitaifa na wafanya maamuzi makuu yatakayoathiri maisha ya kizazi hiki na vizazi vijavyo kwa wema au ubaya. Wanaoshindwa kufanya hili hawatendei haki wajibu na majukumu wanayostahili kuyabeba kama viongozi wa watu na nchi yao.
Uongozi unaoshindwa kutambua kwamba muda wa KUSALIMU AMRI KWA WANANCHI WAKE umefika ni uongozi wenye hatari ya kuiingiza nchi kwenye matatizo makubwa ya kisiasa, kijamii na kiuchumi. Ni uongozi usiotakia kheri kizazi kilichopo na vizazi vijavyo katika nchi husika.
Ukubwa mlionao
Ukubwa mlionao, mmepewa na wananchi,
Hawa ndio waamuao, hatima yenu na nchi,
Na muda wautakao, huwapeleka benchi,
Wafanye maazimio, kula mbivu au mbichi,
Ukubwa muutakao,kwa nachi na upanchi,
Hamjui mfanyayo,si wananchi ni wenyenchi,
Ni hasama mleltao,wana waje enda uchi,
Hayo kama matamanio,iwe kucha haukuchi,
Fanyeni wayatakayo,Tanzania wananchi,
Na siyo muyatakayo,mlio kwenye makochi,
Taabu si mjuao,wala hamli vibichi,
Sio muhangaikao,ni rahisi zenu mechi,
Na sio muelewao,nini hatima ya nchi!
Akizungumzia uwezekano wa kuandikwa katiba mpya ya Tanzania kwa mara yake ya kwanza, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti na mwanachama wa Chama kimojawapo cha siasa nchini Tanzania, CCM, Bwana Jakaya Kikwete pamoja na mambo mengine alionesha kutamani sana kwamba katiba itakayoandikwa iweze kutufaa kwa miaka 50 kama sio 100. Hata hivyo, kile kilichowasilishwa na Waziri wake wa katiba hakikufanana kabisa na matamanio mema yake hayo.
Tofauti na msimamo huu wa mheshimiwa Rais, muswada wa serikali yake kwa bunge la Jamhuri ulidhihirisha nia ya serikali ya Chama cha Mapinduzi kuitumia fursa hiyo ili iweze kujikita vyema zaidi nchini kwa halali au haramu kisiasa kwa kuwatumia wabunge wao ambao ilionekana kama walishapewa mafunzo maalum kuhusu kinachotegemewa kutoka kwao.
Pamoja na spika wa bunge hilo kudai kwamba wanaharakati, wapinzani na waandishi wa habari wanapotosha kilicho mezani mwa wabunge, kazi nzuri ya uchambuzi wa kina iliyofanywa na Mheshimiwa Tundu Lissu (CHADEMA) ilionesha kulikuwa na uwezekano mkubwa wa wabunge wa CCM kutokuwa wameusoma muswada huo na Tundu akawa anapigia gitaa mbuzi.
Pengine wabunge wa CCM walishaambiwa kwamba ni lazima upite kama ulivyo na hakuna aliyesumbuka kuusoma kikwelikweli, lakini baadaye ilidhihirika waziwazi kwamba muswada huo ulikuwa na udhaifu mkubwa na kasoro nyingi za kimaudhui, kisheria, kisiasa na kikanuni kikatiba ambao kwa watunga sheria makini lazima wangelihitaji muda wa ziada wa kuufanyia kazi na sio kama wenzetu walivyoanza kuchangia wakiwa na uelewa 'finyu kiuzalendo' kwa kazi iliyokwa mbele yao.
Sio siri kwamba CCM inachokitaka pengine ni kujihakikishia uzima wa milele. Kitu ambacho hakiwezekani. Na haitawezekana kwa sababu hizi si zama za Nyerere, Mkapa na Mwinyi na chochote kinaweza kutokea kwa watu ambao hali ya uchumi inawawia ngumu kila kukichwa, mali asili zao zinatwaliwa bure, watu wanauawa na kubakwa migodini na wakubwa wanapora fedha, wanyama pori, miti, ardhi na rasilimali nyingine kwa jinsi wanavyotaka. Na wasichonacho wananyang'anywa hata kile kidogo walicho nacho, wakati wenye nacho wanazidi kuongezewa kila siku.
Watanzania hawatakaa wasahau kwamba kunako mwezi Novemba, mwaka 2011 baadhi ya wabunge wao kupitia CCM walipoteza fursa ya kipekee katika kuutanguliza Utanzania mbele ya nafsi na uchama wao. Matokeo ya ubinafsi na uchama wao yakawapotezea fursa hii adhimu ambayo ingeliwaweka pazuri sana katika historia ya nchi yao na watu wake.
Kilichotokea ni kwa wabunge hao wa CCM-CUF kuonesha dhahiri kuwa ni mbwa-mwitu (wawakilishi wa chama na serikali) waliovaa ngozi ya kondoo (wawakilishi wa wananchi). Kipaumbele siku hiyo hakikupewa wananchi na vizazi vyao vijavyo bali chama, matashi yake na ubinafsi wa wabunge hata kama Watanzania kwa ujumla wao watapoteza kikubwa zaidi siku zijazo.
UCCM na UCUF kwa kiasi fulani katika hili umewafanya wengi waamini kuwa wabunge wa vyama hivyo wanastahili kupata shahada ya udaktari katika uchama, usisi, umimi na katika mapambano ya maslahi na maendeleo ya wabunge binafsi.
Kwa maneno mengine, wabunge wa CCM na CUF walikuwa wakituambia kwamba vyama vyao na uongozi wa chama chao ni muhimu kuliko Utanzania wetu au utaifa wetu, watu wetu na vizazi vyetu vijavyo.
Kubwa zaidi ni lile la spika, muwakilishaji muswada na wabunge wa CCM waliochangia muswada huo kusingizia eti kuna urongo, uzushi, upotoshaji na tafsiri mbovu ya kile kilichotakiwa kuwakilishwa. Haraka aliyokuwa nayo spika, wabunge wa CCM kuchangia na mwasilisha muswada na wenzake kuliacha maswali mengi kuliko majibu. Mwisho wa siku kilio cha spika, muwasilisha mada na wabunge wa CCM na CUF kilifanana na kile kilio cha mchunga kondoo aliyekuwa akisumbua wanakijiji wenzake kwa kupiga mayowe ya MBWA MWITU, MBWA MWITU kumbe yote ilikuwa ni mzaha kama sio urongo.
Uzaini wa CCM wa kujionesha eti wana CCM na viongozi wao wanaipenda na wana uchungu sana na Tanzania kuliko watu wengine umewafanya jamaa hao kuangukia pua katika siku ambayo wengi wao hawataiashau na wao wenyewe wameamua kujizika kihistoria.
CCM na wakewenza Unguja
Baya zaidi ni lile la muswada huo kudiriki kuifanya Zanzibar kuwa sawasawa na Tanganyika isiyopo katika kuamua hatima ya nchi yetu na watu wake. Hiki ni kitendo cha waendesha utumwa, kikoloni, kibabe, kihuni na cha kidhalimu ambacho hakistahili kukubalika.
Kwani nia ya kuwapa ukubwa huu Wazanzibari wasiostahili kuupata ni kurahisisha siasa ndani ya CCM kati ya Wazanzibari na Wabara. Kwa maneno mengine, CCM imediriki kuwauza Watanganyika kwa Wazanzibari, kama walivyouza migodi ya dhahabu, ili mradi tu mambo yao yawe safi.
Ukewenza Zanzibar na Serikali ya JMT, unatuweka pabaya kitamathali na kiuyakinifu kwa kiasi cha eti watu asilimia 2 Tanzania kuamua hatima ya asilimia 98 iliyobakia.
Kwa maneno mengine, muswada huo unawageuza Wazanzibar wakoloni na Watanganyika watawaliwa katika nchi yao wenyewe. Sijui hata kama muswada huo utapita kama hili litakaa likubalike kesho na keshokutwa.
Hadhi ya Zanzibar kiukweli haina tofauti na ya mkoa wowote bara. Tofauti tu ni kuwa mikoa inabanwa kuwa huru kisiasa, kijamii na kiuchumi kwa mafaniko yake makubwa na haraka zaidi. Kilichokosekana ni uamsho kwa wakazi mikoani na uadilifu kwa serikali kuipa mikoa serikali huru zinazosimamiwa na waziri mkuu wa mkoa, baraza la mawaziri wa mkoa na wawakilishi wa mkoa na mikoa mingi tu ingeiacha Zanzibar nyuma kimaendeleo, bila ya visiwa hivyo kuona hata indiketa za mikoa hiyo kwenye mbio za ustawi wa jamii na maendeleo ya mkoa.
Itakuwa ni jambo la fedheha kama wabunge na serikali yetu baada ya kushindwa kuafikiana na wapinzani wa kweli ndani ya bunge itakuja kufanza hivyo kwa kupata shinikizo toka Marekani na EU. Jambo hili litaonesha kwamba viongozi wetu hawajaiva wala kukomaa na hakika hawastahili kuiongoza nchi hii kama kweli tunataka kuendelea na umoja na amani tuliyo nayo hivi leo. Kinachoonekana hapa ni kwamba kuna Watanzania wenye akili na uwezo mkubwa tu lakini kwa kukosa uongozi adilifu na mzuri wanashindwa kuwatumia.
Viongozi wa dini
Viongozi wa dini kama ilivyokuwa kwa wenzetu nchini Kenya wana mchango mkubwa katika kuhakikisha Tanzania inakuwa na katiba nzuri na safi na itakayowafaa Watanzania kwa muda mrefu kuliko hii ya kupandikizwa ilivyotsukuma sukuma.
Yapo mambo kadhaa ambayo viongozi wa dini wanaowatakia Watanzania na vizazi vyao amani na umoja wanaweza kuhoji na kutoa mwongozo yaende vipi kwa faida ya watu wote. Mathalani, hivi leo kanisa katoliki linafanya vizuri sana katika elimu na sekta ya afya, lakini siasa za uziwi na upofu zinaweza kuhujumu haya yote kama katiba isipohifadhi sheria na haki muhimu za kulinda kanisa, mali zake na viongozi wake. Misikiti na Makanisa yakikaa nyuma, viongozi wa dini wasije anza kulalama baadaye kwamba katiba imewapendelea hawa, au kuwaonea hawa.
Makampuni na taasisi na katiba
Makampuni na taasisi kisheria ni sawa na mtu au raia. Makampuni na taasisi zikikaa nyuma na kutokushiriki kwenye mchakato wa katiba mpya yapo masuala mengi yanayoweza kuja kuzuka baadaye kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni yakaya kuwa ni kwa hasara kubwa kwa upande wao.
Katika suala hili lal katiba mpya sisi sote ni wadau na washiriki na hakuna anayestahili kubakia kuwa mtazamaji tu au juu ya wenzake kwa namna yoyote ile.
Muswada huu kama ilivyokuwa kwa miswaada mingine dhaifu, inayovuja na dhalimu kwa wananchi na vizazi vijavyo, imedhirisha mapungugu mengi mengine katika muundo, mifumo na taratibu zetu za uongozi na uendeshaji nchi. Baadhi ya kasoro hizi ni pamoja na hatari ya kuwa na wabunge wa kuteuliwa badala ya kuchaguliwa kwenye bunge la kiwakilishi; jinsi ambavyo serikali iliyoko madarakani inaweza ikapora mamlaka na madaraka ya wananchi na kufanya mapinduzi ya kikatiba bila kuwajibishwa ipasavyo; muungano unavyozidi kuonekana kukosa maana kwa Watanganyika na kuwa mzigo usiobebeka; na ule ukweli kuwa nchi bado imo kizani na haijajaliwa kuwa na kiongozi na wanasiasa wanaoweza kututoa kwenye shimo refu la giza ambalo tumejikuta tumo leo.
Sunday, November 13, 2011
Tahadhari: Mswaada wa katiba usisomwe kama vile unasomwa kwa mara ya pili, usomwe kwa mara ya kwanza.....
WAKATI tayari wabunge wanashinikizwa kuusoma mswaada wa katiba mpya kwa mara ya pili badala ya kusomwa mara ya kwanza, ninachukua fursa hii kuwaasa viongozi na wabunge wetu kwamba kitendo cha kuusoma mswaada huu kama unaosomwa mara ya pili haitakuwa tofauti na wao kuipindua katiba ya nchi na kosa hilo ni sawa sawa na mapinduzi ya kijeshi, tofauti ikiwa yale ya kijeshi watu wengi watakufa siku hiyo hiyo, wakati haya ya kikatiba Watanzania wote watakuwa wanauawa taratibu na kimya kimya.
Watanzania wana haki kwa kutumia wawakilishi wao wa kweli na halali kuhusiana na suala la katiba na sio wanafiki na vibarakala wa wale walioko madarakani, kuchukua hatua zote za kisheria ni kiharakati ili 'wanaoazimia kuipindua' katiba kinyume cha sheria wanachukuliwa hatua zinazostahili. Na sio tu serikali imeamua kuipindua katiba, bali inawaziba mdomo na masikio wananchi ili wasijue kinachofanyika kwa kuwatumia wale waliochaguliwa kulinda haki na maslahi ya watawala na sio ya watawaliwa!
Aidha, damu, dhiki na machungu yoyote yatakayosababishwa na kuusoma na kuupitisha mswadaa huu, laana yake iwaangukie viongozi wa Tanzania wa zamani na wa sasa.
Tunajua ugumu wa viongozi wa Afrika na hasa hawa wetu wa Tanzania kusalimu amri. Inatisha pale viongozi hao tena wanaposemekana ni wale wanaosalmi amri kwa Mwenyezi Mungu, lakini labda si hawa wa sasa...na kama wanalaghaiwa na wale wanaowashauri kwa sababu binafsi za washauri hao, basi huu ni wakati muafaka wa hususan rais, kusalimu amri na kuwarudishia Watanzania haki yao ya kikatiba ya kuwa ndio wenye mamlaka na madaraka ya juu kabisa kwenye suala kama hili na sio yeye rais. Anachoshauriwa kukifanya rais kwa hivi sasa ni sawa na 'kuwapindua Watanzania' kwa kuipindua katiba yao iliyopo hivi sasa ambayo ndiyo inayosema wao ndio wenye sauti ya mwisho juu ya katiba na sio rais.
Kwa kuzingatia hayo hapo juu, ni muhimu awali ya yote kuweka jambo moja muhimu kuliko yote sawa hapa. Je, ni rais au ni wananchi wenye haki ya kusimamia mchakato wa katiba mpya ? Je, rais si kiongozi wa seriikali taasisi ambayo ni mmoja wa wadau katika suala hili la katiba? Na rais huyo huyo sio mwenyekiti wa chama tawala ambacho ni mmoja wa wadau katika suala hili la katiba? Katika hali kama hii haki na uadilifu uko wapi? Ni katiba gani inayomruhusu rais kuwapora wananchi haki yao ya kuwa ndio walio na mamlaka na madaraka ya juu na ya mwisho kwenye masuala kama haya?
Kuna mambo kadhaa ambayo ninafikiri ni muhimu
kuwekwa wazi na ikiwezekana kutekelezwa hata kabla ya Tanzania kuwa na katiba mpya.
1. Mosi ni ufafanuzi wa nani ndiye mwenye sauti na maamuzi kuhusu mchakato wa katiba mpya kwa mujibu wa katiba tuliyonayo, yaani, ni nani kati ya wananchi kupitia chombo au vyombo vyao halali vya uwakilishi vilivyopo au kitakachoundwa au ni serikali na kiongozi wake. Utata unakuja pale tunapobaini kwamba serikali nayo pia ni mdau katika mchakato huu. Na kwamba si haki kwa chama au serikali kujipa mamlaka au madaraka ambayo hawastahili kuwa nayo, kwani huko ni sawa na kupora mamlaka ya wananchi na kufanya mapinduzi ya kikatiba bila kutumia silaha.
2. Haki ya Kuandamana na Maandamano. Tofauti na katiba ya sasa inavyoruhusu, utawala wa sasa, unadai kwamba watu hawana uhuru wa kuandamana na kufanya maandamano. Pamoja na kuwatia ulemavu wa maisha baadhi ya Watanzania wasio na kosa, usalama wa taifa na vyombo vya dola hususan FFU, vinatumika kuvuruga amani na kuharibu mali za Watanznia. Kazi ya usalama wa taifa na vyombo vya dola si kuzuia maandamano na mikutano bali kuweka taratibu za kuhakikisha wanaofanya mikutano na maandamano hayo wana ulinzi na usalama wa kutosha.
