Zanzibar yenye wapiga kura laki nne tu iweje iwe na rais, waziri mkuu na baraza la mawaziri wakati mikoa yenye idadi kubwa mata tatu au nne ya hiyo huku bara haina mfumo huo?
. Je, katiba haistahili kuwa na kifungu juu ya mfumo na muundo mpya wa serikali za mikoa ?
. Badala ya kuwa tu serikali za mikoa serikali hizo zikawa ni serikali huru kiuchumi na kijamii?
. Je, serikali hizo huru za mkoa kiuchumi na kijamii hazitakuwa bora kuliko kuwa na Mkuu wa Mkoa ambaye aghalabu ni CCM pigaua? Si mwenye uchungu na mkoa? Huichukulia nafasi yake ya uongozi kama njia ya kujitajirisha kibinafsi na kukinufaisha chama chake kisiasa ?
. Waziri Mkuu wa Mkoa atakuwa mkazi wa mkoa husika, mwenye uchungu na mkoa wake na watu wake na atatoka kwenye chama chenye wabunge wengi kimkoa?
. Bunge litaundwa na wabunge wa kitaifa na wabunge toka makundi yote makuu kijamii na kiuchumi mkoani?
. Mawaziri wa mkoa watatokana na wabunge hao? Na mbunge akishachaguliwa waziri ataachia nafasi ya ubunge ili kufanya kazi zake bila upendeleo ?
. Je, kwa namna hii taifa halitanufaika kwa sababu mikoa yote itakuwa ni shule za viongozi wa aina mbalimbali ? Na kwamba mawaziri wa kitaifa itakuwa ni nadra kuwa watu ambao hawakuwa mawaziri katika ngazi ya mkoa?
. Je ni muundo wa kuwa na Mkuu wa Mkoa wa Kichama au kuwa na Waziri Mkuu, Mawaziri na Wabunge kutakakoharakisha maendeleo ya mkoa na wakazi wake haraka ?
No comments:
Post a Comment