3. Haki ya kukutana na kufanya mikutano. Ilivyo hivi sasa kama hapo juu inaonekana Watanzania hawana haki ya kukutana na kufanya mikutano inayohusu maisha na maendeleo yao na mitaa na vijiji vyao ila pale wanaporuhusiwa na chama tawala kupitia serikali yake iliyoko madarakani.Kazi ya usalama wa taifa na vyombo vya dola si kuzuia maandamano na mikutano bali kuweka taratibu za kuhakikisha wanaofanya mikutano na maandamano hayo wana ulinzi na usalama wa kutosha.
4. Mikoa na haki za wakazi wa mkoa. Hali ilivyo sasa chama tawala na wale wanaoteuliwa kuwa viongozi wa mikoa wanachaguliwa sio kwa uwezo wao wa kimenejimneti na kuchangia maendeleo ya wakazi wa mkoa husika bali kwa sababu za kisiasa. Ni mfumo wa kikoloni ambao mkoloni mkuu anachagua wakoloni wa kumasaidia kuidhulumu na kuinyonya mkoa husika. Tz. kwa mfano mikoa ya Mwanza na Arusha hivi leo. Mikoa inastahili kutawaliwa na chama ambacho kina wabunge na madiwani wengi katika mkoa husika na sio vinginevyo. Aidha, kukidhi changamoto za kimaendeleo zilizopo wakati umefika kwa mkoa kuwa na Waziri wake mkuu na baraza lake la mawaziri wa mkoa husika ili kuimarisha uhuru, umoja, haki na kuharakisha maendeleo ya mkoa husika.
5. Endapo kiongozi anatoa AHADI na anashindwa kuzitekeleza nini kifanyike dhidi yake na wanaohusika kwa ujumla?
6. Nini liwe jukumu la serikali na wanasiasa kuhusu mustakabali wa vijana wasio na ajira, wamachinga na waendesha biashara ndogondogo.
7. Haki ya vyama kuungana. Mpaka sasa haieleweki kwanini kuna ugumu kwa vyama vya kisiasa kuungana ili kupunguza utitiri wa vyama nchini ambao hausaidii kuimarisha mfumo wa vyama vingi nchini bali kuudhoofisha zaidi na zaidi.
8. Haki ya Mgombea huru nchini. Mpaka sasa sheria imepindwa na katiba imepinduliwa kinyemela kwa kumnyima haki Mtanzania anayetaka kugombea uchaguzi bila kufungamana na chama chochote cha kisiasa.
9. Apartheid ya viongozi kutibiwa nchi za nje wakati walalahoi wanakufa kwa kukosa fedha za kuchangia katika zahanati na mahospitali sehemu mbalimbali nchini iendelee au ife kwa kuwa na hospitali bora zaidi nchini na madakta wasio na kazi kwenye nchi zenye matatizo ya kiuchumi hivi leo duniani.
10. Nini iwe nafasi ya upinzani katika uongozi wa nchi, mikoa, wilaya na majimbo? Na je tutarahisishaje vyama mbadala kuchangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika sehemu mbalimbali nchini.
11. Vyama viendeshwe vipi ili vipate mapato halali na sio kutegemea hazina ya serikali au kupata fedha kupitia njia ambazo zitahatarisha uhuru na utu wetu.
12. Vipi vinastahili kuwa vyombo vya habari vya wananchi na vipi vya serikali na chama tawala. Mkurugenzi achaguliwe vipi na nani? Uhuru wa vyombo hivyo utahakikishwaje?
13. Nini iwe kazi za majeshi yetu wakati wa amani? Yatashirikishwaje katika uzalishaji mali, huduma za jamii, biashara, uchimbaji madini ili kuhakikisha rasilimali za Watanzania hazipewi sawa na bure kwa wageni eti tu kwa sababu hatuna utaalamu na mitambo ya kufanya shughuli fulani?
14. Nini yawe majukumu ya usalama wa taifa ili uwe na tija zaidi katika maendeleo ya kiuchumi na kiteknolojia ya Watanzania kuliko ilivyo sasa. Na je ni sahihi usalama wa taifa kuchunguza viongozi wa zamani au wa upinzani kikatiba na kisheria?
15. Je, mamlaka ya Rais kuteua watu kama wakuu wa polisi, wakuu wa mikoa, wakuu wa Wilaya, majaji, mahakimu, wabunge wasiochaguliwa ni jambo zuri na linaloimarisha demokrasia au ni baya na linalodhoofisha uhuru, haki za binaadamu na demokrasia. Nini kifanyike kumaliza utata huu?
16. Je, Soko huru linastahili kuingiliwa na viongozi wa serikali ili kutafuta umaarufu wa bei rahisi? Nini kifanyike kama tumeshakubali kuwa nchi ya kibepari na soko huru. Nchi ifuate mfumo gani wa kisiasa bora kuliko ubepari na ukomunisti kesho na keshokutwa? Nini kimilikiwe na wageni na watu binafsi au wanajamii husika au serikali au ubia wa aina hii au ule?
17. Je, tunahitaji kikomo cha safari za nje ambazo kiongozi aliyeko madarakani anaweza kuzifanya katika kipindi chake cha miaka 5?
18. Je, ni magari ya aina gani na gharama gani wanastahili kuwa nayo viongozi wa serikali na wabunge na watumishi wa umma?
19. Ni vipi maji ya mito, maziwa, bahari, ardhini na mvua yanaweza kupatikana na kuhakikisha upatikanji wa maji safi kwa Watanzania sehemu zote za nchi na wakati wote?
20. Je, ni wanasiasa au watu wenye utaalamu fulani, k.m. walimu, wahadhiri na madaktari ndio wanaostahili kulipwa vizuri zaidi? Na kwanini mwanasiasa asilipwe kutokana na tarafu au kazi aliyoisomea na cheo anachostahili kuwa nacho wakati huu?
KIMSINGI, hayo hapo juu ni machache tu katika kero, vilio, matamanio, ndoto na matarajio ya Watanzania na hususan vijana ambao ndio wazazi na wenye nchi wa kesho kuhusu jinsi ambavyo wangelipenga kuona suala hili la katiba likishughulikiwa kama inavyostahili na sio kwa kutumia ujanja, maguvu, mabavu, uzaini, uzandiki, ubabe na uhuni huku wanaofanya hivi wakijua fika kwamba njia wanayotupeleka ni ya shari na siyo ya kheri!!!
Kama Rais, waziri mkuu, mawaziri, wabunge, jaji mkuu, mwanasheria mkuu na washauri wengine wa waheshimiwa wana nafasi ya kuonesha hekima na busara basi ni leo Jumatatu, tarehe 14, Novemba 2011 ni KUSALIMU AMRI NA KURUHUSU MSWAADA HUU USOMWE MARA YA KWANZA NA SIYO YA PILI!!!
Watanzania wana haki kwa kutumia wawakilishi wao wa kweli na halali kuhusiana na suala la katiba na sio wanafiki na vibarakala wa wale walioko madarakani, kuchukua hatua zote za kisheria ni kiharakati ili 'wanaoazimia kuipindua' katiba kinyume cha sheria wanachukuliwa hatua zinazostahili. Na sio tu serikali imeamua kuipindua katiba, bali inawaziba mdomo na masikio wananchi ili wasijue kinachofanyika kwa kuwatumia wale waliochaguliwa kulinda haki na maslahi ya watawala na sio ya watawaliwa!
Aidha, damu, dhiki na machungu yoyote yatakayosababishwa na kuusoma na kuupitisha mswadaa huu, laana yake iwaangukie viongozi wa Tanzania wa zamani na wa sasa.
Tunajua ugumu wa viongozi wa Afrika na hasa hawa wetu wa Tanzania kusalimu amri. Inatisha pale viongozi hao tena wanaposemekana ni wale wanaosalmi amri kwa Mwenyezi Mungu, lakini labda si hawa wa sasa...na kama wanalaghaiwa na wale wanaowashauri kwa sababu binafsi za washauri hao, basi huu ni wakati muafaka wa hususan rais, kusalimu amri na kuwarudishia Watanzania haki yao ya kikatiba ya kuwa ndio wenye mamlaka na madaraka ya juu kabisa kwenye suala kama hili na sio yeye rais. Anachoshauriwa kukifanya rais kwa hivi sasa ni sawa na 'kuwapindua Watanzania' kwa kuipindua katiba yao iliyopo hivi sasa ambayo ndiyo inayosema wao ndio wenye sauti ya mwisho juu ya katiba na sio rais.
Kwa kuzingatia hayo hapo juu, ni muhimu awali ya yote kuweka jambo moja muhimu kuliko yote sawa hapa. Je, ni rais au ni wananchi wenye haki ya kusimamia mchakato wa katiba mpya ? Je, rais si kiongozi wa seriikali taasisi ambayo ni mmoja wa wadau katika suala hili la katiba? Na rais huyo huyo sio mwenyekiti wa chama tawala ambacho ni mmoja wa wadau katika suala hili la katiba? Katika hali kama hii haki na uadilifu uko wapi? Ni katiba gani inayomruhusu rais kuwapora wananchi haki yao ya kuwa ndio walio na mamlaka na madaraka ya juu na ya mwisho kwenye masuala kama haya?
Kuna mambo kadhaa ambayo ninafikiri ni muhimu
kuwekwa wazi na ikiwezekana kutekelezwa hata kabla ya Tanzania kuwa na katiba mpya.
1. Mosi ni ufafanuzi wa nani ndiye mwenye sauti na maamuzi kuhusu mchakato wa katiba mpya kwa mujibu wa katiba tuliyonayo, yaani, ni nani kati ya wananchi kupitia chombo au vyombo vyao halali vya uwakilishi vilivyopo au kitakachoundwa au ni serikali na kiongozi wake. Utata unakuja pale tunapobaini kwamba serikali nayo pia ni mdau katika mchakato huu. Na kwamba si haki kwa chama au serikali kujipa mamlaka au madaraka ambayo hawastahili kuwa nayo, kwani huko ni sawa na kupora mamlaka ya wananchi na kufanya mapinduzi ya kikatiba bila kutumia silaha.
2. Haki ya Kuandamana na Maandamano. Tofauti na katiba ya sasa inavyoruhusu, utawala wa sasa, unadai kwamba watu hawana uhuru wa kuandamana na kufanya maandamano. Pamoja na kuwatia ulemavu wa maisha baadhi ya Watanzania wasio na kosa, usalama wa taifa na vyombo vya dola hususan FFU, vinatumika kuvuruga amani na kuharibu mali za Watanznia. Kazi ya usalama wa taifa na vyombo vya dola si kuzuia maandamano na mikutano bali kuweka taratibu za kuhakikisha wanaofanya mikutano na maandamano hayo wana ulinzi na usalama wa kutosha.
3. Haki ya kukutana na kufanya mikutano. Ilivyo hivi sasa kama hapo juu inaonekana Watanzania hawana haki ya kukutana na kufanya mikutano inayohusu maisha na maendeleo yao na mitaa na vijiji vyao ila pale wanaporuhusiwa na chama tawala kupitia serikali yake iliyoko madarakani.Kazi ya usalama wa taifa na vyombo vya dola si kuzuia maandamano na mikutano bali kuweka taratibu za kuhakikisha wanaofanya mikutano na maandamano hayo wana ulinzi na usalama wa kutosha.
4. Mikoa na haki za wakazi wa mkoa. Hali ilivyo sasa chama tawala na wale wanaoteuliwa kuwa viongozi wa mikoa wanachaguliwa sio kwa uwezo wao wa kimenejimneti na kuchangia maendeleo ya wakazi wa mkoa husika bali kwa sababu za kisiasa. Ni mfumo wa kikoloni ambao mkoloni mkuu anachagua wakoloni wa kumasaidia kuidhulumu na kuinyonya mkoa husika. Tz. kwa mfano mikoa ya Mwanza na Arusha hivi leo. Mikoa inastahili kutawaliwa na chama ambacho kina wabunge na madiwani wengi katika mkoa husika na sio vinginevyo. Aidha, kukidhi changamoto za kimaendeleo zilizopo wakati umefika kwa mkoa kuwa na Waziri wake mkuu na baraza lake la mawaziri wa mkoa husika ili kuimarisha uhuru, umoja, haki na kuharakisha maendeleo ya mkoa husika.
5. Endapo kiongozi anatoa AHADI na anashindwa kuzitekeleza nini kifanyike dhidi yake na wanaohusika kwa ujumla?
6. Nini liwe jukumu la serikali na wanasiasa kuhusu mustakabali wa vijana wasio na ajira, wamachinga na waendesha biashara ndogondogo.
7. Haki ya vyama kuungana. Mpaka sasa haieleweki kwanini kuna ugumu kwa vyama vya kisiasa kuungana ili kupunguza utitiri wa vyama nchini ambao hausaidii kuimarisha mfumo wa vyama vingi nchini bali kuudhoofisha zaidi na zaidi.
8. Haki ya Mgombea huru nchini. Mpaka sasa sheria imepindwa na katiba imepinduliwa kinyemela kwa kumnyima haki Mtanzania anayetaka kugombea uchaguzi bila kufungamana na chama chochote cha kisiasa.
9. Apartheid ya viongozi kutibiwa nchi za nje wakati walalahoi wanakufa kwa kukosa fedha za kuchangia katika zahanati na mahospitali sehemu mbalimbali nchini iendelee au ife kwa kuwa na hospitali bora zaidi nchini na madakta wasio na kazi kwenye nchi zenye matatizo ya kiuchumi hivi leo duniani.
10. Nini iwe nafasi ya upinzani katika uongozi wa nchi, mikoa, wilaya na majimbo? Na je tutarahisishaje vyama mbadala kuchangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika sehemu mbalimbali nchini.
11. Vyama viendeshwe vipi ili vipate mapato halali na sio kutegemea hazina ya serikali au kupata fedha kupitia njia ambazo zitahatarisha uhuru na utu wetu.
12. Vipi vinastahili kuwa vyombo vya habari vya wananchi na vipi vya serikali na chama tawala. Mkurugenzi achaguliwe vipi na nani? Uhuru wa vyombo hivyo utahakikishwaje?
13. Nini iwe kazi za majeshi yetu wakati wa amani? Yatashirikishwaje katika uzalishaji mali, huduma za jamii, biashara, uchimbaji madini ili kuhakikisha rasilimali za Watanzania hazipewi sawa na bure kwa wageni eti tu kwa sababu hatuna utaalamu na mitambo ya kufanya shughuli fulani?
14. Nini yawe majukumu ya usalama wa taifa ili uwe na tija zaidi katika maendeleo ya kiuchumi na kiteknolojia ya Watanzania kuliko ilivyo sasa. Na je ni sahihi usalama wa taifa kuchunguza viongozi wa zamani au wa upinzani kikatiba na kisheria?
15. Je, mamlaka ya Rais kuteua watu kama wakuu wa polisi, wakuu wa mikoa, wakuu wa Wilaya, majaji, mahakimu, wabunge wasiochaguliwa ni jambo zuri na linaloimarisha demokrasia au ni baya na linalodhoofisha uhuru, haki za binaadamu na demokrasia. Nini kifanyike kumaliza utata huu?
16. Je, Soko huru linastahili kuingiliwa na viongozi wa serikali ili kutafuta umaarufu wa bei rahisi? Nini kifanyike kama tumeshakubali kuwa nchi ya kibepari na soko huru. Nchi ifuate mfumo gani wa kisiasa bora kuliko ubepari na ukomunisti kesho na keshokutwa? Nini kimilikiwe na wageni na watu binafsi au wanajamii husika au serikali au ubia wa aina hii au ule?
17. Je, tunahitaji kikomo cha safari za nje ambazo kiongozi aliyeko madarakani anaweza kuzifanya katika kipindi chake cha miaka 5?
18. Je, ni magari ya aina gani na gharama gani wanastahili kuwa nayo viongozi wa serikali na wabunge na watumishi wa umma?
19. Ni vipi maji ya mito, maziwa, bahari, ardhini na mvua yanaweza kupatikana na kuhakikisha upatikanji wa maji safi kwa Watanzania sehemu zote za nchi na wakati wote?
20. Je, ni wanasiasa au watu wenye utaalamu fulani, k.m. walimu, wahadhiri na madaktari ndio wanaostahili kulipwa vizuri zaidi? Na kwanini mwanasiasa asilipwe kutokana na tarafu au kazi aliyoisomea na cheo anachostahili kuwa nacho wakati huu?
KIMSINGI, hayo hapo juu ni machache tu katika kero, vilio, matamanio, ndoto na matarajio ya Watanzania na hususan vijana ambao ndio wazazi na wenye nchi wa kesho kuhusu jinsi ambavyo wangelipenga kuona suala hili la katiba likishughulikiwa kama inavyostahili na sio kwa kutumia ujanja, maguvu, mabavu, uzaini, uzandiki, ubabe na uhuni huku wanaofanya hivi wakijua fika kwamba njia wanayotupeleka ni ya shari na siyo ya kheri!!!
Kama Rais, waziri mkuu, mawaziri, wabunge, jaji mkuu, mwanasheria mkuu na washauri wengine wa waheshimiwa wana nafasi ya kuonesha hekima na busara basi ni leo Jumatatu, tarehe 14, Novemba 2011 ni KUSALIMU AMRI NA KURUHUSU MSWAADA HUU USOMWE MARA YA KWANZA NA SIYO YA PILI!!!
Monday, May 2, 2011
Yamahitajika Mapinduzi ya Uongozi ngazi za chini
KUNA tabia iliyojengeka miongoni mwa Watanzania kwa baadhi yao kujiona bora na hivyo kuona kwamba nafasi au vyeo vya chini katika uongozi sio laiki yao. Kwa sababu wenzetu hao wanajiona wamesoma sana, matajiri sana au wana vyeo vikubwa sana basi wanawaachia watu wasiosoma, masikini na wanyonge nafasi za uongozi katika ngazi za chini kama vile usimamizi wa nyumba kumi, ukatibu kata, uenyekiti wa mitaa na udiwani. Wao wote wanakimbilia kuwa wabunge, wawakilishi na maraisi japo wanajua fika nafasi hizo ni chache mno na kwamba uongozi si lazima uwe mbunge au waziri au rais wa nchi. Chukulia mfano wa Zanzibar kuna wagombea wengi tu ambao wangelifaa kuwa wakuu wa mikoa na wakaleta mabadiliko ya kweli katika jamii lakini hawataki nafasi hiyo ila wanataka tu urais. Kuna nini Ikulu na kwenye bunge ndugu zetu ? Kwanini vipaji hivyo msivitumie kwenye ngazi ya mkoa na wilaya ? Au mwadhani nafasi zimejaa ? Matokeo yake ni kwamba taifa zima katika ngazi za chini halina viongozi ambao wanajua menejimenti, uongozi (leadership), utawala (governance) achilia mambo kama uchumi, sosholojia, saikolojia, usimamizi wa bajeti na fedha, kompyuta na teknohama, teknolojia nyingine za miaka hii na mlolongo wa mengi mengineyo yanayohitajika katika dunia ya siku hizi ili kuleta mabadiliko ya kina na kimsingi katika jamii inayoongozwa.
Funzo ambalo ningelipenda lijulikane asubuhi na mapema na dhamira kuu ya insha hii ni kwamba bila kuwa na viongozi walioelimika, walioridhikia kimaisha na wanaojua kutofautisha kati ya kutumiwa na viongozi na kuongoza wenyewe nchi hii haitaondokana na umasikini wa kutupwa kwa miaka mingi ijayo.
Kwa maneno mengine, mapinduzi ya kweli ya kiungozi yatakuja tu pale tutakapokuwa na viongozi wa ngazi za chini wanaojua uongozi, uchumi, nadharia tofauti za njia, mbinu, mikakati ya maendeleo na elimu zinazoendana na masuala kama hayo. Hawa watakuwa ni viongozi wanaoweza kuunda baraza la mawaziri la mkoa na ambao wanaweza wakahoji maamuzi yanayofanywa na bunge la taifa na baraza la mawaziri la taifa kwa kuwa wana elimu sawa na walioko juu, ingawa wao zaidi ni katika lugha mama ya taifa, Kiswahili.
Isitoshe uongozi wa namna hii ukipatikana katika ngazi ya chini kabisa itakuwa ni rahisi kutathmini viongozi na kuwapa dhamana kubwa zaidi kulingana na mafanikio yao katika ngazi za chini.
Chini ya Uongozi wa kijamaa Watanzania wengi waliokuwa na elimu, vyeo na mali walikataa katakata kugombea nafasi za ujumbe wa nyumba kumi,udiwani na uongozi wa mitaa. Ikawa ni kawaida kwa nafasi hizo kuchukuliwa na watu wasiokuwa na elimu au wenye elimu ndogo sana; wasiowahi kushika cheo chochote na waliokuwa wanaongoza kwa umasikini na hali ngumu ya maisha katika mitaa yao.
Hali hiyo ukienda leo kwenye mikoa mbalimbali na hasa huko vijijini bado ipo na inaendelea. Swali la kujiuliza ni kwamba ikiwa familia, mitaa na vijiji ndio msingi au matofali ya msingi ya taifa leltu hivi kweli tunaweza kujenga taifa lililo imara kisiasa na madhubuti kiuchumi, kijamii, kitekonoojia na kijeshi endapo uongozi wake unashikwa na watu sampuli hii ?
Ieleweke kwamba siwadharau hata kidogo wale walioshika dhamana hii pale ambapo matajiri, wasomi na watu wengine wenye majina walipoidharau na kuikataa. Ila kutokana na mabadiliko ya wakati ambapo sasa Tanzania ni sehemu tu kiuchumi katika ulimwengu mkubwa zaidi naona upo umuhimu wa kujitazama na kujipanga upya ili tuweze kuzikabili changamoto mbalimbali za maendeleo zinazotukabili.
Pengine kuna kosa la kiufundi lililofanyika katika ugawaji dhamana na maslahi yanayoendana na hili. HIvi anayestahili kulipwa mshahara mzuri ni kiongozi wa ngazi ya chini kabisa (ambaye anaweza kuibadili hali ya watu wake toka umaskini au daraja la tatu wakawa la pili au la kwanza) au kiongozi wa ngazi ya juu ambaye nadra kuwa na mawasiliano na wananchi huko waliko?
Ukweli ni kuwa viongozi wetu wa nyumba kumi, wenyeviti wa mitaa na makatibu kata wote elimu yao, uzoefu wao, uono wao na ufahamu wao wa dunia ya utandawazi bado uko chini kwa upande mmoja. Na kwa upande wa pili maslahi na motisha yao ya kuleta mabadiliko ya kimsingi katika jamii zao ni sawa na hamna au ni kidunchu mno. Hii haina tofauti na mameneja, makocha na viongozi wengine wa timu ya michezo kulipwa mara kumi au ishirini ya wachezaji halafu timu ikawa inadorora mwaka nenda, mwaka rudi -halafu unatafuta mchawi nje yenu !
Viongozi au watu wanaoitwa viongozi katika ngazi za chini kwenye nchi hii ni watu wasiolipwa mishahara; hawana elimu ya kutosha kuongoza na kuleta mabadiliko katika jamii; hawana ari, motisha wala moyo wa kufanya kazi; hawana ujuzi na uzoefu katika kazi wanazozifanya na wala hakuna taasisi iliyojipanga au kupangwa kuwafunza na kuwaendeleza.
Viongozi hao wa chini wengi ni masikini kiasi cha kutisha kiasi ambacho sio tu wana vishawishi vingi bali pia wanakuwa sio amana bali deni kwa taifa na hasa pale wageni toka nje ya eneo lao au nje ya nchi wanapokuja na kitita cha fedha na kuwashawishi zaidi. Au wanapotishwa na viongozi wa ngazi ya kitaifa hadi kuwadhulumu na kuwaonea watu wao wenyewe.
Hata tupate viongozi wa kitaifa ambao wote ni maprofesa lakini huku chini tuna watu wasiosoma, masikini na wenye ujuzi sawa na hamna katika masula ya uchumi, biashara, uwekezaji, ujasiriamli, menejimenti, usimamizi wa fedha, sheria na kadhalika nchi yetu haiwezi kamwe kuendelea.
Tutajenga kama mataifa mengine yaliyopotea kizazi cha viongozi wanaorithiwa na watoto wao mwaka nenda, mwaka rudi. Ni mwanzo wa kuwa na nchi ambayo itakubali na itaendelea kukubali uongozi mbovu kwa sababu mfumo uliopo hauna chachu wala changamoto inayoiwezesha kupata fikra mbadala na viongozi wenye misimamo na mitazamo mipya na inayobadilika na wakati.
Kazi zao nyingi hazina usaidizi wa aina yoyote ile ukiwa ule wa zana, fedha au rasilimali watu. Na kwa hiyo, kwa wakati mwingi ni sehemu ndogo ya yale yaliyostahili kuwa majukumu yao yanatekelezwa kikamilifu.
Wrengi wanajiona wanatumika zaidi kisiasa na baadhi yao wanaamini pengine kile walichostahili kulipwa huliwa na wale walio juu yao. Zaidi ya hilo mara chache sana maamuzi yana sauti katika masuala mbalimbali. Kwa hiyo huiona zaidi ni yoyo kuliko watu wenye sauti katika mambo mengi yanayowazunguka. Nafuu kwao huja wakati wa chaguzi kwani ndipo wanapoweza kupambanisha pande mbalimbali na kuzikamua angalau wapate maziwa ya watoto.
Huu ni wakati mzuri wa kujiuliza, hivi, kama viongozi wa ngazi za chini wangekuwa na elimu, maarifa na uono sawa na wale wa juu majimbo yetu ya uchaguzi yangelikuwa kama hivi yalivyo. Na, je ni mtaji kwa serikali kwa wananchi vijijini kuwa mbumbumbu wa faida za siasa za ushindani ? Na wabunge tunaowapata kwa mfumo huu wa sasa wangelikuwa ndio hao hao katika mazingira ambayo kuna wasomi kushinda wao katika ngazi za uongozi wa chini ?
Ni rahisi kuelewa kwa nini hakuna anayetaka kugombea nafasi za kuwa mjumbe wa nyumba kumi au balozi au diwani au mwenyekiti wa serikali ya mtaa. Kwa upande mwingine kila mtu anataka kugombea ubunge, uwakilishi na urais. Hata hao waliopo asilimia 80 ya muda wao hutumika kujitafutia riziki kwingineko na ni kama asilimia 20 tu ndiyo hutumika kuangalia mambo ya wananchi/serikali.
Kutokana na ukweli huu kwamba kuna mfumo na hali ambayo inasababisha watu watake kugombea ubunge, uwakilishi na urais lakini hakuna wanaotaka kugombea ubalozi wa mitaa au uenyekiti wa mtaa ni dhahiri kuwa ipo haja ya kuleta mapinduzi makubwa ya uongozi katika ngazi za chini ikiwa kama kweli tunataka tujikwamue na hali hii ya kuwa masikini wakubwa duniani. Na uongozi wowote (uwe wa chini au wa juu) lazima uwe ni kazi au tarafu inayolipwa kima mahsusi kinachowawezesha viongozi hao wote kujitoa kwa hali na mali kutimiza zaidi majukumu yao ya kikazi kuliko ya kibinafsi.
Tuanze na utafiti na ushauri
Ninapendekeza kuwa Chuo Kikuu cha Mzumbe kikishirikiana na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania chenye tawi karika kila mkoa waanze kwa utafiti na ushauri katika kila mkoa kuona ni namna gani tunavyoweza kuongeza hatua kwa hatua, ubora wa viongozi waliopo na wakati huo huo kuwashawishi watu wenye uwezo, elimu na ujuzi zaidi kukubali kuwa wajumbe wa nyumba kumi na viongozi wa serikali za mitaa. Bila kuwasahau madiwani wetu. Baada ya kazi za utafiti na ushauri yaanze mafunzo na uandaaji wa mipango ya urithishaji uongozi kwa namna ambayo kila mtaa, kila kata inapata kiongozi anayestahili kushika nafasi hiyo.
Ninaamini ya kwamba, masomo kama vile yale ya uchumi, uongozi( leadership) utawala (governance) , uangalizi wa fedha, menejimenti, sayansi ya jamii, usimamizi rasilimali watu, mipango, udhibiti, sayansi ya maamuzi na kadhalika hayatakosekana na yatatolewa kwa lugha mama ya Watanzania, yaani, Kiswahili.
Sio rahisi bila ya nafasi za uongozi katika ngazi za chini kushikwa na watu wenye ujuzi, elimu na uono mpana wa dunia hii ya utandawazi kwa watu wetu kuamka na kufanya kile kinachotakikana kama majibu yetu kwa mfumo wa uchumi, biashara na teknolojia unaogeuka kila kuchwao.
Mapinduzi ya uongozi Tanzania yataanza pale itakapogundulika kuwa nafasi hizo si za wanasesere au vibarakala(puppets) bali za watu muhimu mno katika kuikwamua Tanzania kutoka kwenye umaskini na wanaostahili kupewa ila nyenzo ili waweze kuhamasisha watu na jambo hilo likafanyika bila kusubiri ziara na misaada ya wakubwa toka makao makuu ya nchi yawayo.
Funzo ambalo ningelipenda lijulikane asubuhi na mapema na dhamira kuu ya insha hii ni kwamba bila kuwa na viongozi walioelimika, walioridhikia kimaisha na wanaojua kutofautisha kati ya kutumiwa na viongozi na kuongoza wenyewe nchi hii haitaondokana na umasikini wa kutupwa kwa miaka mingi ijayo.
Kwa maneno mengine, mapinduzi ya kweli ya kiungozi yatakuja tu pale tutakapokuwa na viongozi wa ngazi za chini wanaojua uongozi, uchumi, nadharia tofauti za njia, mbinu, mikakati ya maendeleo na elimu zinazoendana na masuala kama hayo. Hawa watakuwa ni viongozi wanaoweza kuunda baraza la mawaziri la mkoa na ambao wanaweza wakahoji maamuzi yanayofanywa na bunge la taifa na baraza la mawaziri la taifa kwa kuwa wana elimu sawa na walioko juu, ingawa wao zaidi ni katika lugha mama ya taifa, Kiswahili.
Isitoshe uongozi wa namna hii ukipatikana katika ngazi ya chini kabisa itakuwa ni rahisi kutathmini viongozi na kuwapa dhamana kubwa zaidi kulingana na mafanikio yao katika ngazi za chini.
Chini ya Uongozi wa kijamaa Watanzania wengi waliokuwa na elimu, vyeo na mali walikataa katakata kugombea nafasi za ujumbe wa nyumba kumi,udiwani na uongozi wa mitaa. Ikawa ni kawaida kwa nafasi hizo kuchukuliwa na watu wasiokuwa na elimu au wenye elimu ndogo sana; wasiowahi kushika cheo chochote na waliokuwa wanaongoza kwa umasikini na hali ngumu ya maisha katika mitaa yao.
Hali hiyo ukienda leo kwenye mikoa mbalimbali na hasa huko vijijini bado ipo na inaendelea. Swali la kujiuliza ni kwamba ikiwa familia, mitaa na vijiji ndio msingi au matofali ya msingi ya taifa leltu hivi kweli tunaweza kujenga taifa lililo imara kisiasa na madhubuti kiuchumi, kijamii, kitekonoojia na kijeshi endapo uongozi wake unashikwa na watu sampuli hii ?
Ieleweke kwamba siwadharau hata kidogo wale walioshika dhamana hii pale ambapo matajiri, wasomi na watu wengine wenye majina walipoidharau na kuikataa. Ila kutokana na mabadiliko ya wakati ambapo sasa Tanzania ni sehemu tu kiuchumi katika ulimwengu mkubwa zaidi naona upo umuhimu wa kujitazama na kujipanga upya ili tuweze kuzikabili changamoto mbalimbali za maendeleo zinazotukabili.
Pengine kuna kosa la kiufundi lililofanyika katika ugawaji dhamana na maslahi yanayoendana na hili. HIvi anayestahili kulipwa mshahara mzuri ni kiongozi wa ngazi ya chini kabisa (ambaye anaweza kuibadili hali ya watu wake toka umaskini au daraja la tatu wakawa la pili au la kwanza) au kiongozi wa ngazi ya juu ambaye nadra kuwa na mawasiliano na wananchi huko waliko?
Ukweli ni kuwa viongozi wetu wa nyumba kumi, wenyeviti wa mitaa na makatibu kata wote elimu yao, uzoefu wao, uono wao na ufahamu wao wa dunia ya utandawazi bado uko chini kwa upande mmoja. Na kwa upande wa pili maslahi na motisha yao ya kuleta mabadiliko ya kimsingi katika jamii zao ni sawa na hamna au ni kidunchu mno. Hii haina tofauti na mameneja, makocha na viongozi wengine wa timu ya michezo kulipwa mara kumi au ishirini ya wachezaji halafu timu ikawa inadorora mwaka nenda, mwaka rudi -halafu unatafuta mchawi nje yenu !
Viongozi au watu wanaoitwa viongozi katika ngazi za chini kwenye nchi hii ni watu wasiolipwa mishahara; hawana elimu ya kutosha kuongoza na kuleta mabadiliko katika jamii; hawana ari, motisha wala moyo wa kufanya kazi; hawana ujuzi na uzoefu katika kazi wanazozifanya na wala hakuna taasisi iliyojipanga au kupangwa kuwafunza na kuwaendeleza.
Viongozi hao wa chini wengi ni masikini kiasi cha kutisha kiasi ambacho sio tu wana vishawishi vingi bali pia wanakuwa sio amana bali deni kwa taifa na hasa pale wageni toka nje ya eneo lao au nje ya nchi wanapokuja na kitita cha fedha na kuwashawishi zaidi. Au wanapotishwa na viongozi wa ngazi ya kitaifa hadi kuwadhulumu na kuwaonea watu wao wenyewe.
Hata tupate viongozi wa kitaifa ambao wote ni maprofesa lakini huku chini tuna watu wasiosoma, masikini na wenye ujuzi sawa na hamna katika masula ya uchumi, biashara, uwekezaji, ujasiriamli, menejimenti, usimamizi wa fedha, sheria na kadhalika nchi yetu haiwezi kamwe kuendelea.
Tutajenga kama mataifa mengine yaliyopotea kizazi cha viongozi wanaorithiwa na watoto wao mwaka nenda, mwaka rudi. Ni mwanzo wa kuwa na nchi ambayo itakubali na itaendelea kukubali uongozi mbovu kwa sababu mfumo uliopo hauna chachu wala changamoto inayoiwezesha kupata fikra mbadala na viongozi wenye misimamo na mitazamo mipya na inayobadilika na wakati.
Kazi zao nyingi hazina usaidizi wa aina yoyote ile ukiwa ule wa zana, fedha au rasilimali watu. Na kwa hiyo, kwa wakati mwingi ni sehemu ndogo ya yale yaliyostahili kuwa majukumu yao yanatekelezwa kikamilifu.
Wrengi wanajiona wanatumika zaidi kisiasa na baadhi yao wanaamini pengine kile walichostahili kulipwa huliwa na wale walio juu yao. Zaidi ya hilo mara chache sana maamuzi yana sauti katika masuala mbalimbali. Kwa hiyo huiona zaidi ni yoyo kuliko watu wenye sauti katika mambo mengi yanayowazunguka. Nafuu kwao huja wakati wa chaguzi kwani ndipo wanapoweza kupambanisha pande mbalimbali na kuzikamua angalau wapate maziwa ya watoto.
Huu ni wakati mzuri wa kujiuliza, hivi, kama viongozi wa ngazi za chini wangekuwa na elimu, maarifa na uono sawa na wale wa juu majimbo yetu ya uchaguzi yangelikuwa kama hivi yalivyo. Na, je ni mtaji kwa serikali kwa wananchi vijijini kuwa mbumbumbu wa faida za siasa za ushindani ? Na wabunge tunaowapata kwa mfumo huu wa sasa wangelikuwa ndio hao hao katika mazingira ambayo kuna wasomi kushinda wao katika ngazi za uongozi wa chini ?
Ni rahisi kuelewa kwa nini hakuna anayetaka kugombea nafasi za kuwa mjumbe wa nyumba kumi au balozi au diwani au mwenyekiti wa serikali ya mtaa. Kwa upande mwingine kila mtu anataka kugombea ubunge, uwakilishi na urais. Hata hao waliopo asilimia 80 ya muda wao hutumika kujitafutia riziki kwingineko na ni kama asilimia 20 tu ndiyo hutumika kuangalia mambo ya wananchi/serikali.
Kutokana na ukweli huu kwamba kuna mfumo na hali ambayo inasababisha watu watake kugombea ubunge, uwakilishi na urais lakini hakuna wanaotaka kugombea ubalozi wa mitaa au uenyekiti wa mtaa ni dhahiri kuwa ipo haja ya kuleta mapinduzi makubwa ya uongozi katika ngazi za chini ikiwa kama kweli tunataka tujikwamue na hali hii ya kuwa masikini wakubwa duniani. Na uongozi wowote (uwe wa chini au wa juu) lazima uwe ni kazi au tarafu inayolipwa kima mahsusi kinachowawezesha viongozi hao wote kujitoa kwa hali na mali kutimiza zaidi majukumu yao ya kikazi kuliko ya kibinafsi.
Tuanze na utafiti na ushauri
Ninapendekeza kuwa Chuo Kikuu cha Mzumbe kikishirikiana na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania chenye tawi karika kila mkoa waanze kwa utafiti na ushauri katika kila mkoa kuona ni namna gani tunavyoweza kuongeza hatua kwa hatua, ubora wa viongozi waliopo na wakati huo huo kuwashawishi watu wenye uwezo, elimu na ujuzi zaidi kukubali kuwa wajumbe wa nyumba kumi na viongozi wa serikali za mitaa. Bila kuwasahau madiwani wetu. Baada ya kazi za utafiti na ushauri yaanze mafunzo na uandaaji wa mipango ya urithishaji uongozi kwa namna ambayo kila mtaa, kila kata inapata kiongozi anayestahili kushika nafasi hiyo.
Ninaamini ya kwamba, masomo kama vile yale ya uchumi, uongozi( leadership) utawala (governance) , uangalizi wa fedha, menejimenti, sayansi ya jamii, usimamizi rasilimali watu, mipango, udhibiti, sayansi ya maamuzi na kadhalika hayatakosekana na yatatolewa kwa lugha mama ya Watanzania, yaani, Kiswahili.
Sio rahisi bila ya nafasi za uongozi katika ngazi za chini kushikwa na watu wenye ujuzi, elimu na uono mpana wa dunia hii ya utandawazi kwa watu wetu kuamka na kufanya kile kinachotakikana kama majibu yetu kwa mfumo wa uchumi, biashara na teknolojia unaogeuka kila kuchwao.
Mapinduzi ya uongozi Tanzania yataanza pale itakapogundulika kuwa nafasi hizo si za wanasesere au vibarakala(puppets) bali za watu muhimu mno katika kuikwamua Tanzania kutoka kwenye umaskini na wanaostahili kupewa ila nyenzo ili waweze kuhamasisha watu na jambo hilo likafanyika bila kusubiri ziara na misaada ya wakubwa toka makao makuu ya nchi yawayo.
Saturday, April 30, 2011
Mishahara, Maendeleo na Rasilimali Watu
Ibara ya 23 katika kifungu (1) inabainisha kwamba: "Kila mtu, bila ya kuwapo ubaguzi wa aina yoyote,
anayo haki ya kupata ujira unaolingana na kazi yake, na watu
wote wanaofanya kazi kulingana na uwezo wao watapata malipo
kulingana na kiasi na sifa za kazi wanayoifanya."
Kifungu hiki kinahitaji kupanuliwa ili kutoacha sintofahamu katika masuala muhimu ya ajira, ujira na maslahi ya wafanyakazi.
a) Malipo ya haki ni yepi, yanapimwa vipi, yanarekebishwa vipi na kiwango kinabadilikaje kutokana na mabadiliko katika uchumi na jamii?
b) Kwanini watu wenye ngozi nyeupe, toka nje wanalipwa vizuri kuliko ngozi nyeusi na wazawa kiujumla? Ubaguzi wa aina yoyote hautakiwa kukubalika isipokuwa kama ni ubaguzi wa kumpendelea mzawa.
b) Ni lazima mishahara ioanishwe na kapu la mahitaji ya msingi ya mtu, na kiwango hiki cha chini cha mahitaji ya msingi ndio kiamue ujira wa chini na sio kiwango hiko kuwekwa jinsi wakubwa watakavyo.
c) Mishahara na mapenzi ya rais visiunganishwa. Isiendelee kuonekana kama watu wanapata mishahara kutokana na huruma ya kiongozi huyo.
d) Machelewesho yote ya mfanyakazi au mtumishi wa umma yalipwe riba kwa muda wote utakaocheleweshwa.
e) Makato kwenda NSSF,PPF, LAPF na kwingineko kama huko yawe na kiasi fulani cha ununuzi wa hisa wa mashirika husika. Kinachofanyika hivi sasa ni kuwa wakatwa michango ndio wamiliki wanaostahili, lakini wanaofaidi faida za umilikaji ni serikali na wengineo na sio mwananchi anayestahili kuwa mmilikaji wa mashirika hayo.
f) Mtu yeyote mwenye elimu na ujuzi unaostahili kumfanya aajiriwe lakini hana ajira awe analipwa kiwango na mahitaji ya msingi kwake na familia yake.
g) TUMEWABEBA sana viongozi kwa kuwalipa MISHAHARA MIKUBWA kuliko kazi wanayoifanya katika kuondoa umaskini, ujinga, maradhi na nchi yetu kubaki nyuma kimaendeleo. Kama mwalimu alivyofanya mwaka 1966/7 viongozi wetu walikubali hili; wajione ni wanyonyaji; na mishahara yao iwe nusu kama sio robo ya hii ya leo na iwe inaongezeka kutokana na michango yao katika kuondoa ujinga, umaskini, maradhi katika maeneo yao husika.
h) Wabunge walipwe mishahara inayoendana na elimu, ujuzi na kazi zao za mwisho walizoajiriwa kabla ya kuingia bungeni. Kwa utaratibu huu tutawaondoa wale wote wanaotaka kutajirika kupitia ubunge na siasa.
Wafanyabiashara wote wanaojiingiza katika siasa watatakiwa kujilipa wenyewe bila kugusa senti toka hazina.
i) Ili kujivunia rasilimali watu zetu wenyewe kama Imarati inavyofanya hata pakiwa na bosi toka nje, Mtanzania aliyeko chini yake na anayejifunza kutoka kwake alipwe vizuri kuliko huyo mgeni.
j) Madaktari, manesi, walimu, wahadhiri, wanajeshi na polisi ambao kazi zao haziwaruhusu kufanya (kwa haki) zaidi ya lile waliloajiriwa kama tunataka lifanyike vizuri walipwe mishahara mizuri tu inayowafanya wasitamani kufanya kitu kingine
k) Tofauti kati ya viongozi wa juu na viongozi wa chini na wananchi wengine katika mafao yao baada ya kustaafu yatazamwe na yasipishane kwa kiasi kikubwa na cha kutisha.
l) Wakuu wa mikoa na wilaya kama hawatachaguliwa na wakazi wa mikoa na wilaya husika walipwe na chama tawala.
m) Mishahara miwili iwe marufuku, badala yake mtu apate alawansi inayostahili.
n) Pawe na utaratibu ambao utahakikisha mishahara na mafao ya wafanyakazi ( k.m. EAC) hailiwi na wajanja wachache.
o) Uongezaji mishahara kwa viongozi uendane na jinsi serikali na watumishi wake wanavyochangia kukuza pato la taifa. Likipungua mishahara hiyo ishuke. Likikua mishahara hiyo ipande.
anayo haki ya kupata ujira unaolingana na kazi yake, na watu
wote wanaofanya kazi kulingana na uwezo wao watapata malipo
kulingana na kiasi na sifa za kazi wanayoifanya."
Kifungu hiki kinahitaji kupanuliwa ili kutoacha sintofahamu katika masuala muhimu ya ajira, ujira na maslahi ya wafanyakazi.
a) Malipo ya haki ni yepi, yanapimwa vipi, yanarekebishwa vipi na kiwango kinabadilikaje kutokana na mabadiliko katika uchumi na jamii?
b) Kwanini watu wenye ngozi nyeupe, toka nje wanalipwa vizuri kuliko ngozi nyeusi na wazawa kiujumla? Ubaguzi wa aina yoyote hautakiwa kukubalika isipokuwa kama ni ubaguzi wa kumpendelea mzawa.
b) Ni lazima mishahara ioanishwe na kapu la mahitaji ya msingi ya mtu, na kiwango hiki cha chini cha mahitaji ya msingi ndio kiamue ujira wa chini na sio kiwango hiko kuwekwa jinsi wakubwa watakavyo.
c) Mishahara na mapenzi ya rais visiunganishwa. Isiendelee kuonekana kama watu wanapata mishahara kutokana na huruma ya kiongozi huyo.
d) Machelewesho yote ya mfanyakazi au mtumishi wa umma yalipwe riba kwa muda wote utakaocheleweshwa.
e) Makato kwenda NSSF,PPF, LAPF na kwingineko kama huko yawe na kiasi fulani cha ununuzi wa hisa wa mashirika husika. Kinachofanyika hivi sasa ni kuwa wakatwa michango ndio wamiliki wanaostahili, lakini wanaofaidi faida za umilikaji ni serikali na wengineo na sio mwananchi anayestahili kuwa mmilikaji wa mashirika hayo.
f) Mtu yeyote mwenye elimu na ujuzi unaostahili kumfanya aajiriwe lakini hana ajira awe analipwa kiwango na mahitaji ya msingi kwake na familia yake.
g) TUMEWABEBA sana viongozi kwa kuwalipa MISHAHARA MIKUBWA kuliko kazi wanayoifanya katika kuondoa umaskini, ujinga, maradhi na nchi yetu kubaki nyuma kimaendeleo. Kama mwalimu alivyofanya mwaka 1966/7 viongozi wetu walikubali hili; wajione ni wanyonyaji; na mishahara yao iwe nusu kama sio robo ya hii ya leo na iwe inaongezeka kutokana na michango yao katika kuondoa ujinga, umaskini, maradhi katika maeneo yao husika.
h) Wabunge walipwe mishahara inayoendana na elimu, ujuzi na kazi zao za mwisho walizoajiriwa kabla ya kuingia bungeni. Kwa utaratibu huu tutawaondoa wale wote wanaotaka kutajirika kupitia ubunge na siasa.
Wafanyabiashara wote wanaojiingiza katika siasa watatakiwa kujilipa wenyewe bila kugusa senti toka hazina.
i) Ili kujivunia rasilimali watu zetu wenyewe kama Imarati inavyofanya hata pakiwa na bosi toka nje, Mtanzania aliyeko chini yake na anayejifunza kutoka kwake alipwe vizuri kuliko huyo mgeni.
j) Madaktari, manesi, walimu, wahadhiri, wanajeshi na polisi ambao kazi zao haziwaruhusu kufanya (kwa haki) zaidi ya lile waliloajiriwa kama tunataka lifanyike vizuri walipwe mishahara mizuri tu inayowafanya wasitamani kufanya kitu kingine
k) Tofauti kati ya viongozi wa juu na viongozi wa chini na wananchi wengine katika mafao yao baada ya kustaafu yatazamwe na yasipishane kwa kiasi kikubwa na cha kutisha.
l) Wakuu wa mikoa na wilaya kama hawatachaguliwa na wakazi wa mikoa na wilaya husika walipwe na chama tawala.
m) Mishahara miwili iwe marufuku, badala yake mtu apate alawansi inayostahili.
n) Pawe na utaratibu ambao utahakikisha mishahara na mafao ya wafanyakazi ( k.m. EAC) hailiwi na wajanja wachache.
o) Uongezaji mishahara kwa viongozi uendane na jinsi serikali na watumishi wake wanavyochangia kukuza pato la taifa. Likipungua mishahara hiyo ishuke. Likikua mishahara hiyo ipande.
Katiba, Dini na Madhehebu
Hadidu za rejea muhimu kwa kipengele hiki kijengwe zaidi kwa ufafanuzi wa ibara ya 19 juu ya Uhuru wa mtu kuamini dini atakayo.
i. Nini uwe uhusiano kati ya serikali na dini au madhehebu ?
ii. Nini uwe uhusiano wa wa vyama vya siasa na dini au madhehebu mbalimbali ?
iii. Fidia kwa vyama na na mashirika ya kidini yaliyovunjwa na serikali zilizopita.
iv. Haki ya kila muumini na kila madhehebu kujiunga na kikundi kikubwa au kidogo ili kuendeleza maslahi ya waumini na madhehebu husika na kukataa katakata kikundi chochote kuwa na ukiritimba juu ya waumini wa dini fulani kama ilivyo BAKWATA kwa waislamu.
v. Haki katika kuzipa dini na madehehebu ruzuku.
vi. Uhuru wa kuabudu kwa kuwa na taasisi mbalimbali zinazoendeleza na kulinda imani ya mtu, kwa mfano, Waislamu na Mahakama ya Kadhi.
vii. Taratibu za ugharamiaji taasisi za kidini kutokana na kodi wanayolipwa wanannchi juu ya michango binafasi ya waumini husika.
viii. Haki ya kidemokrasia katika uwakilishi wa taasisi za kidini kutokna na idadi na majukumu ya kila dini, madehehebu na wafuasi wake. Isiwe dini yenye watu wachache ndiyo inayowakilishwa na wawakilishi wengi kuliko ile yenye wafuasi wengi.
ix. Ujenzi wa mahusiano bora na ya amani kati ya dini na dini na madehehebu zao na udhibiti ndani ya dini na miongoni mwa dini kwa wale watakaotaka kutumia dini kuivuruga nchi.
x. Kuoanisha masuala ya kiuchumi na kijamii na maendeleo ya watu ili pasiwe na dini ambayo wafuasi wake wengi ndio matajiri na dini nyingine ambayo waumini wake wengi ndio masikini.
i. Nini uwe uhusiano kati ya serikali na dini au madhehebu ?
ii. Nini uwe uhusiano wa wa vyama vya siasa na dini au madhehebu mbalimbali ?
iii. Fidia kwa vyama na na mashirika ya kidini yaliyovunjwa na serikali zilizopita.
iv. Haki ya kila muumini na kila madhehebu kujiunga na kikundi kikubwa au kidogo ili kuendeleza maslahi ya waumini na madhehebu husika na kukataa katakata kikundi chochote kuwa na ukiritimba juu ya waumini wa dini fulani kama ilivyo BAKWATA kwa waislamu.
v. Haki katika kuzipa dini na madehehebu ruzuku.
vi. Uhuru wa kuabudu kwa kuwa na taasisi mbalimbali zinazoendeleza na kulinda imani ya mtu, kwa mfano, Waislamu na Mahakama ya Kadhi.
vii. Taratibu za ugharamiaji taasisi za kidini kutokana na kodi wanayolipwa wanannchi juu ya michango binafasi ya waumini husika.
viii. Haki ya kidemokrasia katika uwakilishi wa taasisi za kidini kutokna na idadi na majukumu ya kila dini, madehehebu na wafuasi wake. Isiwe dini yenye watu wachache ndiyo inayowakilishwa na wawakilishi wengi kuliko ile yenye wafuasi wengi.
ix. Ujenzi wa mahusiano bora na ya amani kati ya dini na dini na madehehebu zao na udhibiti ndani ya dini na miongoni mwa dini kwa wale watakaotaka kutumia dini kuivuruga nchi.
x. Kuoanisha masuala ya kiuchumi na kijamii na maendeleo ya watu ili pasiwe na dini ambayo wafuasi wake wengi ndio matajiri na dini nyingine ambayo waumini wake wengi ndio masikini.
Hoja, Mantiki na sababu za Mkutano wa Katiba Mpya
Katiba mpya ni mkataba sawa na mkataba mwingine wowote. Na kwa sababu hii hapawezi pakawa na pande yoyote katika mkataba inayoweza kuwa muuzaji na mnunuzi kwa wakati huo huo; wakili wa kiapo na shahidi kwa wakati huohuo na mlipaji na mlipwaji kwa wakati huo huo.
Kwa maneno mengine ukiitazama ibara ya 8.-(1) inadhihiisha yafuatayo: " Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi inayofuata
misingi ya demokrasia na haki ya kijamii, na kwa hiyo -
(a) wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na Serikali
itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa
wananchi kwa mujibu wa Katiba hii;
(b) lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi;
(c) Serikali itawajibika kwa wananchi;
(d) wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali yao
kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.
Ningeliomba tutilie mkazo kwenye vifungu vyenye maneno haya: wananchi ndio msingi wa mamlaka yote; wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali yao;
Demokrasia na haki ya kijamii;
na lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi.
Kwa uelewa wangu wananchi kuwa msingi wa mamlaka yote ina maana kwamba mabwana na wamiliki wa katiba ni wananchi wenyewe na sio stahili ya mtu yeyote kwa nafasi aliyo nayo kuchukua jukumu hili na kuamua kama vile yeye ndiye wananchi. Haifai. Na sio haki wala halali. Ieleweke na kifungu hiki (wananchi ndio msingi wa mamlaka yote) kama katiba ilivyo sheria mama basi ni kifungu mama cha katiba na hakuna kifungu chochote katika katiba kinaweza kuwa juu yake au kukibatilisha au kukivunja.
Kifungu kinachozungumzia kwamba wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali yao ina maana kuna siku au kipindi kitafika na rais, serikali yake, mawaziri, majaji na wabunge watapaswa kukaa pembeni na kuwaachia wananchi wafanye maamuzi yanayowahusu wananchi kama yanavyowahusu viongozi wao. Na kazi kubwa ya serikali inakuwa ni kuwawezesha wananchi kupitia chombo muafaka kitakachowakilisha mawazo, ndoto, kero, kutoridhika, maudhi, dhamira, matamanio na maslahi yao kwa mapana na marefu kuifanya kazi iliyoko mbele ya taifa. Ieleweke kuwa ushiriki huu wa wananchi katika serikali yao hufanyika mara chache katika maisha ya taifa husika.
Lakini ni ushiriki muhimu mno kiasi kwamba huaminika kwamba muda kama huu ndio unaobainisha kati ya viongozi bora na viongozi duni na wapowapo tu, katika historia ya nchi husika.
Ninachukulia pia kwamba kifungu kinachozungumzia Demokrasia na haki ya kijamii kina maana katika wakati kama huo haki inakuwa ni kile kitendo cha kiongozi wa nchi aliyepo kukubali kwamba wanaostahili kufanya maamuzi husika ni wananchi na siyo yeye na neno demokrasia linaimanisha kwamba walio wengi ndio watakaoamua. Au pale inapolazimika wasio na ubinafsi na wanaoona mbali zaidi ya wananchi wengine ndio waamue.
Ninachukulia pia kwamba katika mchakato kama huu uliopo mbele yetu maneno: " lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi," yaana maana kwamba katika kipindi kama hiki serikali inastahili kuwa inatafakari jinsi gani lengo hili la ustawi litaoanishwa na katiba mpya kwa namna ambayo vyote, yaani, serikali na katiba wakati utakapofika vitaonekana kufanya kazi kwa ufanifu na ufanisi uliokusudiwa.
Na hasa ukizingatia pamoja na kwamba tulipata uhuru sawa na Malaysia, Botswana, Singapore, Indonesia, nchi mbalimbali za Kiarabu hivi leo, miaka 50 baada ya uhuru, hatuzioni hata indiketa za magari yao ya kimaendeleo ziko wapi.
Ukifika wakati kama huu kiongozi wa nchi anapaswa awe juu ya siasa, vyama na serikali yenyewe na akajiwezesha na kuwezeshwa kuyaweka mbele maslahi ya nchi na watu wake na kutambua kwamba kazi iliyoko mbele yake ni kazi itakayomjengea jina, heshima na shukrani zisizokwishamilele kama baba wa demokrasia na utaifa katika nchi husika. Ni nafasi kama hii tu inayozaa viongozi ambao maamuzi yao yanaitoa nchi na fikra za wananchi wake kutoka kwenye kizazi ambacho mambo yake yamepitwa na wakati kuingia kwenye kujali na kuzingatia maslahi na manufaa ya walio wengi kwa kizazi kilichopo na vile vitakavyokuja baada ya hapa. Huu ni wakati wa pekee unaotoa rais ambaye maamuzi yake yanakuwa ni makubwa kuliko maslahi binafsi ba maslahi ya chama chake. Huu ni wakati unaotoa rais ambaye kweli ni rais wa wote na sio wale tu wa chama chake na waliompigia kura. Huu ni wakati wa kuiunganisha nchi ambayo tayari ilikuwa ikitishiwa na kusambaratika kutokana na sababu mbalimbali.
Uamuzi katika hatua kama hii ndio unaoamua kama vyama vya siasa vitakuwa ni chombo imara na bora na vinavyotegemewa na wananchi au la; umaskini utapunguzwa au utaongezeka; ufisadi utakwisha au utakuwa kama funza na kujichimbia chini kwa chini; rasilmali watu bora itaongezeka na wote kupatiwa kazi au tatizo la wajuzi na ajira litaendelea kuiandama nchi na vijana wake na maji yanayotuzunguka yatatiririshwa na kutufikia majumbani au yataendelea kuishia maporini na kunyonywa na jua.
Uamuzi huo pia unaoamua tutakuwa na bunge la watu waliobalehe kimwili, kitabia, kimaamuzi na kifikra, kama tutakuwa na dini zinazoheshimiana au zisizoheshimiana; amani na umoja au kinyume cha hivyo; kila Mtanzania kuwa na nyumba kama hitaji la msingi au nyumba kuwa kwa wale waliochaguliwa au kupendelewa tu; umeme utakuwepo katika kila nyumba au ni asilimia 5 ya Watanzania watakaokuwa na umeme.
Baada ya kuizungumzia ibara ya 8 hebu tuangalie yaliyomo katika ibara ya 9 na kujiuliza kama kweli kuna chombo chochote zaidi ya baraza au mkutano wa katiba mpya unaoweza kukidhi malengo ambayo yamo katika katiba iliyopo hivi sasa kwa mapana na marefu yake na kisiwe kinarashiarashia tu na kushindwa kutimiza maazimio hayo na matarajio ya Watanzania wa leo na kesho:
Katika ibara hii kwa maoni yangu ninaamini ndio kuna kiini maridhawa cha uandikaji wa katiba mpya. Kwanza, ipo fursa ya kukubali au kukataa kama nchi hii ni ya kijamaa au la. Na kwa sababu wote tulihusishwa katika suala la ujamaa na kujitegemea tutawatendea haki wananchi wetu pale tutakapowapa fursa ya wao wenyewe kujadili kwa mapana na marefu juu ya kukubali au kuukataa ujamaa. Na kisha wafanye maamuzi juu ya mfumo mpya wa kisiasa wanaoamini utawaharakishia maendeleo yao na utakaoweza kuwafaa kwa miaka 50-100 ijayo.
Baada ya hapo unafuata msururu wa mambo ambayo Watanzania inasemekena kwa niaba ya chama tawala/chama kimoja waliamua kuwa ndiyo mkataba wa malengo na majukumu wanayostahili kubeba watawala ili watawaliwa waridhike na waone wanatendewa ipasavyo:
NInaiorodhesha hapa chini na pembeni yake kukiwa na swali la msingi, yaani, je bila kuwa na baraza au mkutano wa katiba mpya tutaweza kweli kutenda haki kwa Watanzania wa leo na vizazi vyao vijavyo ?
Kifungu (a) kinasema kwamba ni kazi ya watawala kuhakikisha: " kwamba utu na haki nyinginezo zote za binadamu
zinaheshimiwa na kuthaminiwa," je tathmini ya hili linaweza kweli kufanyika na kundi la watu wachache tu katika jamii ambao hawaijui hata 1/100 ya nchi au ni baraza au mkutano wa katiba ambao pengine una wabunge wote; wawakilishi kutoka kila wilaya nchini; wawakilishi wanaowakilisha maslahi ya kila kundi nchini wakiwemo wafanyakazi, wakulima, wafugaji, wavuvi, wawindaji, wanafunzi, vijana, wazee, wanawake na kadhalika?
Kifungu (b) kinataka serikali kuhakikisha : "kwamba sheria za nchi zinalindwa na kutekelezwa," ni nani anayeweza mchakato wa kuonesha hili linafanyika au halifanyiki ipasavyo na ni kwa sababu gani na nini kifanyike ili lifanyike ipasavyo?
Kifungu kingine muhimu ni kile cha (c) ambacho kinaiamuru serikali kuhakikisha : " kwamba shughuli za Serikali zinatekelezwa kwa njia
ambazo zitahakikisha kwamba utajiri wa Taifa
unaendelezwa, unahifadhiwa na unatumiwa kwa
manufaa ya wananchi wote kwa jumla na pia kuzuia
mtu kumyonya mtu mwingine," na baada ya mali za umma kubinfasishwa na wananchi wasirudishiwe kodi/michango yao, CCM kuchukua mali zilizojengwa na jasho na fedha yawananchi, migodi kukodishwa kwa mrabaha sawa na hamna kitu na mikakati ya kupunguza umaskini kukwama, je tunastahili kuwa na chombo cha namna gani kuandika katiba kama sio baraza au mkutano wa katiba mpya?
Nchi iliyobarikiwa kuwa na Azimio la Arusha na maamuzi ya busara kama vile kuziweka njia zote kuu za uchumi chini ya umma ni kichekesho leo kugawa migodi ya madini ovyo kama njugu kwa watu wasio na mapenzi na uchungu na watu wetu na maendeleo yao. Nchi ambayo inajua unyama na unyonyaji wa mabenki inasikitisha kuona kwamba imebinafsisha mabenki ambayo lengo lake ni kuwakaanga Watanzania katika mafuta yao wenyewe. Nchi ambayo inajua faida za ujamaa na kujitegemea inaaibisha kuiona leo inakaribisha wawekezaji kama wale wa simu za mkononi ambao lengo lao ni kupanda na kuvuna papo kwa hapo huku wakifaidika vilivyo na misamaha ya kodi.
Hoja yetu inabakia pale pale kwa vifungu vilivyobakia vifuatavyo: " (d) kwamba maendeleo ya uchumi wa Taifa yanakuzwa na kupangwa kwa ulinganifu na kwa pamoja;
(e) kwamba kila mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi anafanya kazi, na kazi maana yake ni shughuli yoyote ya halali inayompatia mtu riziki yake; (f) kwamba heshima ya binadamu inahifadhiwa na
kudumishwa kwa kufuata Kanuni za Tangazo la
Dunia kuhusu Haki za Binadamu; (g) kwamba Serikali na vyombo vyake vyote vya umma vinatoa nafasi zilizo sawa kwa raia wote, wake kwa
waume, bila ya kujali rangi, kabila, dini au hali ya
mtu; (h) kwamba aina zote za dhuluma, vitisho, ubaguzi,
rushwa, uonevu au upendeleo zinaondolewa nchini; (i) kwamba matumizi ya utajiri wa Taifa yanatilia mkazo maendeleo ya wananchi na hasa zaidi yanaelekezwa kwenye jitihada ya kuondosha
umaskini, ujinga na maradhi;
(j) kwamba shughuli za uchumi haziendeshwi kwa njia zinazoweza kusababisha ulimbikizaji wa mali au njia
kuu za uchumi katika mamlaka ya watu wachache binafsi; na
(k) kwamba nchi inatawaliwa kwa kufuata misingi ya
demokrasia."
Kwa kuwa wananchi ndio msingi wa mamlaka yote wana haki ya kurejesha mamlaka yao kwa muda na wakawapangia watumishi wao majukumu upya. Uundwaji wa katiba mpya unahitaji marejesho haya ya mamlaka kwa muda kwa wananchi. Ni kitendo cha heshima, utii, uaminifu na kiungwana kwa wapiga kura kufanya hivyo katika wakati kama huu.
Ni muhimu kwa wanasiasa na vyama siasa kuwa na imani na wananchi wakati huu. Na ni chama na wanasiasa watakaokuwa na imani na wananchi, na wananchi wakawa na imani nao ndio watakaokuwa cha ushindi kwa wananchi wote.
Ushauri bora wa hivi karibuni ni ule uliotolewa wakati wa pasaka ukisema ya kwamba:' kuandika katiba mpya si sawa na kuandika ilani ya chama fulani cha kisiasa.'
Aidha, vyama vya upinzani havina haki ya kutaka kuandika katiba kwa madhumuni ya kukiondoa chama tawala madarakani, kama ilivyo kwa chama tawala kutotamani kuandika katiba ili kuvizuia vyama mbadala kuja kuingia madarakani wakati ufikapo.
Tujiulize kwa hiyo je, ni baraza ama mkutano wa katiba mpya ambacho kitakuwa chombo kinachoundwa na wananchi wenyewe kupitia wawakilishi wao au Tume ya hiki au kile itakayoundwa kwa kupora mamlaka na madaraka ya wananchi ndicho kitakachoweza kuyashughulikia masuala haya kwa ukamilifu na haki zaidi? Budi fikra za viongozi wetu ziwe kubwa kuliko za kiserikali, kiungozi, kisiasa, kivyama na kibinafsi katika kufanya uamuzi sahihi na muafaka kuhusu kazi iliyoko mbele yetu.
Kwa maneno mengine ukiitazama ibara ya 8.-(1) inadhihiisha yafuatayo: " Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi inayofuata
misingi ya demokrasia na haki ya kijamii, na kwa hiyo -
(a) wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na Serikali
itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa
wananchi kwa mujibu wa Katiba hii;
(b) lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi;
(c) Serikali itawajibika kwa wananchi;
(d) wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali yao
kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.
Ningeliomba tutilie mkazo kwenye vifungu vyenye maneno haya: wananchi ndio msingi wa mamlaka yote; wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali yao;
Demokrasia na haki ya kijamii;
na lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi.
Kwa uelewa wangu wananchi kuwa msingi wa mamlaka yote ina maana kwamba mabwana na wamiliki wa katiba ni wananchi wenyewe na sio stahili ya mtu yeyote kwa nafasi aliyo nayo kuchukua jukumu hili na kuamua kama vile yeye ndiye wananchi. Haifai. Na sio haki wala halali. Ieleweke na kifungu hiki (wananchi ndio msingi wa mamlaka yote) kama katiba ilivyo sheria mama basi ni kifungu mama cha katiba na hakuna kifungu chochote katika katiba kinaweza kuwa juu yake au kukibatilisha au kukivunja.
Kifungu kinachozungumzia kwamba wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali yao ina maana kuna siku au kipindi kitafika na rais, serikali yake, mawaziri, majaji na wabunge watapaswa kukaa pembeni na kuwaachia wananchi wafanye maamuzi yanayowahusu wananchi kama yanavyowahusu viongozi wao. Na kazi kubwa ya serikali inakuwa ni kuwawezesha wananchi kupitia chombo muafaka kitakachowakilisha mawazo, ndoto, kero, kutoridhika, maudhi, dhamira, matamanio na maslahi yao kwa mapana na marefu kuifanya kazi iliyoko mbele ya taifa. Ieleweke kuwa ushiriki huu wa wananchi katika serikali yao hufanyika mara chache katika maisha ya taifa husika.
Lakini ni ushiriki muhimu mno kiasi kwamba huaminika kwamba muda kama huu ndio unaobainisha kati ya viongozi bora na viongozi duni na wapowapo tu, katika historia ya nchi husika.
Ninachukulia pia kwamba kifungu kinachozungumzia Demokrasia na haki ya kijamii kina maana katika wakati kama huo haki inakuwa ni kile kitendo cha kiongozi wa nchi aliyepo kukubali kwamba wanaostahili kufanya maamuzi husika ni wananchi na siyo yeye na neno demokrasia linaimanisha kwamba walio wengi ndio watakaoamua. Au pale inapolazimika wasio na ubinafsi na wanaoona mbali zaidi ya wananchi wengine ndio waamue.
Ninachukulia pia kwamba katika mchakato kama huu uliopo mbele yetu maneno: " lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi," yaana maana kwamba katika kipindi kama hiki serikali inastahili kuwa inatafakari jinsi gani lengo hili la ustawi litaoanishwa na katiba mpya kwa namna ambayo vyote, yaani, serikali na katiba wakati utakapofika vitaonekana kufanya kazi kwa ufanifu na ufanisi uliokusudiwa.
Na hasa ukizingatia pamoja na kwamba tulipata uhuru sawa na Malaysia, Botswana, Singapore, Indonesia, nchi mbalimbali za Kiarabu hivi leo, miaka 50 baada ya uhuru, hatuzioni hata indiketa za magari yao ya kimaendeleo ziko wapi.
Ukifika wakati kama huu kiongozi wa nchi anapaswa awe juu ya siasa, vyama na serikali yenyewe na akajiwezesha na kuwezeshwa kuyaweka mbele maslahi ya nchi na watu wake na kutambua kwamba kazi iliyoko mbele yake ni kazi itakayomjengea jina, heshima na shukrani zisizokwishamilele kama baba wa demokrasia na utaifa katika nchi husika. Ni nafasi kama hii tu inayozaa viongozi ambao maamuzi yao yanaitoa nchi na fikra za wananchi wake kutoka kwenye kizazi ambacho mambo yake yamepitwa na wakati kuingia kwenye kujali na kuzingatia maslahi na manufaa ya walio wengi kwa kizazi kilichopo na vile vitakavyokuja baada ya hapa. Huu ni wakati wa pekee unaotoa rais ambaye maamuzi yake yanakuwa ni makubwa kuliko maslahi binafsi ba maslahi ya chama chake. Huu ni wakati unaotoa rais ambaye kweli ni rais wa wote na sio wale tu wa chama chake na waliompigia kura. Huu ni wakati wa kuiunganisha nchi ambayo tayari ilikuwa ikitishiwa na kusambaratika kutokana na sababu mbalimbali.
Uamuzi katika hatua kama hii ndio unaoamua kama vyama vya siasa vitakuwa ni chombo imara na bora na vinavyotegemewa na wananchi au la; umaskini utapunguzwa au utaongezeka; ufisadi utakwisha au utakuwa kama funza na kujichimbia chini kwa chini; rasilmali watu bora itaongezeka na wote kupatiwa kazi au tatizo la wajuzi na ajira litaendelea kuiandama nchi na vijana wake na maji yanayotuzunguka yatatiririshwa na kutufikia majumbani au yataendelea kuishia maporini na kunyonywa na jua.
Uamuzi huo pia unaoamua tutakuwa na bunge la watu waliobalehe kimwili, kitabia, kimaamuzi na kifikra, kama tutakuwa na dini zinazoheshimiana au zisizoheshimiana; amani na umoja au kinyume cha hivyo; kila Mtanzania kuwa na nyumba kama hitaji la msingi au nyumba kuwa kwa wale waliochaguliwa au kupendelewa tu; umeme utakuwepo katika kila nyumba au ni asilimia 5 ya Watanzania watakaokuwa na umeme.
Baada ya kuizungumzia ibara ya 8 hebu tuangalie yaliyomo katika ibara ya 9 na kujiuliza kama kweli kuna chombo chochote zaidi ya baraza au mkutano wa katiba mpya unaoweza kukidhi malengo ambayo yamo katika katiba iliyopo hivi sasa kwa mapana na marefu yake na kisiwe kinarashiarashia tu na kushindwa kutimiza maazimio hayo na matarajio ya Watanzania wa leo na kesho:
Katika ibara hii kwa maoni yangu ninaamini ndio kuna kiini maridhawa cha uandikaji wa katiba mpya. Kwanza, ipo fursa ya kukubali au kukataa kama nchi hii ni ya kijamaa au la. Na kwa sababu wote tulihusishwa katika suala la ujamaa na kujitegemea tutawatendea haki wananchi wetu pale tutakapowapa fursa ya wao wenyewe kujadili kwa mapana na marefu juu ya kukubali au kuukataa ujamaa. Na kisha wafanye maamuzi juu ya mfumo mpya wa kisiasa wanaoamini utawaharakishia maendeleo yao na utakaoweza kuwafaa kwa miaka 50-100 ijayo.
Baada ya hapo unafuata msururu wa mambo ambayo Watanzania inasemekena kwa niaba ya chama tawala/chama kimoja waliamua kuwa ndiyo mkataba wa malengo na majukumu wanayostahili kubeba watawala ili watawaliwa waridhike na waone wanatendewa ipasavyo:
NInaiorodhesha hapa chini na pembeni yake kukiwa na swali la msingi, yaani, je bila kuwa na baraza au mkutano wa katiba mpya tutaweza kweli kutenda haki kwa Watanzania wa leo na vizazi vyao vijavyo ?
Kifungu (a) kinasema kwamba ni kazi ya watawala kuhakikisha: " kwamba utu na haki nyinginezo zote za binadamu
zinaheshimiwa na kuthaminiwa," je tathmini ya hili linaweza kweli kufanyika na kundi la watu wachache tu katika jamii ambao hawaijui hata 1/100 ya nchi au ni baraza au mkutano wa katiba ambao pengine una wabunge wote; wawakilishi kutoka kila wilaya nchini; wawakilishi wanaowakilisha maslahi ya kila kundi nchini wakiwemo wafanyakazi, wakulima, wafugaji, wavuvi, wawindaji, wanafunzi, vijana, wazee, wanawake na kadhalika?
Kifungu (b) kinataka serikali kuhakikisha : "kwamba sheria za nchi zinalindwa na kutekelezwa," ni nani anayeweza mchakato wa kuonesha hili linafanyika au halifanyiki ipasavyo na ni kwa sababu gani na nini kifanyike ili lifanyike ipasavyo?
Kifungu kingine muhimu ni kile cha (c) ambacho kinaiamuru serikali kuhakikisha : " kwamba shughuli za Serikali zinatekelezwa kwa njia
ambazo zitahakikisha kwamba utajiri wa Taifa
unaendelezwa, unahifadhiwa na unatumiwa kwa
manufaa ya wananchi wote kwa jumla na pia kuzuia
mtu kumyonya mtu mwingine," na baada ya mali za umma kubinfasishwa na wananchi wasirudishiwe kodi/michango yao, CCM kuchukua mali zilizojengwa na jasho na fedha yawananchi, migodi kukodishwa kwa mrabaha sawa na hamna kitu na mikakati ya kupunguza umaskini kukwama, je tunastahili kuwa na chombo cha namna gani kuandika katiba kama sio baraza au mkutano wa katiba mpya?
Nchi iliyobarikiwa kuwa na Azimio la Arusha na maamuzi ya busara kama vile kuziweka njia zote kuu za uchumi chini ya umma ni kichekesho leo kugawa migodi ya madini ovyo kama njugu kwa watu wasio na mapenzi na uchungu na watu wetu na maendeleo yao. Nchi ambayo inajua unyama na unyonyaji wa mabenki inasikitisha kuona kwamba imebinafsisha mabenki ambayo lengo lake ni kuwakaanga Watanzania katika mafuta yao wenyewe. Nchi ambayo inajua faida za ujamaa na kujitegemea inaaibisha kuiona leo inakaribisha wawekezaji kama wale wa simu za mkononi ambao lengo lao ni kupanda na kuvuna papo kwa hapo huku wakifaidika vilivyo na misamaha ya kodi.
Hoja yetu inabakia pale pale kwa vifungu vilivyobakia vifuatavyo: " (d) kwamba maendeleo ya uchumi wa Taifa yanakuzwa na kupangwa kwa ulinganifu na kwa pamoja;
(e) kwamba kila mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi anafanya kazi, na kazi maana yake ni shughuli yoyote ya halali inayompatia mtu riziki yake; (f) kwamba heshima ya binadamu inahifadhiwa na
kudumishwa kwa kufuata Kanuni za Tangazo la
Dunia kuhusu Haki za Binadamu; (g) kwamba Serikali na vyombo vyake vyote vya umma vinatoa nafasi zilizo sawa kwa raia wote, wake kwa
waume, bila ya kujali rangi, kabila, dini au hali ya
mtu; (h) kwamba aina zote za dhuluma, vitisho, ubaguzi,
rushwa, uonevu au upendeleo zinaondolewa nchini; (i) kwamba matumizi ya utajiri wa Taifa yanatilia mkazo maendeleo ya wananchi na hasa zaidi yanaelekezwa kwenye jitihada ya kuondosha
umaskini, ujinga na maradhi;
(j) kwamba shughuli za uchumi haziendeshwi kwa njia zinazoweza kusababisha ulimbikizaji wa mali au njia
kuu za uchumi katika mamlaka ya watu wachache binafsi; na
(k) kwamba nchi inatawaliwa kwa kufuata misingi ya
demokrasia."
Kwa kuwa wananchi ndio msingi wa mamlaka yote wana haki ya kurejesha mamlaka yao kwa muda na wakawapangia watumishi wao majukumu upya. Uundwaji wa katiba mpya unahitaji marejesho haya ya mamlaka kwa muda kwa wananchi. Ni kitendo cha heshima, utii, uaminifu na kiungwana kwa wapiga kura kufanya hivyo katika wakati kama huu.
Ni muhimu kwa wanasiasa na vyama siasa kuwa na imani na wananchi wakati huu. Na ni chama na wanasiasa watakaokuwa na imani na wananchi, na wananchi wakawa na imani nao ndio watakaokuwa cha ushindi kwa wananchi wote.
Ushauri bora wa hivi karibuni ni ule uliotolewa wakati wa pasaka ukisema ya kwamba:' kuandika katiba mpya si sawa na kuandika ilani ya chama fulani cha kisiasa.'
Aidha, vyama vya upinzani havina haki ya kutaka kuandika katiba kwa madhumuni ya kukiondoa chama tawala madarakani, kama ilivyo kwa chama tawala kutotamani kuandika katiba ili kuvizuia vyama mbadala kuja kuingia madarakani wakati ufikapo.
Tujiulize kwa hiyo je, ni baraza ama mkutano wa katiba mpya ambacho kitakuwa chombo kinachoundwa na wananchi wenyewe kupitia wawakilishi wao au Tume ya hiki au kile itakayoundwa kwa kupora mamlaka na madaraka ya wananchi ndicho kitakachoweza kuyashughulikia masuala haya kwa ukamilifu na haki zaidi? Budi fikra za viongozi wetu ziwe kubwa kuliko za kiserikali, kiungozi, kisiasa, kivyama na kibinafsi katika kufanya uamuzi sahihi na muafaka kuhusu kazi iliyoko mbele yetu.
Wednesday, March 30, 2011
Maudhui na misingi ya Katiba Mpya:
Kijumla katiba lazima iwe ya watu na itakayowatumikia watu na matakwa yao na sio kuwa silaha ya kuwakandamiza, kuwanyanyasa na kuwapora utawala wa nchi yao
wazawa na watu wa nchi hii kwa ujumla.
Huu ni uwanja mpana na maoni yangu kijuujuu ni kwamba:
i. Katiba Ihakikishe ina vifungu toshelevu kuhusu haki za mtu (individual) ili jiji na miji yetu isiwe inatumia askari kuwafukuza machinga, mama ntilie na watu
wengine wanaotafuta riziki zao bila kueleweka watu hao wana haki gani. Yaani, mtu akifanya kosa ijulikane ni kosa moja kwa moja toka ndani ya katiba na sheria za
nchi. Na mtu akipewa upendeleo katiba ifichue kuna upendeleo waziwazi. Tusivumilie katu tabia ya kujengwa Vijiwe vya kina CCM mitaani na pale wakaruhusiwa
kuvunja sheria eti kwa kuwa wanaishabikia na 'kuitetea' CCM !
ii. Katiba lazima iwe very specific kwenye hali inayojitokeza nchini ambayo baadhi ya polisi na mahakimu wanaonekana kupiga bei au kuuza na kununua haki
za watu!
iii. Mamlaka ya rais yapunguzwe kwa kiasi kikubwa na ikiwezekana asilindwe pale atakapoonekana na viongozi wenzake kuwa kavunja sheria na katiba ya nchi.
iv. Jaji Mkuu atokane na majaji kadhaa watakaopendekezwa bungeni na kisha kuchaguliwa na bunge.
v. Kamanda mkuu wa polisi atokane na majaji kadhaa watakaopendekezwa bungeni na kisha kuchaguliwa na bunge.
vi. Mwanasheria Mkuu atokane na majaji kadhaa watakaopendekezwa bungeni na kisha kuchaguliwa na bunge.
vii. Katiba ifafanue maana ya Uchochezi na Uhaini katika mazingira ya mfumo wa vyama vingi na kila kitu kiwe bayana na kueleweka vyema na kukubalika na
wote. Tusikubali Watanzania fulani kuwaita wenzao wahaini na wachochezi kwa sababu Watanzania wenzao wamegundua wao ni wezi na mafisadi.
viii. Benki Kuu na Hazina lazima ishurutishwe na Katiba kutenga asilimia fulani katika kusaidia masikini na kuendeleza wazawa.
ix. Wakuu wa mikoa wasiteuliwe na rais bali wachaguliwe na wakazi wa mikoa husika ili kuwawajibisha ipasavyo katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
x. Mikoa iwe na Gavana au Waziri wake mkuu na baraza lake la mawaziri na wa wawakilishi wa mikoani watakaounda bunge la mkoa wakitokea kwenye watu wa
kuchaguliwa na wale wa kuwakilisha maslahi ya makundi mbalimbali katika jamii. Hili litaifanya mikoa kushindana katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi na hivyo
kuendelea kwa haraka zaidi kuliko ilivyo hivi sasa.
xi. Ruksa kwa vyama vya kisiasa kuungana kama ilivyo rahisi kwa watu wa kawaida kufunga ndoa wakati wowote wanapotaka.
xii. Kutoruhusu udikteta katika kundi au chama chochote cha kisiasa au kijamii na kadhalika.
xiii. Mkuu wa TUC (Tanzania University Commision) kupewa kazi na bunge na wakuu wa vyuo vikuu vyote kutathminiwa na kuchaguliwa na TUC!
xiv. Katika migodi na madini katiba itaje wazi utaratibu wa kumiliki, kukodi, kuchimba, kutengeneza vitu vinavyotokana na madini na kuviuza vitu hivyo kwa
manufaa ya wananchi. Lazima pia mipango iwepo ya kuiwezesha nchi hii kwanza kununua na kutengeneza mitambo muhimu kwa sekta husika ili wananchi wafaidi zaidi
mali asili yao. Taratibu hizo ni pamoja na kutaja mrabaha unaokubalika; mtawanyo wa umiliki kwa nchi za Mashariki na Marekani ya Kusini zaidi kuliko zile zilizozoeleka
za Magharibi.
Xv. Katika Umeme lazima katiba ieleze waziwazi aina ya umeme salama na bora kwa nchi na watu wasiwe wanaropoka ropoka tu kuhusu vitu kama umeme wa
nyuklia kwa nchi ambayo imeshindwa kusimamia vyema vitu vya kawaida; ikaja tokea viongozi wetu wanashawishika kuzalisha umeme huo hatari kwa maafa ya vizazi
vijanvyo.
xvi. Kuhusu maji ni lazima katiba iwe chimbuko la sheria ambazo zitakuwa kali na zisizo na huruma kuhusu kutunza vyanzo vya maji na vile vile kuhamasisha
ubunifu na matumizi mazuri ya maji toka kwenye maziwa yanayotuzunguka; bahari, mitoni, ardhini na yale yanayoletwa na mvua.
xvii. Kuhusu Utalii ni lazima katiba ioneshe waziwazi jinsi ambavyo wanavijiji na wanajamii mbalimbali bara na pwani watakavyonufaika na utalii badalal ya utalii
kunufaisha matajiri wachache wa nje na ndani. Ni lazima serikali iainishe mipango na mikakati ya wananchi pwani na bara kutumia ardhi, bahari na vivutio walivyo navyo
kama mtaji wao na hivyo kuhesabika kithamani na kifedha na kukubaliwa na wawekezaji kama uwekezaji wa thamani, halali na unaokubalika katika uendeshaji utalii na
mambo kama hayo.
xviii. Kuhusu viwanda ni muhimu katiba ichambue ndani-nje aina ya viwanda vinavyohitajika na jinsi tunavyoweza kuongeza thamani ya mazao, bidhaa, madini na
mali asili nyingine zetu ili tunufaike zaidi kiuchumi kuliko kunufaisha watu wa nje. Ni lazima kujipanga pia kikatiba na kuona kuwa tunazalisha mashine-mama na
mitambo-mama yote tunayoweza ili uendelezaji sekta ya viwanda uwe rahisi. Katika miaka hii ambayo wahandisi na wataalamu mbalimbali Ulaya, Asia na kwingineko
hawana kazi ni muhimu katiba ikaribishe watu kama hao ili kuongeza nguvu zetu kiteknolojia na kifikra na kiubunifu.
xix. Katika kilimo katiba iweke misingi imara ya ujio wa mapinduzi ya kilimo na pia uundaji wa matrekta madogo kwa makubwa papa hapa nchini ili kuhakikisha
kwamba kilimo chetu hakitegemei mitambo na zana kutoka nje. Na zaidi ya hapo tunakuwa na nafasi nzuri ya kuuza kwingineko zana bora na rahisi za kilimo kwenye
nchi zinazotuzunguka. Ni muhimu katiba ifahamishe umma jinsi ambavyo maendeleo ya kilimo yatakavyosababisha idadi ya wakulima kupungua na watu wengi zaidi
kutegemea ajira nje ya kilimo na jinsi ya kujiandaa kwa majaliwa hayo.
xx. Katiba iamue kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi na wajumbe watakavyostahili kupatikana.
xxi. Katiba iweke miiko kwa jeshi, polisi, usalama wa taifa kuingiliwa au kuingizwa katika masuala ya kisiasa ikiwemo uchaguzi mkuu.
xxii. Katiba isaidie pia kufafanua haki na fidia za wale wanaolazimika kuachia kitu au vitu fulani, wanaoharibikiwa mali zao kutokana na uzembe wa mtu au shirika
fulani; wanaopata ajali au kupoteza kitu fulani. Fidia hiyo iwe kiasi kinachompa mtu unafuu wa kweli na anayeadhibiwa kuona uzito wa makosa zake na kuwa kama dawa
ya tabia zisizokubalika. Katika suala hili la fidia kusiwe na kinga kwa mtu au taasisi au idara yoyote ya serikali ili kuzuia uzembe na upuuzi katika maamuzi yetu wote.
xxiii. Ardhi katika katiba iendelee kuwa ni mali ya taifa. Hata hivyo, wananchi wote wawe na cheti cha umilikaji na wageni/wawekezaji waruhusiwe kukodisha ardhi
kwa miaka 33, 66 na 99 lakini wasiwe na ruksa ya kuuza. Yeyote anayefanya ujanja ashtakiwe, anyang'anywe na afukuzwe nchini.
Katiba iruhusu matumizi ya ardhi katika miji yetu kuboreshwa (urban upgrading), ikiwa ni pamoja na kuondoa baadhi ya mitaa ili kuwe na bustani na viwanja
vya kupumzika na michezo kwa watoto na vijana. Maeneo ya umma yawe ni kwa ajili ya matumzi kwa umma na vinginevyo iwe ni kosa na uhalifu mkubwa nchini.
xxiv. Katika katiba haki ya Mtanzania kuwa na nyumba ibainishwe waziwazi. Na mchango wa serikali, wizara na taasisi zake mbalimbali katika hili ufahamike. Pawe
na mifuko, benki na vyama vya kusaidia ujenzi wa nyumba kwa gharama nafuu. Ifikie wakati ambapo ni Watanzania wachache watakuwa wakizungumza mambo ya
ujenzi wa nyumba au kwenda saiti na vitu kama hivyo kwa sababu kutakuwa na makazi ya kutosha katika maeneo mbalimbali ya nchi na kazi kubwa itakayobakia ni
ukarabati na uboreshwaji.
xxv. Katiba iwe kichocheo cha madaktari, manesi, wahadhiri, walimu na wale wote ambao wanasoma kwa muda mrefu na kufanya kazi katika mazingira magumu
kulipwa vizuri kuliko wanasiasa. Tabia ya kuwalipa wanasiasa mishahara mizuri kuliko wale wanaojikunya kufanya kazi ngumu na muhimu nchini ndiyo iliyotufikisha hapa
tulipo leo.
xxvi. Katiba iweke wazi kiasi cha GDP kitakachotumika katika utafiti na maendeleo kwenye maeneo mbalimbali ili kuharakisha maendeleo ya nchi kitaalamu na
kitaaluma.
xxvii. Katiba iwe kichocheo cha matumizi ya vifaa na zana zisizo chakavu na hususan vile vya uchukuzi na usafiri. Ijulikane kabisa basi linatakiwa lisizidi miaka
mingapi kuwa barabarani, ndege na helikopta hewani miaka mingapi na meli baharini, mitoni na maziwani nazo zisiabiri zaidi ya miaka mingapi.
xxviii. Ni lazima pia katiba ianishe kuwa ni jukumu la kiongozi au viongozi wa juu kabisa kuhakikisha kuwa nchi yetu ina hali ya usafi na utunzaji mazingira wa
kuridhisha. Na kuwa kigezo kimoja cha uongozi bora kiwe ni usafi wa nchi na miji yake.
xxix. Sehemu zote za huduma ikiwemo mahoteli, maduka, mabaa lazima yawekewe katika katiba na sheria za nchi nguvu ya kikatiba kwamba huduma
zinazotolewa lazima ziendane na kule tunakotaka kuipeleka nchi, nikiwa na maana, lazima tufanane fanane na Uchina, Uarabuni, Ulaya, Marekani na sio vinginevyo. Hili
litasaidia sana nchi kuuzika kirahisi kama eneopendwa la watalii duniani. Hivi sasa tunashika nafasi ya nane duniani lakini hatua hizo zikichukuliwa upo uwezekano wa
kuwa 4.
XXXXXXXXX
kitilam@udsm.ac.tz
wazawa na watu wa nchi hii kwa ujumla.
Huu ni uwanja mpana na maoni yangu kijuujuu ni kwamba:
i. Katiba Ihakikishe ina vifungu toshelevu kuhusu haki za mtu (individual) ili jiji na miji yetu isiwe inatumia askari kuwafukuza machinga, mama ntilie na watu
wengine wanaotafuta riziki zao bila kueleweka watu hao wana haki gani. Yaani, mtu akifanya kosa ijulikane ni kosa moja kwa moja toka ndani ya katiba na sheria za
nchi. Na mtu akipewa upendeleo katiba ifichue kuna upendeleo waziwazi. Tusivumilie katu tabia ya kujengwa Vijiwe vya kina CCM mitaani na pale wakaruhusiwa
kuvunja sheria eti kwa kuwa wanaishabikia na 'kuitetea' CCM !
ii. Katiba lazima iwe very specific kwenye hali inayojitokeza nchini ambayo baadhi ya polisi na mahakimu wanaonekana kupiga bei au kuuza na kununua haki
za watu!
iii. Mamlaka ya rais yapunguzwe kwa kiasi kikubwa na ikiwezekana asilindwe pale atakapoonekana na viongozi wenzake kuwa kavunja sheria na katiba ya nchi.
iv. Jaji Mkuu atokane na majaji kadhaa watakaopendekezwa bungeni na kisha kuchaguliwa na bunge.
v. Kamanda mkuu wa polisi atokane na majaji kadhaa watakaopendekezwa bungeni na kisha kuchaguliwa na bunge.
vi. Mwanasheria Mkuu atokane na majaji kadhaa watakaopendekezwa bungeni na kisha kuchaguliwa na bunge.
vii. Katiba ifafanue maana ya Uchochezi na Uhaini katika mazingira ya mfumo wa vyama vingi na kila kitu kiwe bayana na kueleweka vyema na kukubalika na
wote. Tusikubali Watanzania fulani kuwaita wenzao wahaini na wachochezi kwa sababu Watanzania wenzao wamegundua wao ni wezi na mafisadi.
viii. Benki Kuu na Hazina lazima ishurutishwe na Katiba kutenga asilimia fulani katika kusaidia masikini na kuendeleza wazawa.
ix. Wakuu wa mikoa wasiteuliwe na rais bali wachaguliwe na wakazi wa mikoa husika ili kuwawajibisha ipasavyo katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
x. Mikoa iwe na Gavana au Waziri wake mkuu na baraza lake la mawaziri na wa wawakilishi wa mikoani watakaounda bunge la mkoa wakitokea kwenye watu wa
kuchaguliwa na wale wa kuwakilisha maslahi ya makundi mbalimbali katika jamii. Hili litaifanya mikoa kushindana katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi na hivyo
kuendelea kwa haraka zaidi kuliko ilivyo hivi sasa.
xi. Ruksa kwa vyama vya kisiasa kuungana kama ilivyo rahisi kwa watu wa kawaida kufunga ndoa wakati wowote wanapotaka.
xii. Kutoruhusu udikteta katika kundi au chama chochote cha kisiasa au kijamii na kadhalika.
xiii. Mkuu wa TUC (Tanzania University Commision) kupewa kazi na bunge na wakuu wa vyuo vikuu vyote kutathminiwa na kuchaguliwa na TUC!
xiv. Katika migodi na madini katiba itaje wazi utaratibu wa kumiliki, kukodi, kuchimba, kutengeneza vitu vinavyotokana na madini na kuviuza vitu hivyo kwa
manufaa ya wananchi. Lazima pia mipango iwepo ya kuiwezesha nchi hii kwanza kununua na kutengeneza mitambo muhimu kwa sekta husika ili wananchi wafaidi zaidi
mali asili yao. Taratibu hizo ni pamoja na kutaja mrabaha unaokubalika; mtawanyo wa umiliki kwa nchi za Mashariki na Marekani ya Kusini zaidi kuliko zile zilizozoeleka
za Magharibi.
Xv. Katika Umeme lazima katiba ieleze waziwazi aina ya umeme salama na bora kwa nchi na watu wasiwe wanaropoka ropoka tu kuhusu vitu kama umeme wa
nyuklia kwa nchi ambayo imeshindwa kusimamia vyema vitu vya kawaida; ikaja tokea viongozi wetu wanashawishika kuzalisha umeme huo hatari kwa maafa ya vizazi
vijanvyo.
xvi. Kuhusu maji ni lazima katiba iwe chimbuko la sheria ambazo zitakuwa kali na zisizo na huruma kuhusu kutunza vyanzo vya maji na vile vile kuhamasisha
ubunifu na matumizi mazuri ya maji toka kwenye maziwa yanayotuzunguka; bahari, mitoni, ardhini na yale yanayoletwa na mvua.
xvii. Kuhusu Utalii ni lazima katiba ioneshe waziwazi jinsi ambavyo wanavijiji na wanajamii mbalimbali bara na pwani watakavyonufaika na utalii badalal ya utalii
kunufaisha matajiri wachache wa nje na ndani. Ni lazima serikali iainishe mipango na mikakati ya wananchi pwani na bara kutumia ardhi, bahari na vivutio walivyo navyo
kama mtaji wao na hivyo kuhesabika kithamani na kifedha na kukubaliwa na wawekezaji kama uwekezaji wa thamani, halali na unaokubalika katika uendeshaji utalii na
mambo kama hayo.
xviii. Kuhusu viwanda ni muhimu katiba ichambue ndani-nje aina ya viwanda vinavyohitajika na jinsi tunavyoweza kuongeza thamani ya mazao, bidhaa, madini na
mali asili nyingine zetu ili tunufaike zaidi kiuchumi kuliko kunufaisha watu wa nje. Ni lazima kujipanga pia kikatiba na kuona kuwa tunazalisha mashine-mama na
mitambo-mama yote tunayoweza ili uendelezaji sekta ya viwanda uwe rahisi. Katika miaka hii ambayo wahandisi na wataalamu mbalimbali Ulaya, Asia na kwingineko
hawana kazi ni muhimu katiba ikaribishe watu kama hao ili kuongeza nguvu zetu kiteknolojia na kifikra na kiubunifu.
xix. Katika kilimo katiba iweke misingi imara ya ujio wa mapinduzi ya kilimo na pia uundaji wa matrekta madogo kwa makubwa papa hapa nchini ili kuhakikisha
kwamba kilimo chetu hakitegemei mitambo na zana kutoka nje. Na zaidi ya hapo tunakuwa na nafasi nzuri ya kuuza kwingineko zana bora na rahisi za kilimo kwenye
nchi zinazotuzunguka. Ni muhimu katiba ifahamishe umma jinsi ambavyo maendeleo ya kilimo yatakavyosababisha idadi ya wakulima kupungua na watu wengi zaidi
kutegemea ajira nje ya kilimo na jinsi ya kujiandaa kwa majaliwa hayo.
xx. Katiba iamue kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi na wajumbe watakavyostahili kupatikana.
xxi. Katiba iweke miiko kwa jeshi, polisi, usalama wa taifa kuingiliwa au kuingizwa katika masuala ya kisiasa ikiwemo uchaguzi mkuu.
xxii. Katiba isaidie pia kufafanua haki na fidia za wale wanaolazimika kuachia kitu au vitu fulani, wanaoharibikiwa mali zao kutokana na uzembe wa mtu au shirika
fulani; wanaopata ajali au kupoteza kitu fulani. Fidia hiyo iwe kiasi kinachompa mtu unafuu wa kweli na anayeadhibiwa kuona uzito wa makosa zake na kuwa kama dawa
ya tabia zisizokubalika. Katika suala hili la fidia kusiwe na kinga kwa mtu au taasisi au idara yoyote ya serikali ili kuzuia uzembe na upuuzi katika maamuzi yetu wote.
xxiii. Ardhi katika katiba iendelee kuwa ni mali ya taifa. Hata hivyo, wananchi wote wawe na cheti cha umilikaji na wageni/wawekezaji waruhusiwe kukodisha ardhi
kwa miaka 33, 66 na 99 lakini wasiwe na ruksa ya kuuza. Yeyote anayefanya ujanja ashtakiwe, anyang'anywe na afukuzwe nchini.
Katiba iruhusu matumizi ya ardhi katika miji yetu kuboreshwa (urban upgrading), ikiwa ni pamoja na kuondoa baadhi ya mitaa ili kuwe na bustani na viwanja
vya kupumzika na michezo kwa watoto na vijana. Maeneo ya umma yawe ni kwa ajili ya matumzi kwa umma na vinginevyo iwe ni kosa na uhalifu mkubwa nchini.
xxiv. Katika katiba haki ya Mtanzania kuwa na nyumba ibainishwe waziwazi. Na mchango wa serikali, wizara na taasisi zake mbalimbali katika hili ufahamike. Pawe
na mifuko, benki na vyama vya kusaidia ujenzi wa nyumba kwa gharama nafuu. Ifikie wakati ambapo ni Watanzania wachache watakuwa wakizungumza mambo ya
ujenzi wa nyumba au kwenda saiti na vitu kama hivyo kwa sababu kutakuwa na makazi ya kutosha katika maeneo mbalimbali ya nchi na kazi kubwa itakayobakia ni
ukarabati na uboreshwaji.
xxv. Katiba iwe kichocheo cha madaktari, manesi, wahadhiri, walimu na wale wote ambao wanasoma kwa muda mrefu na kufanya kazi katika mazingira magumu
kulipwa vizuri kuliko wanasiasa. Tabia ya kuwalipa wanasiasa mishahara mizuri kuliko wale wanaojikunya kufanya kazi ngumu na muhimu nchini ndiyo iliyotufikisha hapa
tulipo leo.
xxvi. Katiba iweke wazi kiasi cha GDP kitakachotumika katika utafiti na maendeleo kwenye maeneo mbalimbali ili kuharakisha maendeleo ya nchi kitaalamu na
kitaaluma.
xxvii. Katiba iwe kichocheo cha matumizi ya vifaa na zana zisizo chakavu na hususan vile vya uchukuzi na usafiri. Ijulikane kabisa basi linatakiwa lisizidi miaka
mingapi kuwa barabarani, ndege na helikopta hewani miaka mingapi na meli baharini, mitoni na maziwani nazo zisiabiri zaidi ya miaka mingapi.
xxviii. Ni lazima pia katiba ianishe kuwa ni jukumu la kiongozi au viongozi wa juu kabisa kuhakikisha kuwa nchi yetu ina hali ya usafi na utunzaji mazingira wa
kuridhisha. Na kuwa kigezo kimoja cha uongozi bora kiwe ni usafi wa nchi na miji yake.
xxix. Sehemu zote za huduma ikiwemo mahoteli, maduka, mabaa lazima yawekewe katika katiba na sheria za nchi nguvu ya kikatiba kwamba huduma
zinazotolewa lazima ziendane na kule tunakotaka kuipeleka nchi, nikiwa na maana, lazima tufanane fanane na Uchina, Uarabuni, Ulaya, Marekani na sio vinginevyo. Hili
litasaidia sana nchi kuuzika kirahisi kama eneopendwa la watalii duniani. Hivi sasa tunashika nafasi ya nane duniani lakini hatua hizo zikichukuliwa upo uwezekano wa
kuwa 4.
XXXXXXXXX
kitilam@udsm.ac.tz
Sunday, February 6, 2011
Dini na Katiba:
Katiba lazima ibainishe wazi haki na uhuru wa waumini wa dini mbalimbali:
. Je, kila dini inaruhusiwa kuendesha imani zao kwa mujibu wa mafundisho na urithi wao?
. Waislamu wanastahili mahakama ya kdhai?
. Je, kuna chombo chochote cha dini chenye haki ya kuwa na ukiritimba juu ya waumini wa dini au madhehebu fulani? Au kuna uhuru na haki ya kila waumini kuchagua wawe chini ya taasisi gani ya kidini au kimadhehebu?
. Je, dini zina haki ya kuunganisha waumini wa nchi moja na nchi nyingine ili kuwa na mwamvuli mmoja, kwa mfano, Jumuiya ya Wapentakoste au Waislamu wa Afrika Mashariki au Afrika?
. Je, nini haki za dini juu ya wale wanaojenga mabaa na kumbi za starehe au gesti hausi karibu na nyumba zao za ibada ?
. Wanyama ambao ni haramu kwa dini nyingine wanafugwa katika mazingira gani na wale ambao wanyama hao sio haramu?
. Nini haki ya dini moja katika kutumia kitabu au waumini wa dini nyingine kuponda dini fulani?
. Nini haki ya waumini na viongozi wao katika mihadhara na mikutano nje ya nyumba zao za ibada?
. Nini haki ya kila dini kuwa na gazeti, redio na televisheni yake pamoja na biashara zingine? Na serikali isaidieje? Na je televisheni na redio ya taifa itumiwe na dini kwa kiasi gani? Na uwakilishi katika bodi za vyombo hivyo uwe vipi?
. Nini haki ya kila dini kuwa na shule na hospitali na taasisi hizo zipate nini toka serikalini?
. Nani awajibike kuboresha utendaji kazi na menejimenti ya taasisi za kidini?
. Fedha za misaada kwa Waislamu toka nje zirahisishwe vipi kuwafikia na kufanywa yale yanayotakiwa kufanyika bila kuonekana ni fedha za haramu au za kigaidi?
. Je, Siku ya Ijumaa iwe ya Mapumziko kwa Waislamu? Na Jumamosi kwa Wasabato?
Na je, ni haki kuzitumia siku za Ijumaa na Jumamosi kuendesha mikutano wakati ni siku za ibada kwa baadhi ya waumini?
. Je, sherehe za Kiislamu zitambulike kama siku za Mapumziko? Siku gani? Siku ngapi?
. Je, Kalenda ya Kiislamu iambatanishwe katika kalenda za Kirumi au Kizungu?
. Nini kifanyike ili Waislamu waweze kusoma kwa Kiarabu na sio Kiingereza au Kiswahili tu shule za msingi, sekondari na kuendelea ili baadaye iwe rahisi kwao kwenda kujiendeleza katika nchi za Kiarabu?
. Nini kifanyike ili kuona kuwa shule, hospitali na huduma zingine za mashirika ya kidini haziwanyonyi wananchi au kutoa huduma duni kuliko inavyotakiwa na kisha fedha hizo kuliwa na wachache au kwenda kufanya mambo yasiyohusiana na shule husika?
. Je, kila dini inaruhusiwa kuendesha imani zao kwa mujibu wa mafundisho na urithi wao?
. Waislamu wanastahili mahakama ya kdhai?
. Je, kuna chombo chochote cha dini chenye haki ya kuwa na ukiritimba juu ya waumini wa dini au madhehebu fulani? Au kuna uhuru na haki ya kila waumini kuchagua wawe chini ya taasisi gani ya kidini au kimadhehebu?
. Je, dini zina haki ya kuunganisha waumini wa nchi moja na nchi nyingine ili kuwa na mwamvuli mmoja, kwa mfano, Jumuiya ya Wapentakoste au Waislamu wa Afrika Mashariki au Afrika?
. Je, nini haki za dini juu ya wale wanaojenga mabaa na kumbi za starehe au gesti hausi karibu na nyumba zao za ibada ?
. Wanyama ambao ni haramu kwa dini nyingine wanafugwa katika mazingira gani na wale ambao wanyama hao sio haramu?
. Nini haki ya dini moja katika kutumia kitabu au waumini wa dini nyingine kuponda dini fulani?
. Nini haki ya waumini na viongozi wao katika mihadhara na mikutano nje ya nyumba zao za ibada?
. Nini haki ya kila dini kuwa na gazeti, redio na televisheni yake pamoja na biashara zingine? Na serikali isaidieje? Na je televisheni na redio ya taifa itumiwe na dini kwa kiasi gani? Na uwakilishi katika bodi za vyombo hivyo uwe vipi?
. Nini haki ya kila dini kuwa na shule na hospitali na taasisi hizo zipate nini toka serikalini?
. Nani awajibike kuboresha utendaji kazi na menejimenti ya taasisi za kidini?
. Fedha za misaada kwa Waislamu toka nje zirahisishwe vipi kuwafikia na kufanywa yale yanayotakiwa kufanyika bila kuonekana ni fedha za haramu au za kigaidi?
. Je, Siku ya Ijumaa iwe ya Mapumziko kwa Waislamu? Na Jumamosi kwa Wasabato?
Na je, ni haki kuzitumia siku za Ijumaa na Jumamosi kuendesha mikutano wakati ni siku za ibada kwa baadhi ya waumini?
. Je, sherehe za Kiislamu zitambulike kama siku za Mapumziko? Siku gani? Siku ngapi?
. Je, Kalenda ya Kiislamu iambatanishwe katika kalenda za Kirumi au Kizungu?
. Nini kifanyike ili Waislamu waweze kusoma kwa Kiarabu na sio Kiingereza au Kiswahili tu shule za msingi, sekondari na kuendelea ili baadaye iwe rahisi kwao kwenda kujiendeleza katika nchi za Kiarabu?
. Nini kifanyike ili kuona kuwa shule, hospitali na huduma zingine za mashirika ya kidini haziwanyonyi wananchi au kutoa huduma duni kuliko inavyotakiwa na kisha fedha hizo kuliwa na wachache au kwenda kufanya mambo yasiyohusiana na shule husika?
Monday, January 31, 2011
Makazi ya Watu, Mabaa na Ustaarabu
KUMEZUKA mtindo wa viongozi na watendaji katika ngazi za chini kudharau imani misimamo ya wakazi mitaani kitu ambacho kinaashiria kuhatarisha umoja na amani nchini.
Baa, vilabu na maeneo mengine ya starehe kwa upande wa Waislamu, Walokole na watu wa dini nyingine wanaopenda kulea watoto wao katika maadili yanayokubalika visijengwe hadi wakazi wote wameridhia.
Serikali za mitaa hazina sauti kuliko wakazi wa mitaa husika. Na uroho na ulafi wa viongozi usiwe chimbuko la kuwageuza wananchi kuwa wavunja sheria na katiba wakati ni viongozi na mabwana zao ndio wanaovunja katiba.
Kwa mfano hili la ujenzi wa baa na vilabu vya starehe na ngono ovyo ovyo kila mahala kiasi kwamba sasa inakuwa ni vigumu kwa wakazi mitaani kulala na kupumzika kwa amani. Juu ya hili unaongezewa magari yanayopita mitaani na makelele na promosheni za kijinga na zisizoendana na maadili ya Watanzania.
Ni lazima katiba imlinde mwananchi wa kawaida na sio matajiri na wenye fedha na viongozi na hasa wale wenye mabaa na vilabu vya starehe!
Hadidu:
. Baa zijengwe karibu na misikiti, kanisa na makazi ya watu?
. Maduka ya Pombe na Baa ziwepo kwenye maeneo ya watu wenye imani zinazokataza vitu hivyo?
. Kuwe na utaratibu gani wa kuzuia polusheni ya sauti na makelele watu wasiyotaka kusikia?
. Ni nani aruhusu ujenzi wa baa karibu na makazi ya wananchi? Wananchi wenyewe au maofisa serikali na viongozi wa vyama waroho na walafi?
. Malaya waendeshe biashara zao kwa utaratibu gani na mahala gani?
. Wasenge na mabaasha wawe na haki gani katika jamii ya Kitanzania?
. Baa ziruhusiwe kuwa kwenye maeneo ya wazi na kuwatamanisha watoto na vijana wa waumini ambao kwao ni haramu?
Baa, vilabu na maeneo mengine ya starehe kwa upande wa Waislamu, Walokole na watu wa dini nyingine wanaopenda kulea watoto wao katika maadili yanayokubalika visijengwe hadi wakazi wote wameridhia.
Serikali za mitaa hazina sauti kuliko wakazi wa mitaa husika. Na uroho na ulafi wa viongozi usiwe chimbuko la kuwageuza wananchi kuwa wavunja sheria na katiba wakati ni viongozi na mabwana zao ndio wanaovunja katiba.
Kwa mfano hili la ujenzi wa baa na vilabu vya starehe na ngono ovyo ovyo kila mahala kiasi kwamba sasa inakuwa ni vigumu kwa wakazi mitaani kulala na kupumzika kwa amani. Juu ya hili unaongezewa magari yanayopita mitaani na makelele na promosheni za kijinga na zisizoendana na maadili ya Watanzania.
Ni lazima katiba imlinde mwananchi wa kawaida na sio matajiri na wenye fedha na viongozi na hasa wale wenye mabaa na vilabu vya starehe!
Hadidu:
. Baa zijengwe karibu na misikiti, kanisa na makazi ya watu?
. Maduka ya Pombe na Baa ziwepo kwenye maeneo ya watu wenye imani zinazokataza vitu hivyo?
. Kuwe na utaratibu gani wa kuzuia polusheni ya sauti na makelele watu wasiyotaka kusikia?
. Ni nani aruhusu ujenzi wa baa karibu na makazi ya wananchi? Wananchi wenyewe au maofisa serikali na viongozi wa vyama waroho na walafi?
. Malaya waendeshe biashara zao kwa utaratibu gani na mahala gani?
. Wasenge na mabaasha wawe na haki gani katika jamii ya Kitanzania?
. Baa ziruhusiwe kuwa kwenye maeneo ya wazi na kuwatamanisha watoto na vijana wa waumini ambao kwao ni haramu?
Zanzibar, Mikoa na Katiba
Zanzibar yenye wapiga kura laki nne tu iweje iwe na rais, waziri mkuu na baraza la mawaziri wakati mikoa yenye idadi kubwa mata tatu au nne ya hiyo huku bara haina mfumo huo?
. Je, katiba haistahili kuwa na kifungu juu ya mfumo na muundo mpya wa serikali za mikoa ?
. Badala ya kuwa tu serikali za mikoa serikali hizo zikawa ni serikali huru kiuchumi na kijamii?
. Je, serikali hizo huru za mkoa kiuchumi na kijamii hazitakuwa bora kuliko kuwa na Mkuu wa Mkoa ambaye aghalabu ni CCM pigaua? Si mwenye uchungu na mkoa? Huichukulia nafasi yake ya uongozi kama njia ya kujitajirisha kibinafsi na kukinufaisha chama chake kisiasa ?
. Waziri Mkuu wa Mkoa atakuwa mkazi wa mkoa husika, mwenye uchungu na mkoa wake na watu wake na atatoka kwenye chama chenye wabunge wengi kimkoa?
. Bunge litaundwa na wabunge wa kitaifa na wabunge toka makundi yote makuu kijamii na kiuchumi mkoani?
. Mawaziri wa mkoa watatokana na wabunge hao? Na mbunge akishachaguliwa waziri ataachia nafasi ya ubunge ili kufanya kazi zake bila upendeleo ?
. Je, kwa namna hii taifa halitanufaika kwa sababu mikoa yote itakuwa ni shule za viongozi wa aina mbalimbali ? Na kwamba mawaziri wa kitaifa itakuwa ni nadra kuwa watu ambao hawakuwa mawaziri katika ngazi ya mkoa?
. Je ni muundo wa kuwa na Mkuu wa Mkoa wa Kichama au kuwa na Waziri Mkuu, Mawaziri na Wabunge kutakakoharakisha maendeleo ya mkoa na wakazi wake haraka ?
. Je, katiba haistahili kuwa na kifungu juu ya mfumo na muundo mpya wa serikali za mikoa ?
. Badala ya kuwa tu serikali za mikoa serikali hizo zikawa ni serikali huru kiuchumi na kijamii?
. Je, serikali hizo huru za mkoa kiuchumi na kijamii hazitakuwa bora kuliko kuwa na Mkuu wa Mkoa ambaye aghalabu ni CCM pigaua? Si mwenye uchungu na mkoa? Huichukulia nafasi yake ya uongozi kama njia ya kujitajirisha kibinafsi na kukinufaisha chama chake kisiasa ?
. Waziri Mkuu wa Mkoa atakuwa mkazi wa mkoa husika, mwenye uchungu na mkoa wake na watu wake na atatoka kwenye chama chenye wabunge wengi kimkoa?
. Bunge litaundwa na wabunge wa kitaifa na wabunge toka makundi yote makuu kijamii na kiuchumi mkoani?
. Mawaziri wa mkoa watatokana na wabunge hao? Na mbunge akishachaguliwa waziri ataachia nafasi ya ubunge ili kufanya kazi zake bila upendeleo ?
. Je, kwa namna hii taifa halitanufaika kwa sababu mikoa yote itakuwa ni shule za viongozi wa aina mbalimbali ? Na kwamba mawaziri wa kitaifa itakuwa ni nadra kuwa watu ambao hawakuwa mawaziri katika ngazi ya mkoa?
. Je ni muundo wa kuwa na Mkuu wa Mkoa wa Kichama au kuwa na Waziri Mkuu, Mawaziri na Wabunge kutakakoharakisha maendeleo ya mkoa na wakazi wake haraka ?
Subscribe to:
Posts (Atom)